Thursday, June 4, 2015

KAMPUNI YA SWALA YAGAWA UMILIKI WA ASILIMIA 25 ZA RIBA YA LESENI KWA KAMPUNI YA TATA PETRODYNE LIMITED

Kampuni ya mafuta na gesi ya Swala (Tanzania) Plc ("swala" au "Kampuni") inayo furaha kutangaza kwamba imefikia makubaliano ya kugawana umiliki na Kampuni ya Tata Petrodyne Limited ("TPL"), kampuni ambayo ni sehemu ya Kampuni ya Kimataifa ya Tata sons Limited, ambapo TPL itakuwa ikifanya shughuli zake kwenye maeneo ya leseni ya Pangani na Kilosa-Kilombero nchini Tanzania. Hii itaiwezesha Kampuni ya swala kubaki kwenye maeneo yake ya leseni na ili kupata fedha kwa ajili ya shughuli za utafutaji hapo baadaye katika njia ambayo itapunguza hasara kwa wanahisa wake wa sasa.

Kampuni ya Tata Sons Limited ni Mratibu wa uendeshaji wa shughuli kubwa za makampuni ya Tata na kumiliki hisa zote muhimu kwenye makampuni haya, na kwa kawaida inajulikana kama kundi la Tata (Tata Group). Kundi la Tata lina mtaji wa soko wa takribani dola za Kimarekani bilioni 110 na inawakilisha zaidi ya asilimia 8 ya jumla ya mtaji wa soko katika soko la hisa la Bombay.

Katika sekta ya mafuta na gesi, makubaliano ya kugawiana umiliki ni makubaliano yaliyoingiwa kwa mmiliki wa leseni moja au zaidi (anayegawa umiliki huo) na kampuni nyingine ambayo inataka kupata asilimia ya umiliki wa leseni hiyo kwa ajili ya kutoa huduma (na 'kujimilikisha). Makubaliano ya kugawana umiliki yanatofautiana na shughuli za kawaida kati ya wakodishaji wawili wa mafuta na gesi, kwa sababu cha msingi kuzingatia ni utoaji wa huduma, badala ya ubadilishaji rahisi wa fedha.

Makubaliano yaliyofikiwa na TPL:
Baada ya kupokea vibali vya kiserikali kwa ajili ya uhamisho wa maslahi, kampuni ya TPL itailipa  kampuni ya swala Jumla ya dola za kimarekani milioni 5.7 kwa ajili ya usawa wa maslahi, asilimia 25 katika leseni ya Kilosa-Kilombero na usawa wa maslahi wa asilimia 25 katika leseni ya Pangani kama fidia zidi ya gharama zilizotumika zamani kwenye leseni;

Kampuni ya TPL itaibeba Swala kwa gharama ya kisima cha awali kwenye leseni ya Kilosa-Kilombero, hadi kiwango cha juu cha dola za kimarekani milioni 2.5 (swala inakadiria gharama za awali za kisima kuwa dola za kimarekani milioni 10.0);

Kampuni ya TPL itaibeba Swala kwa gharama ya kisima cha awali kwenye leseni ya Kilosa-Kilombero, hadi kiwango cha juu cha dola za kimarekani milioni 2.125 (swala inakadiria gharama za awali za kisima kuwa dola za kimarekani milioni 8.5);

Kampuni ya TPL itailipa swala zaidi ya dola za kimarekani milioni 1.0 dhidi ya gharama ya kisima cha pili kufuatia ugunduzi wa kibiashara katika kisima cha awali kwenye leseni ya Kilosa-Kilombero. Gharama zilizotumika zaidi ya kiasi hiki zitabebwa na washirika kulingana na usawa wao.

Kwenye ukamilisho wa Muamala uliotangazwa leo, usawa katika leseni mbili utakuwa:
Swala TPL * Otto
Kilosa-Kilombero 25% 25% 50%
Pangani 25% 25% 50%
* Otto Energy (Tanzania) Pty Ltd “(Otto”) ni mmiliki mkubwa wa sehemu ya Otto Energy Ltd (ASX: OEL)
Kampuni inakadiria kuwa kwa sasa imejidhatiti kikamilifu kwa majukumu yake yaliyobakia kwenye leseni zote mbili. Kampuni ya swala ilishauriwa katika shughuli hii na kampuni ya First Energy Capital ("FIRSTENERGY") na kampuni ya TPL ilishauriwa na benki ya Rand Merchant.

Naye Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Swala Dk David Mestres Ridge alisema: "Kampuni inayo furaha kutangaza makubaliano ya swala Tanzania na kampuni ya TPL inayofahamika kwa sifa nzuri. Ugawaji huu wa umiliki utatoa mwanya kwa Kampuni kufadhili majukumu yake iliyojiwekea kwa njia ambayo inapunguza hatari kwa wanahisa wetu bila kuwa na haja ya kuongeza hisa ya ziada za kianzio kwa wakati huu.

Napenda kutoa shukurani kwa FirstEnergy kwa ajili ya mbinu zao za kitaalamu katika kuendesha mchakato wa kugawa umiliki na kwa ajili ya kuzalisha riba kutoka kwenye makundi hayo yanayoheshimika sana.

Kwa sasa kampuni ya Swala itazingatia kupata ridhaa muhimu na vibali vya kiserikali ili kuruhusu ubia mpya uliotengenezwa ili kuendeleza mipango ya uchimbaji kwenye leseni zote mbili na tunataraji kuboresha soko pamoja na mwongozo wa lini mambo haya yaanze.

No comments: