Monday, October 13, 2014

RAIS KIKWETE ALIPOFUNGUA JENGO LA KITEGA UCHUMI LA HOTELI YA PPF MWANZA

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe ikiwa ni ishara ya ufunguzi rasmi wa jengo la hoteli ya Gold Crest linalomilikiwa na Mfuko wa Pensheni wa PPF katika hafla fupi ya uzinduzi iliyofanyika hivi karibuni jijini Mwanza.Wengine pichani toka kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza,Mh. Evarist Ndikilo,Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa PPF,ndg. Ramadhan Kijjah,Naibu Waziri wa Fedha,Mh. Adam Malima,Mkurugenzi  Mkuu wa Mfuko wa PPF,William Erio pamoja na Waziri wa Ujenzi,Mh. John Magufuli.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia katika hafla ya ufunguzi wa jengo la kitega uchumi la hoteli linalomilikiwa na Mfuko wa PPF jijini Mwanza.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akifatilia kwa makini maelezo ya Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa PPF Ndg. William Erio.
Naibu Waziri wa Fedha,Mhe. Adam Malima (Mb) akihutubia wageni waalikwa katika hafla ya ufunguzi wa jengo la kitega uchumi la hoteli inayomilikiwa na Mfuko wa PPF jijini Mwanza. Ufunguzi huo uliambatana na Rais kutembelea sehemu mbalimbali za jengo hilo la Hoteli.
Jengo la kitega uchumi la hoteli ya PPF Mwanza Gold Crest.
Mamia ya wakazi wa Mwanza wafurika katika hafla ya ufunguzi wa jengo la kitega uchumi la hoteli ya PPF Mwanza.
Mh. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Pensheni wa PPF. Pamoja nao ni Waziri wa Ujenzi Mhe. John Magufuli, Naibu wa Waziri wa Fedha Mhe. Adam Malima, na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Mhandisi Evarist Ndikilo.
Mh. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa katika picha ya pamoja na Menejimenti ya PPF mara baada ya kuzindua jengo la kitega uchumi la hoteli ya PPF Mwanza.
Mh. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa katika picha ya pamoja na Wafanyakazi wa PPF .
Mh. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa katika picha ya pamoja na Ndg. Meshack Bandawe Meneja wa PPF Kanda ya Ziwa na Mratibu wa hafla ya ufunguzi wa jengo la kitega uchumi la hoteli ya PPF Mwanza.

No comments: