Friday, May 17, 2013

IMEELEZWA VIONGOZI NDIYO CHANZO CHA UVUJAJI WA SIRI MAKAZINI NA SI MASEKRETARI.

Mtoa mada iliyohusu Maadili kazini,Bwa.Alex Senzota kutoka Idara ya Usalama Kazini (GSO),akifafanua zaidi kuhusiana na mada iliyohusu Maadili kazini na namna ya kutunza/kuepuka uvujaji wa siri za ofisi husika,mapema leo kwenye Kongamano la Tatu la Makatibu Muhtasi (Tanzania Personal Secretaries Association - TAPSEA) uliofanyika ndani ya  ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa Arusha (AICC), Jijini Arusha.
Mwenyekiti wa Chama chama cha Makatibu Muhtasi  Nchini Uganda (NASAP),Bi Edith Kutesa Giita akifafanua jambo kuhusiana na mada mojawapo ya iliyohusu Ni namna gani unaweza kuwa Katibu Muhtasi unaekwenda na wakati/wa kisasa,mapema leo kwenye Kongamano la Tatu la Makatibu Muhtasi (Tanzania Personal Secretaries Association - TAPSEA) lililofanyika ndani ya  ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa Arusha (AICC), Jijini Arusha.

 Mwenyekiti wa chama cha Makatibu Muhtasi  (Tanzania Personal Secretaries Association - TAPSEA),Bi Pili Mpenda akifafanua jambo mbele ya washiriki wa Kongamano la Tatu la Makatibu Muhtasi  likiendelea ndani ya  ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa Arusha (AICC), Jijini Arusha,kulia kwake ni Mwenyekiti wa Chama chama cha Makatibu Muhtasi  Nchini Uganda (NASAP),Bi Edith Kutesa Giita.


 
Baadhi washiriki wa Kongamano la Tatu la Makatibu Muhtasi (Tanzania Personal Secretaries Association - TAPSEA) wakifuatilia kwa makini mada mbalimbali zinazojadiliwa  kwenye kongamano hilo lililofanyika dani ya  ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa Arusha (AICC), Jijini Arusha. 
  Mmoja wa wachangia mada kutoka chuo  cha Sokoine,Bi Teddy Salum akizungumza kuhusiana na mada iliyohusu Maadili kazini na namna ya kutunza/kuepuka uvujaji wa siri za ofisi,wakati Kongamano la Tatu la Makatibu Muhtasi (Tanzania Personal Secretaries Association - TAPSEA) likiendelea ndani ya  ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa Arusha (AICC), Jijini Arusha.
 Mmoja wa wachangia mada kutoka chuo Kikuu cha Dar- Es Salaam (UDSM),akifafanua jambo kuhusiana na mada iliyohusu Maadili kazini na namna ya kutunza/kuepuka uvujaji wa siri za ofisi,wakati Kongamano la Tatu la Makatibu Muhtasi (Tanzania Personal Secretaries Association - TAPSEA) likiendelea ndani ya  ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa Arusha (AICC), Jijini Arusha.
Sehemu ya washiriki wa Kongamano la Tatu la Makatibu Muhtasi (Tanzania Personal Secretaries Association - TAPSEA) wakifuatilia kwa makini mada mbalimbali zinazojadiliwa  kwenye kongamano hilo lililofanyika dani ya  ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa Arusha (AICC), Jijini Arusha.

=============  =======  ===========

IMEELEZWA VIONGOZI NDIYO CHANZO CHA UVUJAJI WA SIRI MAKAZINI NA SI MASEKRETARI.

Suala la uvujaji kwa siri kwa baadhi ya sehemu kubwa ya maofisi makazini,imeelezwa kuwa chanzo kikubwa ni viongozi na si makatibu Muhtasi kama ambavyo baadhi  ya watu  wamekuwa wakieleza.

Hayo yameelezwa leo kwenye siku ya pili ya Kongamano la Tatu la Makatibu Muhtasi (Tanzania Personal Secretaries Association - TAPSEA) uliofanyika ndani ya  ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa Arusha (AICC), Jijini Arusha.

Akizungumza mbele ya wageni waalikwa mbalimbali, mtoa mada iliyohusu Maadili kazini,Bwa.Alex Senzota kutoka Idara ya Usalama Kazini (GSO),alipata wakati mgumu wa kujibu maswali kutoka kwa washiriki wa kongamano hilo kuhusiana na mada hiyo iliyozua mjadala mkubwa ukumbini humo.

Mmoja wa washiriki katika kongamano  hilo aliyejitambulisha kwa jina la Teddy Salum kutoka chuo cha Sokoine,alieleza kuwa tatizo kubwa la uvujaji siri kwa asilimia kubwa linatokana na Viongozi wenyewe kutokana na itikadi zao za kisiasa ama ya kutaka umaarufu.

Aidha Mshiriki Mwingine alibainisha kuwa tatizo hilo la uvujaji siri maofisini linatokana na  baadhi ya viongozi a.k.a MABOSS kutozingatia/kupuuza ama kutokuwa na maadili ya kazi katika kuhakikisha siri za ofisi husika zinatunzwa ipasavyo,ili kulinda usalama wa ofisi husika.

Mtoa Mada wa Maadili kazini,Bwa.Alex Senzota alifafanua kuwa kutokana na tatizo hilo kubainika kuwa kubwa katika kongamano hilo,kuna haja ya Serikali kuangalia mfumo mzima wa kuhakikisha maadili ya kazi yanazingatiwa katika Nyanja zote zote,hasa kwa watumishi wa umma.

Kongamano hilo la siku mbili, limehudhuriwa na Makatibu Muhtasi zaidi ya 1,500 kutoka mikoa yote nchini, na baadhi ya wawezeshaji kutoka Kenya, Uganda na Rwanda.

No comments: