Saturday, July 20, 2013

ZIARA YA WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA WILAYA YA SONGEA VIJIJINI

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na mkewe Tunu (kushoto) wakisalimiana na Madwani wa Songea Vijijini baada ya kuwasli kwenye kijiji cha Mkenda kuweka jiwe la Msingi la Soko wakiwa katika ziara ya mkoa wa Ruvuma Julai 19,2013.
Wananchi wa Songea Vijijini wakicheza ngoma ya Lizombe wakti Waziri Mkuu,Mizengo Pinda alipoweka jiwe la Msingi la ujenzi wa soko na kuhutubia wananchi katika kijiji cha Mkenda akiwa katika ziara ya mkoa wa Ruvuma Julai 19,2013.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara , Joyce Mapunjo wakiweka jiwe la msingi la ujenzi wa soko katika kijiji cha Mkenda wialyani Songea Vijijini Julai 19, 2013. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Katibu Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Joyce Mapunjo kabla ya kuweka jiwe la msingi la soko katika kijiji cha Mkenda wilayni Songea Vijijini akiwa katika ziara ya mkoa wa Ruvuma.Katikati ni Mbunge wa Peramiho,Jenista Mhagama.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwaaga wananchi wa Kijiji cha Mkenda, Songea Vijijini baada ya kuweka jiwe la msingi kijijini hapo akiwa katika ziara ya mkoa wa ruvuma Jaulai 19, 2013. Katikati ni Mkewe Tunu na kulia ni Mkuu wa mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na askari wa Msumbiji wakati alipopita kwenye mpakakati ya nchi hiyo na Tanzania katika kijiji cha Mkenda akiwa katika ziara ya mkoa wa Ruvuma Julai 19,2013.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Mkewe Tunu wakiteta na Mbunge wa Peramiho, Jenista Mhagama (kushoto) baada ya kuwasili kwenye kijiji cha Mpitimbi kuzindua msimu wa ununuzi wa mahindi Julai 19, 2013. Walikuwa katika ziara ya mkoa wa Ruvuma.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akipima katika mzani gunia la mahindi kuashiria uzinduzi wa msimu wa ununuzi wa mahindi katika kijiji cha Mpitimbi akiwa katika ziara ya mkoa wa Ruvuma Julai 19, 2013. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Mpitimbi wailayani Songea Vijijini Julai 19, 2013 baada yakuzindua msimu wa ununuzi wa mahindi akiwa katika ziara ya mkoa wa Ruvuama.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiagana na wazee wa Songea baada ya kuzungumza nao kwenye Ikulu ndogo ya Songea akiwa katika ziara ya mkoa wa Ruvuma Julai 19, 2013.

No comments: