Tuesday, March 8, 2016

Kongamano la Moyo wa Wanawake lafana

Mwishoni mwa wikiendi ilipopita kumemalizika tukio kubwa kuelekea siku ya mwanamke Duniani, kulikuwa na Kongamano la Moyo wa Mwanamke Katika kanisa la Living Water Centre kawe,Kongamano hilo lilikuwa na lengo la kuwakutanisha wanawake wa kila dini,rika,rangi na wengine ikiwa ni kwa lengo la kuwakumbusha nafasi yao katika ufalme wa Mungu.

Kongamano hilo liliandaliwa na huduma ya Wamama kanisani hapo ikiongozwa na mmbeba maono Mwalimu Lilian Ndegi kwa msaada wa mme wake Apostle Onesmo Ndegi kiongozio wa huduma ya Living Water Centre Ministry.

Kongamano hilo huwa linalofanyika mara moja kila mwaka kanisani hapo kwa kusudi la kuwajenga Wanawake kuwa na uwezo katika kumtumika Mungu na kujua nafasi yao ya kutumika nafasi aliyowapa katika ufalme Mungu.

Kongamano hilo limefanyika baraka na msaada kwa wakina mama wengi Kuombewa na kwa kufundishwa kukabiliana na mazingira magumu na changamoto mbalimbali katika maisha kwa kujua nafasi yao Mungu aliyowapa na uwezo aliowapa kukabiliana na majukumu katika ngazi ya Familia,Huduma,Jamii na Taifa kwa ujumla.

Kongamano hilo lilikuwa na wazungumzaji kuoka baadhi ya nchi za Afrika Mch. Salome Mushi kutoka Botswana,Askofu Angela Acha Morfow kutoka Cameroom,Mch. Jael Tengu kutoka Nairobi Kenya na Mwenyeji Mwl.Lilian Ndegi.Waimbaji mbalimbali walikuwepo Women of The Kingdom,Living Waters,More than Enough Band na wengine wengi.
Mwenyeji Mwl.Lilian Ndegi 

Askofu Angela Acha Morfow kutoka Cameroom 
Mch. Jael Tengu kutoka Nairobi Kenya 
Mch. Salome Mushi kutoka Botswana 
Mch. Naomi Mhamba wa Living Water Center Tanzania 
Wanaume wachungaji walikuwepo kuhudhulia Kongamano hilo 





Wanenaji wa Kongamano la Mwanamke 2016 katika picha ya pamoja wa kwanza kushoto ni mwenyeji Mwl. Lilian Ndegi,Angela Morfaw kutoka Cameroon,Apostle Onesmo Ndegi mwenyeji,Jael Tengu kutoka Kenya na Salome Mushi Botswana. 
Maombi na Maombezi kwa wenye magonjwa na uhitaji yalikuwepo .

Maombi na Maombezi kwa wenye magonjwa na uhitaji yalikuwepo .

Maombi na Maombezi kwa wenye magonjwa na uhitaji yalikuwepo 

No comments: