Thursday, August 1, 2013

UNIC YAHAMASISHA VILABU VYA KUJISOMEA KWA SHULE ZA MSINGI

IMG_1445
Afisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa nchini (UNIC) Stella Vuzo akielezea jukumu lao kubwa wao kama Unic ni kuelimisha jamii ambapo kwa kufanya hivyo wamehamasika kuanzisha vilabu vya kujisomea kwa shule za msingi vitakavyowajengea watoto msingi mzuri wa kupenda kujisomea ili kufahamu mambo mengi zaidi yanayoendelea duniani katika nyanja ya Sayansi, Teknolojia na habari.
IMG_1488
Msaidizi wa Maktaba ya UNIC Harriet Macha ( wa tatu kushoto) na Mkurugenzi wa Taasisi ya Soma Book Café , mshiriki katika kuhamasisha uanzishwaji wa Klabu za Kujisomea mashuleni Mama Demere Kitunga ( wa nne kushoto) wakikabidhi vitabu vya kujisomea kwa walimu na baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa nchini (UNIC) kwa kushirkiana na Soma Book Café walihamasisha kuanzishwa kwa Klabu za Kujisomea katika shule tatu za msingi ambazo ni Hananasif, Kumbukumbu na Oysterbay ili kujenga tabia ya kujisomea kwa watoto tangu utotoni. Klabu ya Kujisomea ya Shule ya Msingi Oysterbay imezinduliwa rasmi jana tarehe 31 Julai 2013 kwa kukabidhiwa mashelfu na vitabu vilivyotolewa na Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Soma Book Café pamoja na Book Aid International kupitia Maktaba Kuu ya Taifa.
IMG_1498
Afisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa nchini (UNIC) Stella Vuzo akishiriki zoezi hilo la kukabidhi vitabu kwa baadhi ya wanafunzi wa shule ya Msingi Oysterbay wakihamasisha wanafunzi kujenga tabia ya kujisomea tangu wakiwa wadogo.
IMG_1494
Afisa Habari wa UNIC Usia Nkhoma Ledama naye alishiriki zoezi hilo.
IMG_1508
Mwalimu Salome Makanza (kushoto) akitoa shukrani kwa kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa nchini (UNIC) kwa msaada huo ambapo waliahidi kuleta mabadiliko ya maendeleo kwa wanafunzi wao kujijengea tabia ya kujisomea na hata kuongeza ufaulu kwa matokeo ya darasa la saba shuleni hapo. Katikati ni Msaidizi wa Maktaba ya UNIC Harriet Macha na kulia ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Soma Book Café , mshiriki katika kuhamasisha uanzishwaji wa Klabu za Kujisomea mashuleni Mama Demere Kitunga.
IMG_1398
Msaidizi wa Maktaba ya UNIC Harriet Macha akitoa ushauri wa namna ya upangaji vitabu kwa Msimamizi wa Maktaba ya shule hiyo Mwl. Veronica Kassidy.
IMG_1401
Unic team wakijikumbushia baadhi ya vitabu walivyowahi kuvisoma walipokuwa shule za msingi.
IMG_1415
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Oysterbay wakichagulia vitabu vya kujisomea katika maktaba ya shule yao.
IMG_1513
Mkurugenzi wa Taasisi ya Soma Book Café , mshiriki katika kuhamasisha uanzishwaji wa Klabu za Kujisomea mashuleni Mama Demere Kitunga na Afisa Habari wa UNIC Stella Vuzo wakiteta jambo na baadhi ya wanafunzi wa shule mara baada ya kumaliza zoezi la kukabidhi vitabu wanafunzi hao.

No comments: