Monday, April 1, 2013

PROFESA JAY NA FID Q WAFUNIKA KATIKA TAMASHA LA VODACOM COCO BEACH


Msanii mahiri wa mziki wa kizazi kipya,Profesa Jay akiwapagawisha mashabiki waliofurika katika Tamasha la wazi la Vodacom, lililofanyika katika Ufukwe wa bahari ya hindi Coco Beach, jijini Dar  es Salaam,lilohudhuriwa na mashabiki lukuki,waliokwenda kujionea burudani hizo ambapo pia walitumia fursa hiyo kwa kuelimishwa juu ya huduma mbalimbali zinazotelewa na mtandao wa Vodacom.
Msanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya Fid Q,akiandaa muziki katika kompyuta yake ndogo (lap top) wakatiwa Tamasha la wazi la Vodacom Tanzania, lililofanyika katika Ufukwe wa Coco Beach, jijini Dar es Salaam,lilohudhuriwa na mashabiki lukuki, waliokwenda kujionea burudani ambapo pia walitumia fursa hiyo kwakuelimishwa juu ya huduma mbalimbali zinazotelewa na mtandao wa Vodacom,wanaoshuhudia kutoka kulia ni Msanii machachari Dar Stamina  na Afisa Udhamini na Matukio wa Vodacom Tanzania,Ibrahim Kaude.
Umati wa mashabiki wa muziki wa kizazi kipya wakipagawa na muziki wakati wa Tamasha la wazi la Vodacom Tanzania, lililofanyika katika Ufukwe wa Coco Beach, jijini Dar es Salaam,lilohudhuriwa na mashabiki lukuki, waliokwenda kujionea burudani hizo ambapo pia walitumia fursa hiyo kwa kuelimishwa juu ya huduma mbalimbali zinazotelewa na mtandao wa Vodacom.
Wafanyakazi wa Kampuni ya Samsung wakiwa tayari kwa kutoa huduma mbalimbali zilizokuwa zikipatikana ikiwemo na uuzaji wa simu za bei rahisi za Tsh 70,000 na 100,000 ikiwani sehemu ya ofa ya Tamasha la wazi la Vodacom Tanzania, lililofanyika katika Ufukwewa Coco Beach, jijini Dar es Salaam.
Msanii wa Hip Pop nchini mzee wa michano Fid Q akichana vilivyo wakati wa Tamasha la wazi la Vodacom Tanzania, lililofanyika katika Ufukwe wa Coco Beach, jijini Dar es Salaam.
Msanii nguli wa muziki wakizazi kipya nchini,Joseph Haule maarufu kama Profesa Jay akipanda jukwani tayari kwa kukonga nyoyo za mashabiki wake kwenye Tamasha la wazi la Vodacom Tanzania, lililofanyika katika Ufukwewa Coco Beach, jijini Dar es Salaam.
Msanii mahiri wa Hip Pop nchini Fid Q a.k.a Ngosha akiingia katika steji wakati wa Tamasha la wazi la Vodacom Tanzania, lililofanyika katika Ufukwe wa Coco Beach, jijini Dar es Salaam.
Msanii wa kizazi kipya wa muziki wa Hip Pop nchini,Dar Stamina akiwapagawisha mashabiki walio furika katika ufukwe wa CoCo Beach katika Tamasha la wazi la Vodacom Tanzania, lililofanyika jana katika Ufukwe huo, jijini Dar esSalaam.
Baadhi ya mashabiki wakifuatilia jinsi wanamuziki walivyokuwa wanachana katika Tamasha la wazi la Vodacom Tanzania, lililofanyika jana katika Ufukwewa Coco Beach, jijini Dar es Salaam.


MKALI wamuziki wa Hip Hop nchini, Joseph Haule, maarufu kama Profesa Jay, juzi alifanya makubwa katika tamasha la wazi lililoandaliwa na Kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania nakufanyika katika Ufukwe wa Coco Beach.

Mbali na Jay, wengine waliokuwapo na kufanya makubwa katika tamasha hilo lililohudhuriwa na watu wengi, alikuwapo Dar Stamina na Fid Q, ambapo wote kwa pamoja walifanikiwa kuwapatia burudani za aina yake.

Tamasha hilo lililofanyika maalum katika Sikukuu ya Pasaka, liliandaliwa maalum kwa ajili ya kusherehekea na wateja wao, pamoja na kuelimishwa kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na kampuni ya hiyo, ikiwapo Cheka Nao na promosheni ya Mahela, inayowawezesha wateja kujishindia pesa taslimu.

Akizungumza katika tamasha hilo, AfisaUdhamini na Matukio wa Vodacom Tanzania, Ibrahim Kaude, aliwashukuru Watanzania kwenda kwa wingi katika tamasha hilo la bure na kushiriki pamoja katika tukio hilo la kiburudani.

Alisema kuwa katika tamasha hilo, wateja wao walikuwa wakipewa elimu jinsi mtandao wao unavyofanyakazi, ikiwapo kujulishwa kwa huduma mbalimbali zinazotolewa na kampuni hiyo kwa kupitia tukio hilo lililofurika watu wengi.

"Sisi kama Vodacom tunashukuru kuwa pamoja na mashabiki wa muziki katika tukio hili la wazi lililoandaliwa mahususi kwa ajili yao, huku tukiamini kuwa tutaendelea kuwa pamoja kwa huduma mbalimbali zinazotolewa.

"Tunawaahidi kufanya kazi kwa moyo, pamoja na kuendeleza promosheni zenye mguso wa aina yake, ikiwapo hii ya Vodacom Mahela, ambapo wateja wetu wanapata fursa ya kujishindia fedha taslimu kutoka kwetu," alisema Kaude.

Aidha, msanii Profesa Jay alikuwa wa kwanza kupanda jukwaani kuwapatia burudani mashabiki wake na kuungwa mkono, sambamba na kuwaimbisha kila wimbo aliotaka kuimba katika tamasha hilo lililokuwa na mvuto wa aina yake.

Baada ya kushuka kwa msanii huyo, alitoa fursa ya Stamina kupanda, huku dakika kumi baadaye, Fid Q naye alipanda na kufanya shoo pamoja na mkali huyo wa Hip Hop anayekubalika na watu wengi kutokana na nyimbo zake kali, ukiwapo wa 'Kabwela'.

Tamasha la wazi la Vodacom lililofanyika kwa siku mbili katika ufukwe huo wa Coco Beach, ambapo wateja wao wote walipata fursa ya kushuhudia burudani hiyo bila kutoa kiingilio cha aina yoyote.

No comments: