Monday, April 18, 2016

MWILI WA MAREHEMU HENRY KIHERILE WAAGWA HOUSTON, TEXAS

Jioni ya jana Jumamosi (16/04) Jumuiya ya Watanzania waishio katika jiji la Houston na miji mingine ya karibu ilifanya Ibada Takatifu katika kanisa la Umoja kumuaga mpendwa wao Henry Kiherile aliyefariki wiki moja na nusu iliyopita baada ya kupigwa risasi na watu wasiojulikana. 
Ibada hiyo ilihudhuriwa na idadi kubwa ya watu waliokuwa na huzuni kubwa juu ya kifo hicho kilichogusa mioyo ya watu wengi. Mwili wa marehemu Henry unatarajiwa kusafirishwa jioni ya leo kuelekea nyumbani Tanzania kwa mazishi yanayotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam siku ya Ijumaa tarehe 22/04/2016. Pata picha za Misa hiyo hapa chini.
 
Marehemu Henry Kiherile enzi za uhai wake

Mr.& Mrs. Tenende ( Baba na Mama mkubwa wa marehemu ) wakiwa kanisani

Waombolezaji
 
Gari lililobeba mwili wa Henry likiingia kanisani 







 


Wachungaji wakiwa nje ya kanisa kabla ya ibada 









 


Jeneza lililobeba mwili wa Henry likiingizwa kanisani 




 


Dada Lulu ( mdogo wa Marehemu Henry ) akimuaga kwa uchungu kaka yake




 


Waombolezaji wakilia kwa uchungu 




 


Rafiki wa Henry kutoka Cameroon


























































































































































































































No comments: