Wednesday, January 14, 2015

KATIBU MKUU WA CCM NDUGU KINANA AANZA ZIARA YA SIKU 16 YA UNGUJA NA PEMBA

 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akiwasalimia baadhi ya Wananchi hawapo pichani alipokuwa akiwasili katika uwanja wa Tawi la CCM Matarumbeta katika jimbo la Jang'ombe,ambapo Ndugu Kinana alikabidhi vifaa vya michezo kwa vijana,alikabidhi vifaa vya mradi wa maji safi,pia alikabidhi hati kwa kikundi cha vijana Jang'ombe
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akikabidhi bati kwa ajili ya ujenzi wa msikiti kwa mmoja wa wananchi kwenye uwanja wa Tawi la CCM Matarumbeta katika jimbo la Jang'ombe,ambapo Ndugu Kinana alikabidhi vifaa vya michezo kwa vijana,alikabidhi vifaa vya mradi wa maji safi,pia alikabidhi hati kwa kikundi cha vijana Jang'ombe.
Msafara wa Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana ukiwasili katika tawi la CCM Mikunguni (shehia ya Mikunguni),kushiriki katika shughuli za uchimbaji na utandazaji wa mabomba ya maji na salama.
 Mbunge wa Jimbo la Kwahani,Mh.Dkt.Hussein Ali Mwinyi akizungumza mbele ya wakazi wa Shehia ya Mikunguni (hawapo pichani),wakati wa ziara ya Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana aliyoianza leo wilaya ya mjini Zanzibar.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na baadhi ya wananchi na wanachama wa Shehia ya Mikunguni ,wakati wa ziara yake aliyoianza leo wilaya ya mjini Zanzibar.
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa pamoja na Mbunge wa Jimbo la Kwahani,Mh.Dkt.Hussein Ali Mwinyi akishiriki uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama kwa wakazi wa Shehia ya Mikunguni ,katika jimbo la Kwahani.
  Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa pamoja na Mbunge wa Jimbo la Kwahani,Mh.Dkt.Hussein Ali Mwinyi wakishiriki katika shughuli za uchimbaji na utandazaji wa mabomba ya maji safi na salama kwa wakazi wa Shehia ya Mikunguni ,katika jimbo la Kwahani.
 Baadhi ya wakazi wa mji wa Shehia ya Makadara wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana alipotembelea jimbo la Rahaleo,ambapo alishiriki katika ujenzi wa Taifa za uchimbaji wana utandazaji wa Mabomba ya maji safi na salama.
 Wananchi wa mji wa Shehia ya Makadara na wanachama wa CCM,wakishangilia jambo  Katibu Mkuu wa CC,Ndugu Kinana akiwa
Katibu Mkuu wa CC,Ndugu Kinana akishiriki ujenzi wa Ofisi ya tawi la CCM-Mwembeladu katika jimbo la Rahaleo
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akisalimiana na Balozi Ali Karume alipowasili katika Shehia ya Miembeni,katika jimbo la Kikwajuni,ambapo Ndugu Kinana alipokea taarifa fupi ya mradi wa Zahanati  na kushiriki katika ujenzi wa Taifa wa Ukarabati wa Zahanati ya Miembeni (Nyumba ya Yasu).Pichani kulia ni Muwakilishi wa jimbo la Kikwajuni,Mh.Mahamoud Mohamed Mussa pamoja na Mbunge wa jimbo hilo la Kikwajuni Mh.HamadiYussuf Massauni
Katibu wa NEC-Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye akifurahia jambo na  Balozi Ali Karume  walipokutana leo katika Shehia ya Miembeni,katika jimbo la Kikwajuni
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akipata maelezo mafupi ya mradi mkubwa wa kisasa alipokwenda kutembelea Tawi la CCM Vikokotoni katika jimbo la MjiMkongwe
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akipata taarifa fupi ya mradi wa maduka kwa vijana wajasiliamali katika Shehia ya Kilimani,ambapo Ndugu Kinana alishiriki shughuli za uchimbaji na utandazaji wa mabomba ya mradi wa maji safi na salama na ujenzi wa Maskani ya Fishamen,katika jimbo la Mjimkongwe..
 Katibu Mkuu wa CCM,Abdulrahman Kinana pamoja na wanachama wa CCM wakiwemo na Wananchi kwa pamoja wakishiriki katika shughuli ya za uchimbaji na utandazaji wa mabomba ya mradi wa maji safi na salama katika shehia ya Kilimani,kwenye jimbo la Mjimkongwe.
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akipata maelezo mafupi ndani ya chumba cha kufundishia Kompyuta katika kituo cha Vijana (Tanzania Youth Icon),cha kuwaendeleza na kuwawezesha katika masuala mbalimbali ikiwemo elimu,Ajira na Michezo kilichopo Shehia ya Miembeni,Mwembemadema katika jimbo la Kikwajuni.
 Mwenyekiti wa Kituo cha Tanzania Youth Icon (TAYI),Bwan.Abdullah Miraji Othman akisoma hotuba Mbele ya Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana kuhusiana na mambo mbalimbali yahusuyo kituo hicho cha huduma rafiki kwa Vijana kilichopo Muembemadema ndani ya jimbo la Kikwajuni sambamba na changamoto wazipatazo juu ya kituo hicho.
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana  akizungumza mbele ya wanachama wa chama hicho pamoja na Wananchi nje ya Kituo cha Tanzania Youth Icon (TAYI),ambapo mlezi na mhamasishaji wake ni Mbunge wa jimbo la Kikwajuni,Mh.Hamad Yusuf Masauni.Kituo hicho cha TAYI ni Taasisi ya vyama visivyokuwa vya kiserikali,ambayo ina muelekeo wa kuwasaidiana na Wadau mbalimbali katika kufanikisha shughuli za maendeleo.Mwenyekiti wa Kituo cha Tanzania Youth Icon (TAYI),Bwan.Abdullah Miraji Othman amesema kuwa Taasisi hiyo hivi sasa ina ina wanachama wasiopungua 500 ambao tayari wameandikishwa na kuwepo katika rekodi na kumbukumbu za ofisi,Bwana Abdullah aliongeza kuwa kituo hicho kinawajenga vijana kiuchumi na pia kuwapa taaluma ya uongozi ili waje kuwa viongozi wazuri ,''kituo hiki kimekuwa kiwanda kizuri cha kuzalisha vijana wazuri kwa Taifa'',alisema Bwan.Abdullah .
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akikabidhi piki piki kwa  mmoja wa makatibu wa CCM.
Mmoja wa Mabalozi akifurahi mara baada ya kukabidhiwa baiskeli yake na Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana,kwa shughuli mbalimbali za kichama,baiskeli hizo ilikuwa ni ni moja ya ahadi alizoahidi kutoa Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni,Mh Masauni,ambapo pia alitoa piki piki kwa makatibu wa chama.

No comments: