Thursday, June 2, 2016

Benki ya Barclays yatoa msaada wa madawati 70 Handeni.

 Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martin Shigela (kushoto) akipokea sehemu ya madawati 70  kutoka kwa  Meneja Masoko  wa Benki ya B arclays Tanzania  (BBT) Nasikiwa Berya  yaliyotolewa ba benki hiyo kusaidia  Shule ya Sekondari Handeni kupitia timu yake ya soka iliyopewa jina la ‘Blue Eagle’ ikiwa ni sehemu ya juhudi za benki hiyo katika kusaidia jamii. Hafla ya makabidhiano ilifanyika wilayani Handeni mkoani Tanga hivi karibuni.
 Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martin Shigela (kushoto), akikabidhi madawati hay kwa baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari Handeni wilayani humo hivi karibuni. 
 Meneja Masoko  wa Benki ya B arclays Tanzania  (BBT) Nasikiwa Berya (watatu kushoto), akikabidhi sehemu ya  msaada wa madawati 70 kwa Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari handeni, Amani Mmbaga, yaliyotolewa na benki kupitia timu yake ya soka iliyopewa jina la ‘Blue Eagle’ ikiwa ni sehemu ya juhudi za benki hiyo katika kusaidia jamii. Hafla ya makabidhiano ilifanyika wilayani Handeni mkoani Tanga .  
 Mmoja wa maofisa wa Benki ya Barclays Tanzania, Raymond Bunyinyiga (kushoto), akizungumza na wanafunzi wa shule hiyo.  
 Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya Barclays wakibeba madawati tayari kuyakabidhi kwa mkuu wa mkoa wa Tanga kusaidia shule za sekondari wilayani Handeni.
Mchezaji wa timu ya soka ya Benki ya Barclays iitwayo ‘Blue Eagle’ Edwin Makata, akichuana na Issa Silaji (kulia) wa timu ya soka ya Shule ya Sekondari Handeni, katika mchezo wa kirafiki mara baada ya kukabidhi msaada wa madawati 70 yaliyotolewa na timu hiyo.

No comments: