Kikosi cha Timu ya Wakata Miwa Kagera Sugar wameanza leo hii safari kuelekea jijini Tanga kwa ajili ya mchezo wa ufunguzi wa Ligi kuu soka Tanzania bara katika uwanja wa CCM Mkwakwani dhidi ya wenyeji Mgambo JKT, septemba 20 mwaka huu.
Kocha msaidizi wa Kagera Sugar, Murage Kabange amesema klabu hiyo ina jumla ya wachezaji 25 na hii leo tayari wapo safari na viongozi watano kwenda kusaka pointi tatu muhimu.
Kabange aliongeza kuwa wameamua kuanza safari mapema kwasababu kutoka Kagera kwenda Tanga ni mbali sana.
Viongozi wa Kagera Sugar
Wachezaji wa Kagera Sugar wakifaya mazoezi yao kwenye Uwanja wa Kaitaba Hivi karibuni.
Baadhi ya Viongozi wa Timu ya Kagera Sugar wakiwa Uwanjani Kaitaba wakishuhudia mazoezi ya Vijana wao. Wakijifua kujiandaa na Ligi Kuu Vodacom msimu mpya 2014/15 inayotarajia kuanza hivi Karibuni sep.20 mwaka huu.
Kikosi cha Kagera Sugar
Murage Kabange, kocha msaidizi wa Kagera Sugar (kulia) tayari amebainisha kuwa mapungufu waliyokuwa nayo katika kikosi chao kuwa wameishayafanyia marekebisho na wako tayari kupambana na Mgambo JKT ya Mjini Tanga.![](https://blogger.googleusercontent.com/img/proxy/AVvXsEg2G2fb2agiy2Ew844qDM1Y4OU0pITMDtsmVj_eSybom08JLUkg-RDNEREIVJaX39Yt-XlOzxP3FuE0f2f97yIwbxRJhWY9L5p-SxBD7C7u8OJc7fsdU_hj0gqZMFVPjN_KTjwonOlS6nFaLkWtYnjX8fA86fDkn7KVKdarxBQ76e74dTc4Zx9SvbdOE9lZR-osZSIQFLsnmPVSYwS1vm3H-h0Jh-MmzdEFHaOHPdGc9Mci7hsfVPDq2Xceg689CUwYu4_iSTCySFou-i_ejQJCXkaqEAkq0o9im7WpnWqs7P5qRmNSuPV34QMNQNhL4uXnLFyywtCrIy3-N_Xr8VH3hWs_cDPLeIE_TFxdunko2bXK-KBrC7h1oq_K_qSejGNst5GxRswr9LUHtjh6C9HxYelWSia7WHk=s0-d-e1-ft(12).JPG)
Kocha Mkuu wa Kagera Sugar (kulia) Bw. Jackson Mayanja akiangalia vijana wake wakati w mazoezi yao kwenye Uwanja wao wa Nyumbani Kaitaba hivi karibuni.
No comments:
Post a Comment