Tuesday, March 8, 2016

SERIKALI YAZISHAURI TAASISI ZA KIBENKI NCHINI KUWA NA VILABU VYA MICHEZO NA MASHINDANO

Serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imezishauri Taasisi za Kibenki zilizopo nchini kuanzisha timu na vilabu vya michezo ili kukuza michezo pamoja na kuongeza fursa za ajira kwa vijana walio wengi ambao wana vipaji lakini hawana timu za kuwaendeleza.

Hayo yamebainishwa kupitia kwa Waziri mwenye dhamana, Mh. Nape Nnauye mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam wakati wa kukabidhi zawadi mbalimbali ikiwemo tuzo za wachezaji bora walioshinda katika michezo maalum ya BRAZUKA KIBENKI iliyoandaliwa na benki ya Barclays na wadau wengine.

Waziri Nape amebainisha kuwa, Nia ya Serikali ya awamu ya tano ni kuhakikisha inakuza michezo na kuwa na fursa za kiuchumi kupitia michezo hivyo taasisi hizo zinazo fursa ya kuongeza ajira na ustawi mzuri wa michezo endapo zitaanzisha timu za michezo na kimashindano kwani zinaweza na zinao wajibu huo.

Kwa mujibu wa Mratibu wa michuano hiyo, Nasikiwa Berya alieleza kuwa, jumla ya timu 16 zilishiriki huku ikianza 28 Novemba 2015 na kufikia tamati 20 Februari 2016 ilikuwa ni ya aina yake na kutoa mwangaza wa kimaendeleo wa kimichezo ambapo pia imesaidia kuimarisha afya, ushikamano na undugu kwa baina ya wachezaji na washangiliaji ambao wengi wao walitoka katika mabenki shiriki 15 ikiwemo matawi yao ya Tanzania Bara na Visiwani.

Katika tukio hilo, washindi mbalimbali walipatiwa vyeti vya shukrani hii ni pamoja na wadhamini wa mashindano hayo ikiwemo kutoka mabenki, kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (MeTL Group) na makampuni mengine walipewa vyeti vya shukrani katika kufanikisha michuano hiyo.
Imeandaliwa na Andrew Chale,Modewjiblog/MO tv)Nao
Mwakilishi kutoka MeTL Group, Bw.Zainul Mzige (kulia) akikabidhi cheti cha ushindi kwa Mchezaji Nuhu Mkuchu kutoka benki ya NMB.
nape bora
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mh. Nape Nnauye akikabidhi tuzo ya golikipa bora, Gabriel Bernard.
Nape boraa
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mh. Nape Nnauye akikabidhi tuzo ya mfungaji bora mchezaji kutoka benki ya NMB, Ahmed Nassoro.
nape ddfBaadhi ya washiriki na wageni mbalimbali walifika katika tukio hilo...
nape ff
Mratibu wa michuano hiyo Brazuka Kibenki, Bi. Nasikiwa Berya akikabidhi cheti kwa mmoja wa washindi wa michuano hiyo..
nape fg
Mratibu wa michuano hiyo, Nasikiwa Berya akikabidhi cheti kwa mshindi..
nape h
Waratibu wa mashindano ya Brazuka Kibenki, Bi.Nasikiwa Berya akiwa na Raymond Bunyinyiga wakifurahia jambo kutoka kwa Waziri wa Habari, Nape Nnauye. (Hayupo pichani).
Nape mchezji
Waziri Nape akimkabidhi tuzo ya mchezaji Bora, Ahmed Nassoro.
nape na maliz
Rais wa shirikisho la Soka nchini, (TFF), Jamal Malinzi akikabidhi cheti cha ushind kwa moja ya washiriki wa michuano ya Brazuka Kibenki.
nape oo
Mratibu wa michuano hiyo, Nasikiwa Berya akikabidhi cheti kwa mshiriki..
nape rr
Baadhi ya washiriki..
nape vbc
zoezi likiendelea..
nape vbv
Utoaji wa vyeti ukiendelea..
Nape yu
Waziri Nape akimkabidho tuzo, Kocha Bora, Bw. Mohamed Hussen 'Machinga' ambaye aliwahi kuwa mchezaji wa timu za Taifa na klabu kubwa za Tanzania ikiwemo Simba.
NAPE ZANI
Mwakilishi kutoka MeTL Group, Zainul Mzige akikabidhi cheti kwa mmoja wa washindi wa michuano ya Brazuka Kibenki. Zainul alikabidhi cheti hicho akimwakilisha Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (MeTL Group), Mohammed Dewji 'MO'.
nape zx
Waziri Nape akimkabidhi cheti Rais wa TFF, Jamali Malinzi, ambapo cheti hicho ni maalum kwa TFF kuongeza mchango wao kaatika kukuza michezo nchini..
Nape4rt
Waziri Nape akitoa tuzo hizo..
Nape112
Waziri Nape akitoa tuzo hizo..
Nape112
Waziri Nape akitoa tuzo hizo..
Napecheti
Rais wa TFF akikabidhi tuzo hizo
naper tyu
Utoaji wa tuzo hizo ukiendelea..
napess
Waziri Nape akitoa tuzo hizo..
NAPESSS
wageni waalikwa na washiriki kutoka mabenki mbalimbali..
Napeww
Waziri Nape akitoa tuzo hizo..
Npaae
Mwakilishi kutoka MeTL Group, Zainul Mzige akitoa vyeti kwa washiriki
Npe2
Baadhi ya washindi walifanikiwa kutwaa tuzo hizo za Brazuka Kibenki kutoka benki ya NMB.
Npe222
Wachezaji bora 11, wakipata picha ya pamoja..
npe44
Waziri Nape Nnauye akitoa nasaha fupi katika tukio hilo..
Nape22
Mwandishi Mwandamizi wa habari wa mtandao wa Modewjiblog, Bw. Andrew Chale akiwa katika picha ya pamoja na Mwakilishi kutoka MeTL Group, Zainul Mzige.
Npe33
Baadhi wa washriki na washindi wa Brazuka Kibenki..
Nape2
Hapa ilikuwa ni furaha kwa washiriki katika tukio hilo la Brazuka Kibenki..
Nape
Ilikuwa ni mwendo wa kucheza na kufurahia Kibrazuka..
Nape
Waziri Nape akipeana mkono naMwakilishi wa MeTL Group, Zainul Mzige katika meza kuu ya wageni waalikwa. Zainul Mzige alimwakilisha Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa MeTL Group, Mohammed Dewji 'MO'.
Nape222
Baadhi ya washiriki wakipata picha za ukumbusho katika tukio hilo.

No comments: