Monday, July 28, 2014

WANAHABARI ,WADAU WA MICHEZO WAJITOKEZA KUHANI MSIBA WA MPIGANAJI HENRY LYIMO (KIPESE), MOSHI

Baadhi ya waamuzi waliofanya kazi ya Uamuzi na Marehemu Henry Lyimo (KIPESE),Nathan Lazaro na Vitaris wakiwa nyumbani kwao na Marehemu kuhani msiba.
Kocha Hamad Haule ambaye amekuwa karibu sana na Marehemu Kipese akijaribu kuweka mambo sawa ili kuhakiksha wanaofika Msibani wanapata sehemu ya kuketi.
Wadau wa Michezo wakijadiliana jambo katika Msiba huo.
Viongozi wa Machava fc ,Abuu Masudi,(wa kwanza walioketi) ,Mtangazaji wa Moshi fm radio Bahati Nyakiraria na Sembi Hassan Sembi alioketi wakisiliza jambo toka kwa Mwamuzi Thomas Mkombozi (aliyesiamama)
Baadhi ya waamuzi wa mchezo wa soka mkoa wa Kilimanjaro.
Waombolezaji waliofika katika msiba huo.
Baadhi ya wanahabari wakijadiliana jambo.
Wanahabari wa kike wao pia walikuwa ni miongoni mwa waombolezaji waliofika nyumbani kwao na Marehemu.
Mratibu wa Klabu ya waandishi wa Habari mkoa wa Kilimanjaro Yusuph Mazimu pamoja na Mweka hazina Msaidizi Rodrick Mushi wakiwa buze na simu zao kuhakikisha taarifa zinawafikia watu waliokuwa karibu na Marehemu.
Afisa Habari wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa Shaban Pazi akiteta jambo na mwandishi Charles Ndagulah.
Marehemu Henry Lyimo enzi za uhai wake akitekeleza majukumu yake katika kituo cha radio cha Moshi fm.
Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

No comments: