Thursday, June 23, 2016

SPIKA AFUTURISHA WABUNGE JIONI YA LEO MJINI DODOMA

 Waziri Mkuu wa Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akifurahia Jambo na Mbunge wa Ilala Azzan Zungu wakati wa futari iliyoandaliwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai  kwa ajili ya wabunge leo katika viwanja vya Bunge Mjini Dodoma.
 Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akishiriki futari iliyoandaliwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ajili ya wabunge, kulia ni Naibu Spika Dkt. Tulia Ackson.
 Wabunge wakishiriki futari kwenye viwanja vya Bunge jioni ya leo Mjini Dodoma.
 Wabunge wakichukua futari iliyoandaliwa na Spika wa Bunge katika viwanja vya Bunge, Mjini Dodoma
 Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akitoka kuchukua futari iliyoandaliwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai jioni ya leo katika viwanja vya Bunge.
 Wabunge wakifurahia futari iliyoandaliwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mhe. Job Ndugai.
Wabunge wakifurahia futari iliyoandaliwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mhe. Job Ndugai.

No comments: