Friday, January 9, 2015

RAIS KIKWETE AKABIDHI VITABU 201 KWA CHUO CHA TAIFA CHA ULINZI, AAGANA NA MABALOZI WA TANZANIA NCHINI CANADA NA RWANDA

Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimsikiliza Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange alipokuwa akimjshukuru kwa kutoa vitabu 2752 kwa Chuo cha Ulinzi na makataba zingine za JWTZ wakati wa hafla fupi ya kukabidhi vitabu 201 kwa ajili ya Maktaba ya Chuo cha Ulinzi (National Defence College - NDC) iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Ijumaa January 9, 2015.
Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi baadhi ya vitabu na Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange. Rais Kikwete amekabidhi vitabu hivyo 201 kwa ajili ya Maktaba ya Chuo cha Ulinzi (National Defence College - NDC) iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Ijumaa January 9, 2015. Rais kikwete, ambaye ameshachangia jumla ya vitabu 2752 katika maktaba ya chuo hicho na chuo cha Monduli katika vipindi tofati, amesema elimu imo vitabuni, na ili kuelemika yapaswa mtu asome vitabu, na kwamba taasisi ya elimu inakamilika ikiwa na vitabu.
Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange na maafisa waandamizi wa JWTZ wakiangalia vitabu wakati wa hafla fupi ya kukabidhi vitabu 201 kwa ajili ya Maktaba ya Chuo cha Ulinzi (National Defence College - NDC) iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Ijumaa January 9, 2015.
Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange na maafisa waandamizi wa JWTZ baada ya hafla fupi ya kukabidhi vitabu 201 kwa ajili ya Maktaba ya Chuo cha Ulinzi (National Defence College - NDC) iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Ijumaa January 9, 2015.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mhe Ali Siwa, Balozi wa Tanzania nchini Rwanda aliyefika Ikulu jijini Dar es salaam leo Ijumaa January 9, 2015 kuaga rasmi kabla ya kwenda kuripoti kwenye kituo chake cha kazi.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mhe Jacky Zoka, Balozi wa Tanzania nchini Canada aliyefika Ikulu jijini Dar es salaam leo Ijumaa January 9, 2015 kuaga rasmi kabla ya kwenda kuripoti kwenye kituo chake cha kazi.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Mhe Jacky Zoka, Balozi wa Tanzania nchini Canada na Mhe Ali Siwa, Balozi wa Tanzania nchini Rwanda, walipofika Ikulu jijini Dar es salaam leo Ijumaa January 9, 2015 kuaga rasmi kabla ya kwenda kuripoti kwenye vituo vyao vya kazi. PICHA NA IKULU.

No comments: