Friday, October 23, 2015

MKURUGENZI MKUU MAMLAKA YA VIWANJA VYA NDEGE TANZANIA (TAA) AHUDHURIA MAHAFALI YA 46 YA SHULE YA SEKONDARI PUGU

 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Mhandisi Suleiman S. Suleiman (kulia) akipewa maelezo na mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Pugu, Godwin Ogweyo kuhusu utengenezaji wa kadi ambazo hazichafui mazingira alipotembelea maonesho ya shughuli zinazofanywa na wanafunzi hao alipokuwa mgeni rasmi katika Mahafali ya 46 ya wanafuzi wa kidato cha nne shuleni hapo, Dar es Salaam juzi (Oktoba 22). Kulia kwake ni Mkuu wa Shule hiyo, Jovinus Mutabuzi.
 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Mhandisi Suleiman S. Suleiman (katikati) akiongozwa na  Mkuu wa Shule ya Sekondari Pugu, Jovinus Mutabuzi kukagua bweni la wanafunzi la Ujamaa alilokuwa akilala alipokuwa mwanafunzi hapo miaka ya 70 wakati alipohudhuria sherehe za Mahafali ya 46 ya wanafunzi wa kidato cha nne shuleni hapo, Dar es Salaam juzi (Oktoba 22). Kushoto ni Mkuu Mwandamizi wa Taaluma, Simon Chumila.
 Wahitimu wa kidato cha nne katika Shule ya Sekondari Pugu, Dar es Salaam wakipiga makofi kumkaribisha mgeni rasmi, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Mhandisi Suleiman S. Suleiman wakati akiwasili ukumbini kuhudhuria sherehe za mahafali ya 46 ya wanafunzi hao, shuleni hapo juzi (Oktoba 22).
 Sehemu ya wanafunzi wenye ulemavu wa Shule ya Sekondari Pugu wakifuatilia matukio ya sherehe za Mahafali ya 46 ya wanafunzi wa kidato cha nne yaliyohudhuriwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Mhandisi Suleiman S. Suleiman, shuleni hapo, Dar es Salaam juzi (Oktoba 22).
 Wazazi wa wahitimu wa kidato cha nne katika Shule ya Sekondari Pugu, Dar es Salaam wakiwa wamesimama kumkaribisha Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Mhandisi Suleiman S. Suleiman alipokuwa akiwasili kuhudhuria sherehe za mahafali ya 46 ya wanafunzi hao shuleni hapo, Dar es Salaam juzi (Oktoba 22).
 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, Mhandisi Suleiman S. Suleiman akivishwa skafu na mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Pugu kama heshima ya kuwa mgeni rasmi katika sherehe za mahafali ya 46 ya wanafunzi wa kidato cha nne shuleni hapo, Dar es Salaam juzi (Oktoba 22). Kushoto ni Mkuu wa Shule hiyo, Jovinus Mutabuzi.

No comments: