Saturday, July 13, 2013

Mfuko wa Starkey Hearing watoa huduma za kutibu masikio kwa wakazi wa Dar

Mwanzilishi wa Mfuko wa Starkey Hearing William Austin (kulia) akisaidiana na Mkewe Tani Austin(kushoto) kumuvalisha kifaa cha kumwezesha kusikia mtoto Lilian Vincent (leo) jijini Dar es salaam wakati Mfuko huo ulipoendesha huduma ya kutoa vifaa vya kusaidia kusikia kwa watu wenye matatizo ya kusikia ambayo wanatarajia kuitoa kwa wakazi wa Dar es salaam zaidi 2000 kwa muda wa siku nne katika Hoteli ya Serena.
Mwanzilishi wa Mfuko wa Starkey Hearing William Austin (kulia) akisaidiana na Mkewe Tani Austin(kushoto) kumuvalisha kifaa cha kumwezesha kusikia mtoto Malechela Juma (katikati) leo jijini Dar es salaam wakati Mfuko huo ulipoendesha huduma ya kutoa vifaa vya kusaidia kusikia kwa watu wenye matatizo ya kusikia ambayo wanatarajia kuitoa kwa wakazi wa Dar es salaam zaidi 2000 kwa muda wa siku nne katika Hoteli ya Serena.
Mwanzilishi wa Mfuko wa Starkey Hearing William Austin akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam juu ya huduma ya vifaa vya kusaidia kusikia kwa watu wenye matatizo ya kusikia ambayo wanatarajia kuitoa kwa wakazi wa Dar es salaam zaidi 2000 kwa muda wa siku nne katika Hoteli ya Serena.
Baadhi ya wakazi na watoto kutoka sehemu mbalimbali za jiji la Dar es salaam wakiwa katika foleni ya kupatiwa matibabu ya huduma ya vifaa vya kuwasaidia kusikia kutoka Mfuko wa Starkey Hearing leo jijini Dar es salaam. Mfuko huo umeweka kambi katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam ambapo wanatarajia kutoa huduma hiyo bure kwa watu zaidi ya 2000 kwa kipindi cha nne.
Mwanzilishi wa Mfuko wa Starkey Hearing William Austin (wa tatu kutoka kulia) akiwa amemkumbatia Mkewe Tani Austin leo jijini Dar es salaanm katika picha ya pamoja na Teddy Mapunda (wa pili kutoka kulia) wakati wa zoezi la utoaji wa vifaa vya kuwasaidia kusikia kusikia kwa watu wenye matatizo ya kusikia wa jiji la Dar es salaam ambayo itatolewa kwa wakazi zaidi ya 2000 kwa muda wa siku nne katika Hoteli ya Serena.
Baadhi ya wafanyakazi wa Hoteli ya Serena wakishirikiana na wafanyakazi wa Mfuko wa Starkey Hearing kuwavisha vifaa cha kuwawezesha kusikia wakazi mbalimbali wa jijini Dar es salaam leo wakati Mfuko huo ulipoendesha huduma ya kutoa vifaa vya kusaidia kusikia kwa watu wenye matatizo ya kusikia ambayo wanatarajia kuitoa kwa wakazi wa Dar es salaam zaidi 2000 kwa muda wa siku nne.
Mtalaam wa kusafisha masikio Dkt. Leigh Kassneo akimsafisha sikio mtoto Rashid Said leo jijini Dar es salaam kabla ya kupata huduma ya kuchunguzwa na kupatiwa vifaa vya kumwezesha kusikia wakati Mfuko wa Starkey Hearing ulipoendesha zoezi la kusaidia vifaa watu wenye matatizo ya kusikia ambapo wanatarajia kutoa kwa wakazi wa Dar es salaam zaidi ya 2000 kwa muda wa siku nne katika Hoteli ya Serena.Picha na MAELEZO_ Dar es salaam.

No comments: