Saturday, May 7, 2016

YANGA YAWATUNGUA WAANGOLA BAO 2-0 TAIFA LEO

Wachezaji wa Timu ya Yanga, Juma Abdul (kushoto) na Simon Msuva (kulia) kwa pamoja wakishangilia baada ya kupata goli la pili lililotiwa kimiani na Matheo Anthony (kati), wakati wa Mchezo wa Makundi wa Kombe la Shirikisho Barani Afrika dhidi ya GD Sagrada Esperanca ya nchini Angola, uliopigwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es salaam. Yanga imeshinda bao 2-0.
Beki wa Yanga, Juma Abdul, akijaribu kumtoka Mchezaji wa Timu ya GD Sagrada Esperanca ya nchini Angola, katika mchezo uliopigwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es salaam. Yanga imeshinda bao 2-0.
Mshambuliaji wa Yanga, Simon Msuva, akiipachikia timu yake bao la kuongoza wakati wa Mchezo wa Makundi wa Kombe la Shirikisho Barani Afrika dhidi ya GD Sagrada Esperanca ya nchini Angola, uliopigwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es salaam. Yanga imeshinda bao 2-0.
 Mshambuliaji wa Timu ya Yanga, Amisi Tambwe, pamoja na Beki wa Timu ya GD Sagrada Esperanca ya nchini Angola, wakiwania mpira wa juu, wakati wa Mchezo wa Makundi wa Kombe la Shirikisho Barani Afrika dhidi ya GD Sagrada Esperanca ya nchini Angola, uliopigwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es salaam. Yanga imeshinda bao 2-0.
Mchezaji wa Yanga, Matheo Anthony akipiga shuti kali lililopelekea Goli la pili, katika Mchezo wa Makundi wa Kombe la Shirikisho Barani Afrika dhidi ya GD Sagrada Esperanca ya nchini Angola, uliopigwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es salaam. Yanga imeshinda bao 2-0.

Kipa wa tiku ya GD Sagrada Esperanca ya nchini Angola, Roadro Juan Da Semero akiusindikiza mpira kwa macho ulipokuwa ukiingia langoni kwake, ikiwa ni mkwaju mkali uliopigwa na Matheo Anthony wa Yanga.
















No comments: