Monday, April 16, 2018

SERIKALI IMEFANIKIWA KUDHIBITI MATUKIO YA UVUVI HARAMU NCHINI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba katikati akipanda moja kati ya mikoko ya miche 140,000 iliyotolewa na Kampuni ya Vodacom Foundation katika mikoa inazungukwa na bahari ya hindi ili kuzuia mabadiliko ya tabia ya nchi Jijini Tanga kulia ni  Mwakilishi wa Vodacom Foundation Rosalynn MworiaWaziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba katikati akipanda moja kati ya mikoko ya miche 140,000 iliyotolewa na Kampuni ya Vodacom Foundation katika mikoa inazungukwa na bahari ya hindi ili kuzuia mabadiliko ya tabia ya nchi Jijini Tanga kulia ni  Mwakilishi wa Vodacom Foundation Rosalynn Mworia 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba wa tatu kutoka kulia akiwa na Mwakilishi wa Vodacom Foundation Rosalynn Mworia kushoto wakitembela kwenye ufukwe wa bahari ya hindi mara baada ya kupanda moja kati ya mikoko iliyotolewa na Kampuni ya Vodacom Foundation katika mikoa inazungukwa na bahari ya hindi ili kuzuia mabadiliko ya tabia ya nchi Jijini Tanga. 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba katika akizungumza mara baada ya kupanda miti hiyo ya mikoko kushoto ni Mwakilishi wa Vodacom Foundation Rosalynn MworiaWaziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba kulia akimsikiliza kwa umakini Mwakilishi wa Vodacom Foundation Rosalynn Mworia katikati aliyekuwa akieleza dhamira yao ya kusaidia upandaji wa miti hiyo ya mikokoSehemu ya Wafanyakazi wa Kampuni ya Vodacom wakipiga selfie na WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) January Makamba mara baada ya kumaliza zoezi la upandaji wa miti ya mikokoWafanyakazi wa Kampuni ya Vodacom wakiwa kwenye picha ya pamoja na WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) January Makamba mara baada ya kumalzika kwa zoezi la upandaji wa miti ya mikoko


WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) January Makamba amesema serikali imefanikiwa kudhibiti matukio ya uvuvi haramu kwa zaidi ya asilimia 80 katika maeneo ya bahari na maziwa baada ya kuimarisha doria na ukaguzi wa samaki wanaovuliwa. 

Aliyasema hayo wakati wa upandaji wa mikoko katika Pwani ya Bahari ya Hindi ambayo ilipandwa eneo la Mwambani Jijini Tanga chini ya Udhamini wa Mfuko wa Vodacom (Vodacom Faundation). 

Alisema kuimarika kwa doria hizo kumesaidia wananachi kuwa na uelewa mpana kuhusu madhara ya uvuvi haramu na hivyo kuanz kuchukua hatua za kudhibiti hali hiyo ikiwemo ulinzi wa mazingira ya bahari ya hindi na rasilimali zake. 

Waziri huyo alisema pamoja na jitihada za wizara katika kudhibiti fukwe za bahari zinasiendelee kuathiriwa na mabadiliko ya tabia ya nchi lakini bado kuna maeneo mengi ambayo yanahitaji kuhifadhiwa kwa kupandwa miti ya mikoko. 

Pamoja na hayo Waziri huyo alitumia nafasi hiyo kuwashukuru Vodacom Foundation kwa kuja na kampeni ya upandaji wa mikoko ili kuhifadhi mazingira ya bahari kwa kile alichosema kuwa kutasaidia kuboresha mazingira hayo. 

Naye kwa upande wake Mwakilishi wa Vodacom Foundation Rosalynn Mworia alisema taasisi hiyo kwa kushirikiana na chama cha skauti Tanzania waliamua kuja na kampeni hiyo upandaji wa mikoko ili kuhifadhi mazingira ya Fukwe. 

Alisema kwamba kwa kuanzia kampeni hiyo wameanzia kwa mkoa wa Tanga na wanatarajia kuipeleka nchi nzima ili kuhamasisha utunzaji wa mazingira na kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi.(Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha) 

No comments: