Thursday, May 12, 2016

ZANZIBAR YASHEREHEKEA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI

Brasbendi ya Chipkizi ikiongoza matembezi ya wauguzi yakipita katika maeneo ya Kisonge kuelekea Studio za Rahaleo ambapo sherehe hizo ziliadhimishwa rasmi.
Waandamanaji wakiingia kwa furaha eneo la Studio za Rahaleo ambapo sherehe za sikuya Waguzi Duniani ziliadhimishwa.
Mrajis Baraza la Wauguzi na Wakunga Zanzibar Vuai Kombo Haji akiongoza kiapo cha wauguzi katika maadhimisho ya siku ya wauguzi Duniani yaliyofanyika Ukumbi wa Sanaa Rahaeo.
Mkurugenzi Tiba Katika Wizara ya Afya Dkt. Salhia Ali Muhsin akimkaribisha mgeni rasmi Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo aliemwakilishi Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein katika maadhimisho hayo.
Baadhi ya wauguzi walioshiriki maadhimisho hayo wakifuatilia hotuba zilizokuwa zikitolewa katika Ukumbi wa Sanaa Rahaleo, Mjini Zanzibar.
Waziri wa Afya Mhmoud Thabit Kombo aliemuwakilisha Mke wa Rais wa Zanzibar akisoma hotuba katika maadhimisho ya siku ya wauguzi Duniani yaliyofanyika Ukumbi wa Sanaa Rahale Mjini Zanzibar.
Picha ya pamoja ya baadhi ya viongozi wa wauguzi na Mgeni rasmi, Waziri wa Afya Mhmoud Thabit Kombo. Picha na Makame Mshenga Maelezo Zanzibar.

No comments: