Friday, January 31, 2014

MH. MIGIRO AITEMBELEA TUME YA KUREKEBISHA SHERIA TANZANIA

 Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanazania,Mh. Jaji Aloysius Mujulizi (kushoto) akimpokea Waziri wa Katiba na Sheria,Mh. Dkt. Asha Rose Migiro wakati alipokuwa akiwasili kwenye ofisi za Tume hiyo na kukutana na Watumishi wa Tume,jijini Dar es Salaam.Anaefuata nyuma ya Mh. Migiro ni Naibu Waziri wa Katiba na Sheria,Mh. Angela Kairubi.
 Waziri wa Katiba na Sheria Mh. Asha Rose Migiro (kushoto) akipokea maua kutoka kwa Afisa Tawala wa Tume Bi. Suzan Magoti.
 Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Asha Rose Migiro akipokea Ripoti zilizofanyiwa kazi na Tume kutoka kwa Katibu Mtendaji wa Tume Bi. Winfrida Korosso 
 Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Asha Rose Migiro akizungumza wakati wa kikao chake na uongozi wa Tume  
 Mwenyekiti wa Tume akizungumza wakati Waziri wa Katiba na Sheria  Mhe Asha Rose alipoitembelea Tume
 Baadhi ya Watumishi wa Tume wakiwa katika kikao na Mhe Waziri wa Katiba na Sheria.Picha Zote na Munir Shemweta, Ofisa Habari wa Tume.

No comments: