Monday, December 14, 2015

RAIS MAGUFULI AFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA JAPAN NCHINI

 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Balozi wa Japan nchini Masaharu Yoshida aliyefika Ikulu Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya mazungumzo. Katika Mazungumzo hayo Balozi Yoshida amempongeza Rais Magufuli kwa kuchaguliwa kuiongoza Tanzania katika awamu hii ya tano na pia amezungumzia miradi mbalimbali inayofadhiliwa na Japan hapa nchini.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na mmoja wa Maofisa walioambatana na Balozi Yoshida Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Kalenda kutoka kwa Balozi wa Japan hapa  nchini Mheshimiwa Masaharu Yoshida mara baada ya kumaliza mazungumzo Ikulu jijini Dar es Salaam.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kulia akiagana na Balozi wa Japan Nchini Mheshimiwa Masaharu Yoshida mara baada ya kumaliza mazungumzo Ikulu jijini Dar es Salaam. Picha na IKULU.

No comments: