Sunday, January 18, 2015

KISOMO CHA KUMWOMBEA RASHID MKAKILE APONE HARAKA BOSTON, MASSACHUSETTS NCHINI MAREKANI

Ustadh Hemed (mwenye kipaza sauti) akiongoza kisomo cha kumwombea Rashid Mkakile apone haraka kilichofanyika siku ya Jumamosi Januari 17, 2015 mjini Boston jimbo la Massachusetts, Rashid Mkakile (hayupo pichani) alipata stroke alipokua kikazi jimboni hapo na kumpelekea kulazwa katika hospitali ya Beth Israel Deaconess Medical Center tangia mwezi wa Oktoba 2014 na baadae kuendelea na mazoezi ya mama cheza (Physical therapy) na kumfanya kuendelea vizuri na kesho Jumapili atarejea Dallas atapokua akindelea na mazoezi ya mama cheza na tunaomba muendelee kumtia kwenye maombi na sala zeni za kila siku. Kulia ni Salum mmoja wa mkazi wa Massachusetts na kiongozi wa Jumuiya ya Watanzania jimbo hilo ambaye yeye na wenzake walikuwa mstari wa mbele katika kumsaidia Rashid Mkakile na kuhakikisha hayupo peke japo hapo Massachusetts ambapo Mkakile alikuwepo kwa kizazi sio jimbo analoishi.
Watanzania wa Massachusetts wakifanya kisomo cha kumwombea Rashid Mkakile aendelee kupata nafuu kilichofanyika siku ya Jumamosi Januari 17, 2015. mjini Boston jimbo la Massachusetts.
Kushooto n Mohammed Mkakile(mdogo wa Rashid), Rashid Mkakile na Eliud Mbowe wakifuatilia kisomo.
Ikota akifuatilia kisomo 
Eddy akitoa shukurani kwa niaba ya Watanzania wa Massachusetts.
Rashid Mkakile akitoa shukurani zake kwa Watanzania wa Massachusetts kwa kuwa karibu nae kwa muda wote tangia siku ya kwanza ya maradhi yake.
Ikota nae akitoa shukurani kwa niaba ya familia ya Rashid Mkakile.
Mayor Mlima akitoa shukurani kwa niaba ya Watanzania wa DMV na Massachusetts.
Watanzania wa Massachusetts na baadhi kutoka Michigan na DMV wakijumuika pamoka kwenye kisomo cha kumwombea Rashid Mkakile aendelee kupata nafuu na hatimae kupona haraka.
Picha ya pamoja na Mkakile
Kwa picha zaidi bofya HAPA

No comments: