Thursday, July 26, 2012

Maadhimisho ya kumbukumbu ya mashujaa mjini Songea

 Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Mhe. Said Mwambungu akipokea heshima kutoka kwa askari na maafisa wa jeshi la wananchi tanzania wakati wa maadhimisho ya siku ya mashujaa iliyofanyika katika viwanja vya makumbusho mjini Songea 
 Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Mhe. Said Mwambungu akielekea katika mnara wa kumbukumbu kuweka silaha ikiwa ni kuwakumbuka mashujaa wakati wa kilele cha siku ya mashujaa nchini
 Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Mhe. Said Mwambungu akiweka mkuki katika mnara wakati wa kilele cha siku ya  kumbukumbu ya mashujaa katika viwanja vya makumbusho mjini Songea
 Mkuu wa brigedi ya 401 Songea Kanali John Chacha akiweka moja ya silaha za jadi  katika mnara wa kumbukumbu ya mashujaa mjini Songea
 Mmoja wa Machifu wa kabila la Wangoni  akiweka silaha katika mnara wa kumbukumbu wakati wa maadhimisho ya mashujaa mjini songea
 Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu akibonyeza moja ya kitufe kilichoandaliwa na jwtz kwa ajili ya mlipuko wa heshima kuwaenzi mashujaa wakati wa kilele cha siku ya mashujaa katika viwanja vya makumbusho mjini songea 
  Baadhi ya askari wa jeshi la wananchi wa Tanzania wakito heshima wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya mashujaa mjini Songea
 Mkuu wa brigedi ya 401 Songea Kanali John Chacha (wa pili kushoto) akiwa na  baadhi ya viongozi wa serikali, Mkuu wa mkoa wa Ruvuma  Mhe.Said Mwambungu (wa pili kulia),katibu tawala msaidi mipango Bi Vestina Nguruse (kulia) na meya wa manispaa ya Songea Mstahiki Charles Mhagama wakitoa heshima wakati wa kilele cha siku ya mshujaa iliyofanyika katika viwanja vya makumbusho mjini Songea
 Mmoja wa viongozi wa dini akitoa dua huku akisaidiwa na askari wa JWTZ.
Gwaride likitoka nje baada ya kumaliza shughuli za maadhimnisho ya siku ya mashujaa katika viwanja vya makumbusho mjini songea

No comments: