Tuesday, July 21, 2015

Ujumbe wa Maafisa Waandamizi kutoka Nigeria watembelea Wizara ya Mambo ya Nje, yawapokea Madaktari kutoka Marekani

Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya akiukaribisha Ujumbe wa Maafisa Waandamizi kutoka Taasisi ya Taifa ya Mafunzo ya Sera na Stratejia ya Nigeria walipotembelea Wizarani  tarehe 20 Julai, 2015. Ujumbe huo upo nchini kwa ziara ya mafunzo ya siku 12 ambapo watatembelea Wizara na Taasisi mbalimbali za hapa nchini.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Zuhura Bundala akimkaribisha Kaimu Katibu Mkuu kuzungumza na ujumbe huo kutoka Nigeria.
 JUU NA CHINI:
Baadhi ya wajumbe wa msafara huo wakimsikiliza Kaimu Katibu Mkuu (hayupo pichani) wakati wa kikao hicho.
 Kaimu Katibu Mkuu, Balozi Simba akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa msafara huo Bw.Hamakim Jonny Godwin. 
Picha ya pamoja.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bibi Rosemary Jairo akiwakaribisha nchini Timu ya Madaktari kutoka Marekani mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam hivi karibuni. Madaktari hao wapo nchini kwa ajili ya kutoa huduma za matibabu kwa magonjwa mbalimbali katika Hospitali za Mwananyamala ya Jijini Dar es Salaam na Mnazi Mmoja, Zanzibar. Ziara ya Madaktari hao ambao wametoka Majimbo ya Washington DC, Maryland na Virginia imeratibiwa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa  kwa kushirikiana na Jumuiya ya Watanzania waishio Marekani (Diaspora).
Rais wa Jumuiya ya Watanzania waishio Marekani, Bw. Iddi Sandaly ambaye amefuatana na Madaktari hao kutoka Marekani akielezea jambo mara baada ya kuwasili nchini.
Bibi Jairo akizungumza na waandishi wa Habari kuhusu dhumuni la ziara ya madaktari hao hapa nchini.
Mmoja wa Madaktari kutoka Marekani akizungumza na Waandishi kuhusu  ziara yao hapa nchini
Bw. Sandaly akifafanua jambo kwa waandishi kuhusu ziara ya madaktari hao kutoka Marekani.

No comments: