Sunday, October 8, 2017

NHIF YATOA HUDUMA ZA UPIMAJI KWENYE BONANZA LA MICHEZO JIJINI TANGA LEO


 Afisa Mdhibiti wa Viwango na Ubora Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Mkoani Tanga,Dkt Lwi Kupaza akiangalia taarifa za moja ya wakazi wa Jiji la Tanga ambao walijitokeza kupima uzito,sukari na presha wakati wa bonanza la michezo ambalo limefanyika leo kwenye viwanja vya shule ya sekondari Popatlaly kushoto ni Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu
 Daktari wa NHIF kushoto akimpima presha Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu wakati wa bonanza la michezo
Afisa Mdhibiti Viwango na Ubora Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Dkt Lawi Kupaza akichukua maelezo ya Ofisa wa Polisi kutoka Ofisi ya RCO,Saidi Mwagara wakati wa bonanza hilo
Afisa Madai wa NHIF mkoani Tanga,Marry Daniel katikati aliyevaa tisheti ya njano akifuatilia taarifa wakati wa wananchi walipojitokeza kwenye banda lao kwenye bonanza la michezo ambalo lilifanyika viwanja wa shule ya Sekondari Popatlaly kupima afya 

Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga(Ras) Mhandisi Zena Saidi akiwa kwenye banda la Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) kuangalia zoezi la upimaji wa afya kwa wanamichezo 150 waliweza kupima afya ambapo kati yao
waliokuwa na uzito mkubwa 65,waliokutwa na sukari juu wanne,waliokuwa na Presse sita na wasiokuwa na matatizo 75
 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga (RPC) Benedict Wakulyamba akiwaongoza askari wa Jeshi hilo kuwavuta kamba Bandari Tanga wakati wa Bonanza hilo leo
 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga (RPC) Benedict Wakulyamba akiwaongoza askari wa Jeshi hilo kuwavuta kamba Bandari Tanga wakati wa Bonanza hilo leo
 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga (RPC) Benedict Wakulyamba kulia akifurahia jambo wakati wa bonanza hilo
 Ofisa Uhamiaji wa Mkoa wa Tanga,Crispin ngonyani akiwaongoza idara hiyo kuvuta kamba kwenye bonanza hilo.
 wa Pili kutoka kushoto ni Afisa wa NHIF Mkoa wa Tanga akiteta jambo na wanamichezo walioshiriki bonanza hilo leo.
 Afisa Madai wa NHIF mkoani Tanga,Marry Daniel kulia kushoto ni Afisa Madai wa Mfuko huo pia Petro Aloyce wakigawa vipeperushi vinavyohamasisha huduma wanazozitoa kwa wanamichezo.
 Afisa Madai wa NHIF mkoani Tanga,Marry Daniel kulia akiendelea kuwahamaisha wanamichezo namna ya kuweza kujiunga na mfuko huo
 Naibu Mkuu wa Takukuru Mkoani Tanga,Sadick Nombo kushoto akibalishana mawazo na Afisa Utumishi Mkoa wa Tanga,Jakobo Kingazi wakati wa bonanza hilo

 Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga(Ras) Mhandisi Zena Saidi akisalimiana na moja kati ya timu zilizokuwa zinashiriki bonanza hilo ambapo alisema michezo ina imarisha mahusiano mazuri kazini na ni muhimu kuimarisha miili yao na kuongeza ufanisi
Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga(Ras) Mhandisi Zena Saidi katika akiwa kwenye picha ya pamoja .Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha 

No comments: