Thursday, March 31, 2016

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MIUNDOMBINU YAVUTIWA NA UJENZI WA DARAJA LA KIGAMBON



Barabara za kuingia na kutoka katika Daraja la Kigamboni jijini Dar es Salaam zinavyoonekana, wakati Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu walipotembelea na kujionea maendeleo ya ujenzi wa daraja hilo ambalo limekamilika kwa asilimia 99.9 na litaanza kutumika rasmi kuanzia Aprili 16.
Mkurugenzi Mkuu mpya wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Prof. Godius Kahyarara (kulia) akibadilishana mawazo na Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa NSSF, Juma Kintu na Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja ala Kigamboni, Karim Mataka wakati Wajumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Miundombinu ilipotembelea dalaja hilo.
Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja ala Kigamboni, Karim Mataka wakati Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu ilipotembelea dalaja hilo.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu wakikagua ujenzi wa daraja la Kigamboni.


Meneja Mradi wa ujenzi wa daraja la Kigamboni kutoka Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mhandisi, Karim Mataka akiwaonyesha wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu barabara zinazoingia katika daraja hilo, wakati walipofanya ziara ya kuangalia maendeleo ya ujenzi wake jijini Dar es Salaam.
Meneja Mradi wa ujenzi wa daraja la Kigamboni kutoka Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mhandisi, Karim Mataka akifafanua jambo mbele ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu mpya wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Prof. Godius Kahyarara.
Ufafanuzi kwa Wabunge.
Meneja Mradi wa ujenzi wa daraja la Kigamboni kutoka Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mhandisi, Karim Mataka akitoa ufafanuzi kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu jijini Dar es Salaam jana, walipotembelea kuangalia ujenzi wa daraja hilo linalotarajiwa kuzinduliwa Aprili 16. Kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Prof. Norman Sigala na kulia ni Mkurugenzi wa Mipango, Uwekezaji na Miradi wa NSSF, Yacoub Kidula.
Muonekano wa barabara za kuingia katika daraja la Kigamboni.
Darala la Kigamboni linavyonekana baada ya kukamilika kwa asilimia 99.9.
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Joseph Nyamhanga akifafanua jambo mbele ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu. Kulia ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Prof. Norman Sigala.
Wabunge wa Kamati hiyo wakipata ufafanuzi kutoka kwa Meneja Mradi wa ujenzi wa daraja la Kigamboni kutoka Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mhandisi, Karim Mataka.

No comments: