Friday, May 23, 2014

TASWIRA MBALI MBALI KUTOKA BUNGENI MJINI DODOMA

Waziri wa Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki Mhe.Samweli Sitta akijibu hoja za wabunge kabla Bunge halijapitisha Bajeti ya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki kwa Mwaka 2014/2015.
Maofisa wa wizara ya Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki wakiwa pamoja na Wabunge wa Afrika ya Mashariki wakifuatilia kikao cha Bajeti ya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki kwa 
Mwaka 2014/2015.
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki Mhe.Samweli Sitta akijadiliana jambo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki,Joyce Mapunjo mara baada ya Bunge kupitisha Bajeti ya Wizara hiyo kwa Mwaka 2014/2015.
Wabunge wa Afrika Mashariki wakiwasili Bungeni Mjini Dodoma.
Mbunge wa kuteuliwa Mhe.James Mbatia akifurahia jambo na Mhe.Shyrose Banji Mbunge wa Afrika Bunge la Afrika ya Mashariki.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki,Joyce Mapunjo (kulia) akijadiliana jambo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano,Mhe.Samia Suluhu (kushoto) na Mhe.Celina Kombani.
Mbunge wa Chalinze,Mhe.Ridhiwani Kikwete (kushoto) akijadiliana jambo na Mbunge wa Bunge la Afrika ya Mashariki,Mhe. Shyrose Banji 
Wanachuo kutoka Chuo cha Mipango Dodoma wakiwa katika picha ya pamoja nje ya viwanja vya Bunge wakati walipofanya ziara ya kimafunzo Bungeni na kufuatilia Bajeti ya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki kwa Mwaka 2014/2015.
Wanachuo kutoka Chuo cha Uuguzi Mirembe Dodoma wakiwa kwenye picha ya pamoja nje ya viwanja vya Bunge wakati waliofanya ziara ya kimafunzo Bungeni na kufuatilia Bajeti ya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki kwa Mwaka 2014/2015 .
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki Mhe.Samweli Sitta na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki ,Joyce Mapunjo wakiwa kwenye picha ya pamoja na Maofisa wa wizara yake pamoja na Wabunge wa Afrika ya Mashariki mara baada ya Bunge kupitisha Bajeti ya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki kwa Mwaka 2014/2015.Picha na Deusdedit Moshi,Globu ya Jamii

No comments: