Friday, March 7, 2014

KAMPENI ZA CCM KALENGA ZATINGA KIJIJI ALICHOZALIWA MGOMBEA WA CHADEMA, MWENYEKITI WA CHADEMA NA WANACHAMA 50 WATIMKIA CCM

 Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Kijiji cha Wangama, Fred Mgata (kulia) akikabidhi kadi za chyama hicho kwa Katibu wa CCM Mkoa wa Iringa, Hassan Mtenga baada ya yeye na wanachama wengine 50 wa Chadema kuamua kukihama na kujiunga CCM katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika  katika Kijiji hicho kilichopo Kata ya Luhota, Iringa Vijijini leo. Mgombea ubunge wa Jimbo la Kalenga kupitia Chadema ambaye ni mzaliwa wa kijiji hicho,  Grace Tendega alikuwa chini ya uongozi wa Mgata.
 Mgata akisalimiana na mgombea wa CCM Jimbo la Kalenga, Godfrey Mgimwa
 Mgata akipongezwa na wafuasi wa CCM kwa kitendo chake cha kuamua kuihama Chadema na kujiunga na CCM
 Ofisa wa Umoja wa Vijana wa CCM Makao Makuu, Mariana Shonzaakimuombea kura  mgombea ubunge wa CCM, Mgimwa.
 Katibu Mkuu wa CCM Mkoa wa Mtwara, Shaibu Akwilombe akihutubia katika mkutano wa kampeni katika Kijiji cha Wangama.
 Mgombea ubunge Jimbo la Kalenga kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Godfrey Mgimwa 9kulia) akilakiwa kwa shangwe na vigeregere na wananchi wa Kijiji cha Ikuvilo, Kata ya Luhota alipowasili kwa ajili ya mkutano wa kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo hilo leo Iringa Vijijini.
 Mgombea ubunge Jimbo la Kalenga kupitia CCM, Godfrey Mgimwa (wa pili kushoto) na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa, Joyce Msambatavangu wakiungana na wananchi wa Kijiji cha Wangama alichozaliwa mgombea ubunge wa Chadema, Grace Tendega, wakati wa mkutano wa kampeni katika Kata ya Luhota, Iringa Vijijini leo.
 Baadhi ya mabalozi wa CCM wa Kijiji cha Wangama wakinyoosha juu mikono ikiwa ni ishara ya kukubali kumpigia kura mgombea ubunge Jimbo la Kalenga kupitia chama hicho, Godfrey Mgimwa, wakati wa mkutano wa kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo hilo utakaofanyika Machi 16, mwaka huu.
 Mkazi wa Kijiji cha Wangama akifurahia sera za CCM zilizokuwa zinatolewa kwenye mkutano huo.
 Katibu wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM Wilaya ya Arusha Mjini, Rehema Mohamed akionesha moja ya majeraha  yaliyvyomuathiri mguuni wakati wa vurugu zilizofanywa katika maandamano ya Chadema mkoani Arusha. Rehema ambaye kabla ya kuhamia CCM alikuwa Diwani wa Chadema, alikuwa akihutubia katika mkutano wa kumnadi mgombea ubunge Jimbo la Kalenga kupitia CCM, Godfrey Mgimwa leo katika Kijiji cha Ikuvilo, katika Kata ya Luhota, Iringa Vijijini leo.
 Mfuasi wa CCM, Sabinus Segerela akishangilia baada ya kufurahishwa na hotuba ya mgombea ubunge Jimbo la Kalenga, Godfrey Mgimwa katika mkutano wa kampeni katika Kijiji cha Ikuvilo, Kata ya Luhota, Iringa Vijijini leo.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM Taifa, Seif Shaaban Mohamed, akihutubia katika mkutano wa kampeni za CCM za kumnadi mgombea ubunge Jimbo la Kalenga, Godfrey Mgimwa katika katika Kijiji cha Ikuvilo, Kata ya Luhota, Iringa Vijijini leo. (PICHA ZOTE NA KAMANDA WA MATUKIO BLOG.

No comments: