Friday, March 18, 2016

KAMPUNI YA HUSEA YASHEREKEA KUTIMIZA MWAKA MMOJA NA AKINAMAMA WALIOJIFUNGUA LEO KATIKA HOSPITALI YA PALESTINA SINZA.

Na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.
KAMPUNI ya HUSEA imeadhimisha mwaka mmoja tangu kuazishwa kwake Machi mwaka huu kwa kutoa msaada wa vifaa vya hospitali na kuwapa zawadi akinamama waliojifungua leo katika hospitali ya Palestina Sinza jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na wandishi wetu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya HUSEA , Pamela Maro amesema kuwa Kampuni hiyo inajishughulisha na Mipango miji, utoaji ushauri bure kuhusiana na Ardhi, Upimaji wa Ardhi pamoja na uchoraji ramani za nyumba, pia amesema kuwa ofisi za Kampuni ya kampuni ya Husea zipo Sinza Palestina kwa yeyote anayetaka ushauri kuhusiana na ardhi anaweza kufika maeneo hayo kujipatia ushauri bila malipo.

Pia Pamela amewaasa wanawake waliotoka kujifungua leo na wanawake wote wanaopenda kumiliki ardhi kisheria waende katika ofisi zao ili waweze kupata ushauri wa bure kuhusiana na maswala ya ardhi.

Kwa upande wa Daktari Mkuu wa Hospitali ya Palestina Sinza, Wandi Kariame amewapongeza wafanyakazi wa  kampuni ya HUSEA kwa kuadhimisha mwaka mmoja leo.

Pia amewashukuru kwa  kuona mahitaji ya Hospitali hiyo na kuwapongeza wanawake waliojifungua leo kwa kuwapa zawadi ikiwa ni kuadhimisha siku iliyofunguliwa ofisi hiyo kwa kufikisha mwaka mmoja wa kampuni hiyo kwani wangeweza kwenda  katika hospitali nyingine au kwenda kilabu cha  pombe (Bar) kwenda kuadhimisha mwaka mmoja wa kampuni yao kwa kunjwa na kula vitu wanavyovitaka au kunywa pombe tuu lakini wamewaona wao.
Mratibu Huduma Tiba katika wodi ya wazazi katika hospitali ya Palestina Sinza, Faith Mdee akitoa maelekezo kwa wafanyakazi wa Kampuni ya Husea inayojishughulisha na utoaji ushauri, upimaji wa viwanja, uchoraji ramani za nyumba pamoja na mipango miji.
  Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya HUSEA, Pamela Maro akimkabidhi Daktari Mkuu wa Hospitali ya Palestina Sinza, Dkt. Wandi Kariame  aadhi ya vifaa vinavyotumika katika uzalishaji katika wodi la wazazi katika hospitali ya Palestina Sinza jijini Dar es Salaam leo.Kushoto ni Muuguzi katika wodi ya wazazi katika hospitali Palestina Sinza.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya HUSEA, Pamela Maro  pamoja na madaktari wa hospitali ya Palestina Sinza wakimkabidhi baadhi ya zawadi zilizotolewa na wafanyakazi wa kampuni ya Husea, mama aliyotoka kujifungua katika hospitali hiyo, Bahati Ramadhani.
Mfanyakazi wa Kampuni ya HUSEA akimwangalia mtoto aliyetoka kuzaliwa masaa machache yaliyopita. 
 Baadhi ya wazazi wakiwa wamewapakata watoto waliojifungua leo mara baada ya kupata zawadi na kampuni ya HUSEA jijini Dar es Salaam leo.


Mfanyakazi wa Kampuni ya HUSEA akimkabidhi mama aliyetoka kujifungua mda mfupi kabla ya kupewa zawadi hiyo katika hospitali ya Palestina Sinza leo jijini Dar es Salaa.
 Mfanyakazi wa kampuni ya HUSEA akimkabidhi mama aliyejifungua kwa njia ya Operesheni katika hosipitali ya Palestina Sinza jijini Dar es Salaam.
 Mama na mwana.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya HUSEA, Pamela Maro(Kushoto) akiwa na baaadhi ya wafanyakazi wa Kampuni ya HUSEA katika picha ya pamoja mara baada ya kutoa zawadi kwa watoto walipozaliwa leo katika hospitali ya Palestina Sinza jijini Dar es Salaam leo ikiwa ni kuadhimisha mwaka mmoja wa kampuni hiyo tangu kuanzishwa.
Picha na Avila Kakingo wa Globu ya Jamii.

No comments: