Helkopta iliyokuja na Rais Kikwete ikitua eneo la daraja la Dumila mkoani Morogoro leo.
Rais Kikwete akisalimiana na bibi mmoja wa kijiji cha Magole.
Rais Kikwete akiongea na wakazi wa Magole leo.
RAIS Dk. Jakaya Kikwete leo ametua kwa helikopta kijijini Magole, Dumila ili kukagua daraja lililoharibiwa na mvua pamoja na kuongea na wananchi wa eneo hilo waliokumbwa na mafuriko yaliyotokea Januari 22, mwaka huu wilayani Mvomero, Morogoro.
(PICHA NA DUSTAN SHEKIDELE / GPL)
No comments:
Post a Comment