Tuesday, September 10, 2013

kinana awakuna wakazi wa kahama kwa hotuba yake,avuna wanachama zaidi kutoka upinzani.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kishepu Ndugu Isabela Chilumba  wakati wa mapokezi yake katika kata ya Isaka.

Wakazi wa Isaka wakiwasikiliza viongozi wa CCM Taifa waliowasili mkoani Shinyanga leo kwa ziara ya siku nne.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwahutubia wakazi wa Isaka na kuwaambia muda wa kudanganyika na wanasiasa uchwara umefikia kikomo.
 Mwanachama wa CCM akifurahia hotuba ya Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Isaka.
 Mbunge wa Msalala Ndugu Ezekiel Maige akizungumza na wakazi wa Isaka wakati wa mkutano wa hadhara .




 Wana CCM wa Isaka wakishangilia hotuba ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Ndugu Hamisi Mgeja kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Isaka .

 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akishiriki kufyatua matofali ya ujenzi wa tanki la maji katika kijiji cha Kagongwa kata ya Kagongwa.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongea na wananchi wa kijiji cha Mwendakulima baada ya kuzindua awamu ya kwanza ya ujenzi wa kituo cha afya kilichodhaminiwa na kampuni ya uchimbaji wa madini ya Africa Barrick Gold.
 Katibu Mkuu akishiriki kupanda mti katika kituo cha afya kilichodhaminiwa na mgodi wa Buzwagi chini ya kampuni ya Africa Barrick Gold .
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akimwagia maji mti alioupanda kwenye kituo cha afya katika kijiji cha Mwendakulima.
 Katibu Mkuu wa CCM akishiriki kupiga lipu ofisi ya kata ya Majengo katika wilaya ya Kahama.
 Katibu Mkuu wa CCM akifungua SACCOS ya Mkombozi ya vijana wa CCm mjini Kahama ambapo aliwezesha kutatua masuala yote ya msingi yanayowakabili vijana hapo, hasa yanayohusu elimu ya uraia , uchumi ,elimu za ufundi ambapo vijana kumi watapata nafasi ya kulipiwa na Katibu Mkuu na masuala ya maeneo ya kufanya shughuli za biashara.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdul Rahman Kinana akiingia ukumbini kwa ajili ya kufanya mkutano na mabalozi wa nyumba kumi kwenye ukumbi wa Halmashauri  ya Kahama.
 Katibu wa NEC Nape Nnauye akiingia kwenye uwanja wa CDT tayari kwa kuhutubia mkutano wa hadhara.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasili kwenye kiwanja cha CDT kwa ajili ya kutubia wakazi wa Kahama.
 Katibu Mkuu wa CCM Taifa Abdulrahman Kinana akiwapongeza wacheza sarakasi waliokuja kumsabahi kwa staili ya kipekee kabisa.

No comments: