Wednesday, May 11, 2016

KIKAO CHA SAA TANO NZIMA KUJADILI MUSTAKABAL NA MUUNGANO WA WATANZANIA UINGEREZA

Habari na Picha za Freddy Macha, London 1- Nembo ya muda ya Jumuiya - pic by F Macha 2016 Nembo iliyopendekezwa...

Jumamosi Mchana 7 Aprili ilikuwa siku ya jua kali Uingereza. Wananchi wengi walijazana bustanini au sehemu za starehe wakiota jua na kula barafu za sukari yaani "Ice Cream." Magari yalipiga honi, wenyeji waliheushwa na ujoto ujoto huu adimu mazingira ya Ulaya. Ndani ya ofisi ya Ubalozi wa Tanzania London, kundi la Watanzania wanane lilikaa mchana wote likijadili (kwa ari na mori) maslahi ya wananchi wenzao Uingereza.
2- Kikao kikiwa motomoto- pic by F Macha 2016 Chini ya uenyekiti wa Bi Mariam Kilumanga Kikosi Kazi (Task Force – UK, juu pichani) kilichoundwa na Balozi wa zamani Uingereza Mhe Peter Kallaghe, kabla hajamaliza wakati wake hakikulegeza kamba. Mazungumzo makali yaliangalia kuhusu katiba mpya yrnyr kurasa 16. Itafanyiwa marekebisho kusimamia Jumuiya Mpya ya Watanzania Uingereza. Moja ya matumaini yake ni kuunganisha na kuendeleza maisha ya wananchi wetu nje ili kuwafaidi wao na walioko nyumbani. Hebu tazama picha na video uone taswira ilivyokuwa... 3-Mariam Kilumanga - Mwenyekiti - pic by F Macha 2016 Mwenyekiti Mariam Kilumanga, akihimiza jambo. Bi. Kilumanga ni pia mwenyekiti wa muda mrefu wa Chama cha Kina Mama Watanzania Uingereza , TAWA. Anaipenda sana nchi, dada huyu. 4- Michael Semuguruka- Mjumbe - pic by F Macha 2016 Michael Semuguruka, mkazi wa LondoN Mashariki, ni kati ya wajumbe 12 wanaojitolea wakati wao kwa shughuli hii. ... 5- Cleopa John na Respigy Peter Michael Ubalozini- pic by F Macha 2016 Katibu Mkuu, Cleopa John (kulia) na mjumbe Respigy Peter Michael ndani ya kikao. Akili zinazotoa cheche. 6- Jane Ngereza - Mjumbe- pic by F MachaJane Ngereza, Mmoja wa wajumbe na kati ya wanawake watano ndani ya kikosi hiki kisichotaka kubabaisha watu. Alisafiri toka Birmingham kuhudhuria kikao London. 7-Daniel Semwenda akijadili moja ya vipengele- pic by F Macha 2016Daniel Semwenda, mjumbe asiyecheka cheka ovyo, akichangia hoja. 8- Vijana wenye nidham - Surur na Mgetta- pic by F MachaVijana , Said Surur na Renatus Mgetta, wenye bidii, nidhamu, uzalendo na azma ya kuunganisha Watanzania. Uzalendo kitu adimu simu siku hizi Afrika. 9- Ubalozi wa Tanzania - London- pic by F Macha 2016Taswira ya Ubalozi wa Tanzania, mtaa wa Bond Street, katikati ya London. Ubalozi ulimlipa mlinzi wake, fedha za OVATAIM, kuwasubiri wazalendo hawa kuumiza vichwa. WAJUMBE AMBAO HAWAKUWEPO KATIKA KIKAO
  1. Raymond Binya
  2. Henry Kimani
  3. Brian Ngerangera
  4. Jackson Msuku
  5. Sabrina Karim
  6. Lucile Shigikile
  7. Peter Gabagambi
  8. Jane Kimani
  9. Amos Msanjila - Afisa Balozi , mhusika, aliyekuwepo halafu akaendelea na shughuli nyingine za Ubalozini.
SIKILIZA UFAFANUZI ZAIDI https://youtu.be/P76coQOLM98 Katibu... https://youtu.be/izA1IWHWeuI Naibu Mwenyekiti... https://youtu.be/Y_0Po4Inp4o Katibu Mwenezi... https://youtu.be/U3OwiI3_K-I Mjadala mkali kutafuta ufafanuzi haklka wa Katiba ...

No comments: