Tuesday, January 15, 2013

MWANRI AMALIZA ZIARA YAKE YA SIKU SABA MKOANI RUKWA, ASEMA HALMASHAURI ZITAKAZOPATA HATI CHAFU KUTOPATA RUZUKU SERIKALINI


Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Ndugu Agrey Mwanri akitoa maelekezo mbalimbali kwa uongozi wa Mkoa wa Rukwa katika majumuisho ya ziara yake iliyodumu kwa muda wa siku saba Mkoani Rukwa ambapo alitembelea miradi zaidi ya 22 ambayo baadhi yake aliiwekea mawe ya msingi. Katika hotuba yake hiyo alitoa maagizo mbalimbali ambayo yote yalikuwa yakilenga kwenye utawala bora, matumizi bora ya fedha za Serikali katika miradi pamoja utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010. Katika hotuba yake iliyodumu kwa zaidi ya saa tatu alizionya halmashauri zote nchini zitakazopata hati chafu kuwa hazitapata fedha ya ruzuku ya miradi ya maendeleo (LGCDG-Local Government Capital Development Grant) ikiwa ni kutoa funzo kwa watendaji wa halmashauri pamoja na kupandisha hasira za madiwani ili waweze kuisimamia vizuru halmashauri husika. 
Mama Grace Mwanri, mke wa Naibu Waziri wa TAMISEMI Agrey Mwanri akitoa ushuhuda kuhusu utendaji wa mumewe "Anavyoongea na kutenda mume wangu ndivyo alivyo hata nyumbani na si kwamba anafanya hivyo kupata sifa wala umaarufu kwani mara zote huwa hapendi mambo ya kipuuzipuuzi" alisema mama Mwanri.
Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Alhaj Salum Mohammed Chima akizungumza kuwatambulisha wageni na washiriki katika kikao hicho cha majumuisho kwa mgeni rasmi Ndugu Agrey Mwanri kushoto. Katika hotuba yake fupi alimuhakikishia Naibu Waziri kuwa maagizo yote aliyoyatoa kwenye ziara yake yatafanyiwa kazi na kwamba miradi iliyokuwa na mapungufu itarekebishwa.
Naibu Waziri Mwanri akizungumza na washiriki wa kikao hicho ambacho kilihudhuriwa na makundi mbalimbali wakiwemo viongozi wa Dini, Chama na Serikali. Taasisi za Umma, mashirika binafsi, wajasiriamali, na watumishi mbalimbali wa halmashauri na taasisi za Umma.
Sehemu ya washiriki wa kikao hicho katika ukumbi wa RDC katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa wakifuatilia hotuba ya majumuisho ya Ndugu Mwanri.
Kutoka kushoto ni Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasilimali Watu Mkoa wa Rukwa Ndugu Samson Mashalla na Kaimu Katibu Tawala Wilaya ya Sumbawanga Ndugu Festo Chonya wakifuatilia kikao hicho.
Baadhi ya wadau walioshiriki kikao hicho wakifuatilia kwa makini, wa kwanza kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga Ndugu Godfrey Shona, Kaimu Mkurugenzi manispaa ya Sumbawanga, Mbunge Mst. na muwekezaji wa ndani Ndugu Chrissant Majiyatanga Mzindakaya na kwa kwanza kulia ni muwekezaji wa ndani Ndugu Reina Lukara.
Naibu Waziri wa TAMISEMI Agrey Mwanri akimkabidhi maagizo yatokanayo na ziara yake ya siku saba Mkoani Rukwa Katibu Tawala wa Mkoa huo Alhaj Salum Mohammed Chima aweze kuyafanyia kazi katika Mkoa wake.
Naibu Waziri wa TAMISEMI Agrey Mwanri akimkabidhi maagizo yatokanayo na ziara yake ya siku saba Mkoani Rukwa Mkuu wa Wilaya ya Kalambo Ndugu Moshi Chang'a aweze kuyafanyia kazi katika Wilaya yake.
Naibu Waziri wa TAMISEMI Agrey Mwanri akimkabidhi maagizo yatokanayo na ziara yake ya siku saba Mkoani Rukwa Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Ndugu Idd Kimanta aweze kuyafanyia kazi katika Wilaya yake.
Naibu Waziri wa TAMISEMI Agrey Mwanri akimkabidhi maagizo yatokanayo na ziara yake ya siku saba Mkoani Rukwa Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Ndugu Mathew Sedoyeka aweze kuyafanyia kazi katika Wilaya yake. (Picha na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa).

No comments: