Thursday, May 19, 2016

SIKU YA MAKUMBUSHO DUNIANI YAFANYIKA ZANZIBAR


Waziri wa Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo Rshid Ali Juma akizungumza na wafanyakazi na wananchi walioshiriki maonyesho ya sanaa katika maadhimisho ya siku ya Makumbusho Duniani yaliyofanyika Makumbusho ya Mnazi mmoja Zanzibar.


Waziri wa Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo Rashid Ali Juma akikata utepe kuashiria ufunguzi wa Maonyesho ya kudumu ya sanaa katika maadhimisho ya Makumbusho Duniani yaliyofanyika Makumbusho ya Mnazimmoja Mjini Zanzibar.

Mkuu wa Divisheni ya Makumbusho kutoka Idara ya Mkumbusho na Mambo ya Kale Khamis Abdalla akisoma risala ya wafanyakazi wa Idara hiyo katika ufunguzi wa maonyesho ya sanaa ikiwa ni maadhimisho ya siku ya Makumbisho Duniani yaliyofanyika Makumbusho ya Mnazimmoja Zanzibar.

Baadhi ya viongozi wa Wizara na wageni waalikwa waliohudhuria ufunguzi wa maonyesho ya sanaa katika maadhimisho ya siku ya Makumbusho Duniani yaliyofanyika Mnazimmoja Mjini Zanzibar wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi.
Mkuu wa Divisheni ya Makumbusho Zanzibar Khamis Abdalla akimuonyesha Waziri wa Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo sanaa ya ufumaji kofia za asili ya Zanzibar katika maonyesho ya sanaa yanayofanyika makumbusho ya Mnazimmoja.

Waziri wa Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo Rashid Ali Juma akiangalia kazi ya ubunifu iliyofanywa na msanii Naaman Ali Khamis wa kwanza (kulia) anaetumia majani makavu ya migomba.Picha na Makame Mshenga/Maelezo Zanzibar.

No comments: