Monday, December 23, 2013

SEGEREA VETERANS WAANDA BONANZA YA KUMKUMBUKA MCHEZAJI MWENZAO ALIYEFIA UWANJANI

 Marehemu Jacob Arid kwa jina maarufu Oming'o enzi za uhai wake
Familia ya Marehemu Oming'o ikiwa uwanjani wakati wa bonanza lililopewa jina la OMING'O SOCCER BONANZA kwa ajili ya kumbukumbu ya marehemu Jacob Arid kwa jina maarufu Oming'o   lililofanyika kwenye kiwanja cha Segerea siku ya jumapili December 22, 2013 . Marehemu ameacha mjane na watoto wanne.
 Msemaji wa Timu ya Segerea Veterans Sports Club akizungumza jambo wakati wa bonanza lililofanyika kwa ajili ya kumkumbuka mchezaji mwenzao aliyefariki akiichezea timu hiyo katika uwanja wa Segerea ulioko Tabata jijini Dar es Salaam
 Timu kapteni wa Segerea Veterans Sports Club akizungumza na vyombo vya habari wakati wa bonanza la OMING'O SOCCER BONANZA lililofanyika jana kwenye kiwanja cha Segerea, Tabata jijini Dar es Salaam hapo jana.
 Mechi zikiendelea wakati wa bonanza la kumkumbuka mchezaji mwenzao aliyefariki uwanjani akiichezea timu yake ya Segerea Veterans Sports Club
 Mchezaji wa timu ya Kigamboni akiwa ameumia wakati wa nusu fainali ya kwanza
 Ilikuwa ni furaha baada ya timu ya Kigamboni kuingia Fainali
 Ubishi katika mechi kama hizi huwa haukosekani lakina refa ndo ana maamuzi yote
 Wachezaji wa timu ya Segerea Veterans Sports Club wakishangilia baada ya kushida ubingwa wa bonanza la OMING'O SOCCER BONANZA lililofanyika kwenye kiwanja cha Segerea kwa ajili ya kumkumbuka mchezaji mwenzao Oming'o aliyefariki akiichezea timu hiyo ya Segerea Veterans Sports Club
 Wachezaji wa timu ya Segerea Veterans Sports Club baada ya kushinda fainali hiyo walielekea meza kuu ilipokuwa picha ya mchezaji mwenzao marehemu Jacob Arid kwa jina maarufu Oming'o na kumwombea mungu ampumzishe mahali pema.
 Hapa ni furaha  kwa timu ya Segerea Veterans Sports Club baada ya kuchukua ubingwa
Mmoja wa mashabiki wa timu ya Segerea Veterans Sports Club akiwa amebeba picha ya marehemu Jacob Arid kwa jina maarufu Oming'o baada ya kumalizika kwa bonanza hilo

No comments: