Friday, June 17, 2016

RC WA MWANZA MHE JOHN MONGELLA APOKEA GARI LA WAGONJWA

 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella, akizungumza na watumishi kabla yakupokea msaada wa gari la wagonjwa.
 Mkuu wa mkoa akikata Utepe kuashiria uzinduzi wa mapokezi ya Gari la Wagonjwa kutoka Rafiki Surgical Mission.
 Balozi  Issaya Chialo alipokuwa akitoa maelezo mafupi juu ya msaada wa gari la wagonjwa walilo likabidhi kwa hospitali ya Mkoa wa Mwanza.
 Watumishi katika hospitali ya Mkoa wa Mwanza, wakimasikiliza kwa makini mkuu wa mkoa wa Mwanza hayupo pichani, wakati wa hafla fupi yakukabidhi gari hilo.
 Mganga mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt. Subi, akitoa maelezo ya awali kuhusu huduma za afya katika mkoa wa Mwanza wakati wa hafla hiyo ya makabidhiano.
 Wananchi wanao hudumiwa katika hospitali hiyo ya mkoa nao hawakuwa nyuma katika hilo, hapo wakisiliza kwa makini maelezo ya mkuu wa mkoa.
 Katibu Tawala wa Wilaya ya Nyamagana, Bi Maricella, akimkaribisha mkuu wa mkoa wa Mwanza.
 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella, akikabidhi cheti cha Shukrani kwa Balozi Issaya Chialo, kama sehemu ya shukrani kwa kutambua mchango wa Rafiki Surgical Mission, walio utoa kwa Mkoa huo wa Gari la Wagonjwa.
Hilo ndilo gari lililotolewa na Rafiki Surgical Mission.
(Habari na picha zote na Afisa habari wa mkoa wa Mwanza)

No comments: