Tuesday, June 21, 2016

BENKI YA NBC YANDAA FUTARI KWA WATEJA WAKE WA DAR NA MTWARA

 Ofisa Mwendeshaji Mkuu wa Benki ya NBC Tanzania, James Kinyanyi (wa pili kushoto), Mkuu wa Huduma Rejereja za Kibenki wa benki hiyo, Musa Jallow (wa pili kulia), pamoja na baadhi ya wateja wa benki hiyo wakishiriki mlo wa futari iliyoandaliwa na NBC kwa wateja wake jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
 Mjumbe wa Bodi ya Benki ya NBC, Dk. Kassim Hussein (kushoto), akisalimiana na mmoja wa wateja wao, Ibrahim Shaddad katika hafla ya futari iliyoandaliwa na NBC kwa wateja wao jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mkuu wa Huduma Rejareja za Kibenki wa benki hiyo, Musa Jallow.
 Baadhi ya wateja wa Benki ya NBC na wafanyakazi wa benki hiyo, wakishiriki mlo wa futari iliyoandaliwa na NBC jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wateja wa Benki ya NBC jijini Dar es Salaam na wafanyakazi wa benki hiyo, wakishiriki mlo wa futari iliyoandaliwa na NBC jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Kitengo cha Islamic Banking cha Benki ya NBC, Yassir Masoud (kulia) akishikana mikono na Sheikh wa mkoa huo na Naibu Kadhi wa Mtwara,  sheikh Nurdin Mangochi.
 Baadhi ya wateja wa Benki ya NBC jijini Mtwara na wafanyakazi wa benki hiyo, wakishiriki mlo wa futari iliyoandaliwa na NBC mkoani humo hivi karibuni.

No comments: