Tuesday, May 17, 2016

RC KILIMANJARO AFANYA ZIARA KATIKA MAGHALA NA MADUKA YA MARENGA INVESTMENT KUJIONEA HALI YA TATIZO LA SUKARI


Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Sadicky akiwasili katika ghala la kuhifadhia bidhaa la Kampuni ya Marenga Investment alipofanya ziara ya ghafla kwa lengo la kujionea hali ya upungufu wa sukari pamoja na kufanya ukaguzi mwingine.aliiongozana nao ni kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro,Wilbroad Mutafungwa na Mkuu wa wilaya ya Moshi,Novatus Makunga.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Sadicky akiwa katika ghala la kuhifadhia bidhaa mbalimbali la kampuni ya Marenga Investment.kulia ni kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro Wilbroad Mutafungwa.
Mifuko ya Sukari iliyopo katika ghala hilo.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Sadicky akiwana Mkuu wa wilaya ya Moshi,Novatus Makunga na Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro,Wilbroad Mutafungwa wakimngojea mmiliki wa Ghala hilo.
Sehemu ya Sukari inayozalishwa na kampuni ya sukari ya TPC ikiwa katika mifuko ya kilogramu 2.
Sehemu ya bidhaa ya unga ikiwa katika Ghala hilo.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Sadicky akibadilishana mawazo na Mkuu wa wilaya Novatus Makunga na Kamanda wa Polisi ,Wilbroad Mutafungwa wakati wakimngojea mmiliki wa ghala hilo.
Mmilikiwa ghala la kuihifadhia bidhaa za kampuni ya Marenga Investment,Joseph Kimosso (katikati) akizungumza jambo na Mkuu wa mkoa Saidi Mecky Sadicky mara baada ya kuwasili katika ghala hilo.
Sehemu ya Mchele ukiwa katika gunia .
Mmiliki wa Ghala la kuhifadhia bidhaa mbalimbali za kampuni ya Marenga Investment,Joseph Kimosso akiumuongoza Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ,Said Mecky Sadicky kutembelea maeneo zilipohifadhiwa bidhaa mbalimbali.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Sadicky akitembelea kukagua ghala la kampuni ya Marenga.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Sadicky akikagua moja ya bidhaa ili kujua endapo muda wake wa matumizi umemalizika ama la.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Sadicky akikagua sukari ilifungwa katika mfuko maalum ya uzito wa Kg 2 alipotembelea Super Market ya Marenga iliyopo Kiboriloni mjini Moshi.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Sadicky akizungumza na wateja waliofika katika duka la Marenga kwa ajili ya kununua Sukari.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Sadicky akitoka katika Duka la Marenga Investment.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Sadicky akiagana na mmiliki wa kampuni ya Marenga Investment ,Joseph Kimosso baada ya kutembelea Maduka ya kampuni hiyo pamoja na kufanya ukaguzi katika maghara ya kampuni hiyo.
Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

No comments: