Friday, February 12, 2016

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI, TEKNOLOJIA NA UFUNDI MHANDISI STELLA MANYANYA AFANYA ZIARA KATIKA MAMLAKA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI (VETA) MAKAO MAKUU, CHANG`OMBE JIJINI DAR ES SALAAM.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Mhandisi Stella Manyanya akizungumza na wafanyakazi wa VETA Makao Makuu (hawapo pichani) alipofanya ziara katika mamlaka hiyo Changombe jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa VETA Geofrey Sabuni na kulia ni Wakurugenzi wa Wizara hiyo walioongozana na Naibu waziri.
Meneja Uhusiano wa VETA Sitta Peter akitoa maoni yake wakati wa mazungumzo kati ya Naibu Waziri na wafanyakazi wa Mamlaka hiyo.
Wafanyakazi wa VETA Makao Makuu wakimsikiliza Naibu Waziri Mhandisi Stella Manyanya wakati wa ziara hiyo.
Mkurugenzi wa Mafunzo wa VETA Leah Lukindo akitoa wasilisho wakati Naibu waziri alipokutana na Menejimenti ya Mamlaka hiyo.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa VETA Geofrey Sabuni akimkaribisha Naibu Waziri Mhandisi Stella Manyanya kuzungumza na wafanyakazi wa VETA Makao Makuu wakati Naibu waziri alipofanya ziara katika Mamlaka hiyo.

No comments: