Wednesday, June 10, 2015

WAZIRI CHIKAWE ACHUKUA FOMU YA KUOMBA KUTEULIWA KUGOMBEA URAIS KUPITIA CCM

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe (katikati) akionyesha kabrasha lenye fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM). Kushoto ni Katibu wa Halmashauri Kuu Taifa (Nec) ya CCM wa Idara ya Oganizesheni, Dk. Mohamed Seif Khatibu. Kulia ni mkewe Waziri Chikawe, Profesa Amandina Lihamba. Tukio hilo la uchukuaji wa fomu lilifanya katika Ofisi za Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma leo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe akisaini kitabu kabla ya kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM). Tukio hilo la uchukuaji wa fomu lilifanya katika Ofisi za Makao Makuu ya CCM mjini, Dodoma leo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe akiwaonyesha wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na waandishi wa habari (hawapo pichani) kabrasha lenye fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM kabla ya kuanza kuzungumza na kujibu maswali mbalimbali ya waandishi wa habari. Kulia ni mkewe Waziri Chikawe, Profesa Amandina Lihamba. Tukio hilo la uchukuaji wa fomu lilifanya katika Ofisi za Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma leo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe akizungumza na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na waandishi wa habari mara baada ya kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM. Waziri Chikawe ambaye alijibu maswali ya waandishi wa habari kiufasaha huku akishangiliwa na wanachama hao, alisema yeye ni kiongozi mwenye uzoefu mkubwa na pia akiteuliwa na chama chake kugombea nafasi hiyo ataendeleza mapambana zaidi dhidi ya maadui watatu ambao ni ujinga, maradhi na umaskini pamoja na adui mwingine rushwa ambaye ni adui wa maendeleo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe akizungumza na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na waandishi wa habari mara baada ya kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM, Waziri Chikawe ambaye alijibu maswali ya waandishi wa habari kiufasaha huku akishangiliwa na wanachama hao, alisema yeye ni kiongozi mwenye uzoefu mkubwa na pia akiteuliwa na chama chake kugombea nafasi hiyo ataendeleza mapambana zaidi dhidi ya maadui watatu ambao ni ujinga, maradhi na umaskini pamoja na adui mwingine rushwa ambaye ni adui wa maendeleo. Kulia ni mkewe, Profesa Amandina Lihamba.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe akishangiliwa na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mara baada ya kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM, Waziri Chikawe ambaye alijibu maswali ya waandishi wa habari kiufasaha huku akishangiliwa na wanachama hao, alisema yeye ni kiongozi mwenye uzoefu mkubwa na pia akiteuliwa na chama chake kugombea nafasi hiyo ataendeleza mapambana zaidi dhidi ya maadui watatu ambao ni ujinga, maradhi na umaskini pamoja na adui mwingine rushwa ambaye ni adui wa maendeleo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe (kulia aliyekaa) akiongoza zoezi la uhakiki wa kadi za wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliokuja kumdhamini kugombea kuteuliwa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM, katika ofisi ya Katibu wa CCM, Wilaya ya Dodoma mjini. Waziri Chikawe wakati akiwa anajibu maswali ya waandishi wa habari, alisema yeye ni kiongozi mwenye uzoefu mkubwa na pia akiteuliwa na chama chake kugombea nafasi hiyo ataendeleza mapambana zaidi dhidi ya maadui watatu ambao ni ujinga, maradhi na umaskini pamoja na adui mwingine rushwa ambaye ni adui wa maendeleo. Picha zote na Felix Mwagara.

No comments: