Tuesday, February 9, 2016

WAFANYABIASHARA WAASWA KULIPA KODI.



WAFANYABIASHARA waasa kulipa kodi  kwa kuto kulipa kodi ni kinyume cha sheria kwani huleta kuleta msukumo kwa Mamlaka ya Mapato kukusanya wa mapato ya serikali ili fedha hizo zitumike kwa matumizi yaliyokusudiwa.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Philip Mpango wakati akizungumza na wafanyabiashara jijini Dar es Salaam leo.

Pia amesema kuwa   wafanyabiashara wanatakiwa kushirikiana na serikali ya awamu ya tano katika ukusanyaji mapato ili kujenga mazingira bora ya wafanyabiashara.

Mpango amewaomba wafanyabiashara kutumia mashine za EFD ili kuongeza mapamo ya serikali wanampango wa kununua Mashine za EFD ili kuwapa wananchi ambao hawajaanza kuzitumia kwaajili ya kukusanya mapato ya serikali.

 Waziri wa Fedha na Mipango, Philip Mpango akizungumza na wafanyabiashara leo katika ofisi za wizara ya Fesha jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Taasisi ya sekta binafsi (TPSF), Salum Shamte.
Kutoka kulia ni Naibu waziri wa Fedha na Mipango, Ashantu Kijaji, katika ni Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Alphayo Kidata na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile wakiwa kwenye mkutano wa waziri wa Fedha na Mipango leo jijini Dar es Salaam.
 Makamu Mwenyekiti wa Taasisi ya sekta binafsi (TPSF), Salum Shamte akizungumza na wafanyabiashara  waliokusanyika leo katika ofisi za Wizara ya Fedha na Mipango jijini Dar es Salaam leo.

Kutoka kulia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya sekta binafsi (TPSF), Felix Mosha  na Mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya sekta binafsi (TPSF) wakiwa kwenye mkutano wa wafanyabiashara leo jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wafabiashara wakimsikiliza Waziri wa Fedha na Mipango, Philip Mpango katika mkutano huo uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.

Mwakilishi wa sekta ya Kilimo Sinari Sinari akizungumzia kuhusiana na sekta ya Kilimo jijini Dar es Salaam leo. 
Mkurugugenzi wa Bravo Logistics, Angelina Ngalula akizungumza na wafanyabiashara katika mkutano uliofanyika jijini Dar es Salaam leo, kuhusiana na usafilishaji wa mizigo kwa kutumia magari na jinsi adha ya usafari katika sekta ya usafirishaji hapa nchini.
Picha na Avila Kakingo wa Globu ya Jamii.

No comments: