Thursday, March 17, 2016

MONGELLA AANZA NA KIPINDIPINDU JIJINI MWANZA

Na. Atley Kuni- Afisa habari Mwanza. 

 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella amesema ifikapo tarehe 30. Mei, 2016 endapo viongozi wa Wilaya za mkoa huo watakuwa bado wanakabiliwa na Ugonjwa wa Kipindupindu katika wilaya zao basi wajiandae kuwajibika.

Alitoa kauli hiyo wakati akizungumza kwenye kikao cha kujitambulisha kwenye ukumbi wa ofisi ya mkuu wa Mwanza mara baada yakuwasili mkoani humo na kuanza kazi mara moja.

Mongella alisema moja ya jambo lililonikera nikuona mkoa huo bado unakabiliwa na adha ya kipindupindu huku Wakuu wa Wilaya, wakurugenzi na wataalam wakiwa hawana mipango madhubuti yakutokomeza janga hilo “sasa tutaanza Operesheni maalum ijulikanayo Tukomeza Kipindupindu Mkoa wa Mwanza kuanzia tarehe 01 Aprili,2016 na hatutakuwa na simile na yeyote atakayetukwamisha” alisema na kusisitiza “Nina Machinery zote kwa nini nishindwe? 

 Mongela amesema Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi ambaye kufikia tarehe 30, Mei atashindwa kudhibiti kipindupindu itabidi wawiane radhi kwani hata kuwa tayari kuona anaadhibiwa kwa makosa ya mtu mwingine kwa uzembe.

“ Jamani suala la Kipindupindu tatizo lake kubwa ni uchafu” Mnataka mkuu wa mkoa kila siku aende kufagia, no haiwezekani, sitaweza kufanya hivyo, mimi mkuu wa mkoa nitatoka siku moja, nitaonesha mfano lakini sio kila siku, haya nikifagia Nyamagana na Sengerema nikafagie lini? Alihoji Mongella, “lazima kila mmoja awajibike kwa majukumu yake”.

Kwa mujibu wa taarifa za ugonjwa wa kipindupindu kutoka ofisi ya Mganga mkuu wa Mkoa hadi kufikia tarehe 17, Machi, 2016 jumla ya wagonjwa 1,775 walikuwa wameugua ugojwa wa huo ilihali wagonjwa waliopo kwenye matibabu ni kumi nanne (14) wagonjwa wapya wakiwa 5, wagonjwa hawa wanatokea katika Wilaya za Ukerewe (11), Ilemela (2) na Nyamagana (1).

Mongella katika hatua nyingine ameomba kupewa ushirikiano na watendaji wote, huku akisema katika kutekeleza majukumu yake ya ukuu wa mkoa hata muonea mtu kwani kufanya hivyo nikumkosea hata Mungu.

“ Najua wananchi huko nje wakisikia fulani katumbuliwa wanafurahi kweli kwakuwa ndio haja ya mioyo yao wanayo yapata wao, wananchi huunganisha na huduma tunazo zitoa” hivyo ni vizuri tu ukatekeleza wajibu wako kwa kufuta kanuni kama za jeshini, “wenzetu jeshini mimi nawapenda kweli kweli maana kule ni Usimamizi, Maelekezo na Utendaji hakuna blablaa alisema Mongela.

John Mongella anakuwa Mkuu wa mkoa wa Mwanza wa ishini na mbili, tangu mkoa huo ulipo anzishwa mwaka 1961, huku akiwa ni miongoni mwa wakuu wa mikoa 26 walioteuliwa na Rais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli kushika wadhifa huo siku ya jumapili tarehe 13. Machi. 2016, akichukua nafasi iliyo achwa wazi na Magessa Mulongo aliye teuliwa na kuhamishiwa katika Mkoa wa Mara.

No comments: