Friday, September 16, 2016

KAMPUNI YA SHANTA GOLD MINING YALIPA FIDIA AWAMU YA KWANZA KWA WANUFAIKA SASA KUANZA MRADI WA UCHIMBAJI MADINI YA DHAHABU

Meneja wa Kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Shanta Gold Mine Ltd mkoani Singida Philbert Rweyemamu akitoa maelekezo ya awali kabla ya kuanza kwa zoezi la kuwalipa fidia wanufaika wote
Watendaji wa kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Shanta Gold Mine Ltd wakifanya maandalizi ya malipo hayo katika ukumbi wa mikutano Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ikungi
 Baadhi ya wananchi wakisubiri maandalizi yakamilike ili wakabidhiwe mlungula wao

Dear Mama Exp ndio ndinga iliyotumika kuwafikisha wananchi hao eneo la tukio la kukabidhiwa cheki za malipo kwa wanufaika wote wa Mradi huo
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akizungumza na Mwandishi wa habari wa kituo cha ITV Elisante Mkumbo kuhusu mchakato wa malipo utakavyo wanufaisha wananchi kupoitia mradi wa uchimbaji madini ya Dhahabu
Bi Juliana Kidamwe mkazi wa Kijiji cha Mlumbi akihakiki malipo yake kabla ya kukabidhiwa mbele ya Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Male Samson
Kushoto ni mwasibu wa Shanta Gold Mining Ltd Caroline na Mwanasheria wa kampuni ya Shanta Gold Mining David Rwechungura wakikagua fomu zote za wanufaika kabla ya kuanza zoezi la kuwapatia cheki wanufaika wote wa Mradi huo
Meneja wa Kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Shanta Gold Mine Ltd mkoani Singida Philbert Rweyemamu akitoa maelekezo kwa wanufaika wote ya namna mchakato mzima utakavyokwenda
Kizito Ramadhani mkazi wa Kijiji cha Mlumbi akikagua fomu za malipo yake mbele ya Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Male Samson kabla ya malipo
Kutoka kushoto ni Andrea Mtarim Mwenyekiti wa kijiji cha Kinyamberu, Ramadhani Mkuki Mwenyekiti wa Kijiji cha Mlumbi, Selemani Hema Mtendaji wa Kijiji cha Mlumbi,na Jumanne Gwaye Mtendaji wa Kata ya Mang'onyi wakifatilia kwa makini zoezi la ulipaji fidia
Kushoto ni Meneja wa Kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Shanta Gold Mine Ltd mkoani Singida Philbert Rweyemam na Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Male Samson wakisisitiza jambo wakati wakizungumza na wanufaika.
 Wananchi wakisikiliza kwa makini maelezo ya malipo yao
Meneja wa Kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Shanta Gold Mine Ltd mkoani Singida Philbert Rweyemamua akikusanya vitambulisho kwa wananchi waliofika ili kurahisisha zoezi la malipo yao
Wanufaika wakipongezana mara baada ya kukamata cheki zao kwa ajili ya malipo ya fidia

Na Mathias Canal, Singida
Katika miezi miwili ijayo kampuni ya Uchimbaji wa Madini ya dhahabu (Shanta Gold Mining  Limited) iliyopo katika kijiji cha Sambaru Kata ya Mang’onyi Wilayani Ikungi, Mkoani Singida huenda ikaanza uchimbaji wa madini ya dhahabu baada ya kuanza kulipa fidia ya zaidi ya Milioni mia nane (800,000,000) wanufaika awamu ya kwanza.

Malipo hayo yamekabidhiwa kwa wahusika ikiwa ni siku tatu tu zimepita tangu Meneja wa Mradi huo Philbert Rweyemamu alipotoa ahadi ya kuwalipa mwishoni mwa wiki hii ili kupisha shughuli za uchimbaji kuanza.
Wanufaika waliolipwa fedha hizo ni wale ambao wanatokanana na mazoezi mawili ya uthamini yaliyofanywa kwenye eneo la mradi kwa ajili ya upanuzi wa kambi.
Hafla ya malipo hayo imefanyika kwenye ukumbi wa mikutano kwenye Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu ambapo wananchi 39 wamejipatia kitita chao huku wengine wakishindwa kufika hivyo watakabidhiwa malipo yao wakati watakapoyahitaji.
Malipo hayo yanakamilisha umiliki wa maeneo hayo kwa Kampuni ya Shanta Gold mining kwa ajili ya uchimbaji na kuwafanya wananchi hao kupisha mradi wa uchimbaji dhahabu pasina kinyongo chochote.
Akizungumzia mchakato huo wa malipo hayo Meneja wa Kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Shanta Gold Mine Ltd mkoani Singida Philbert Rweyemamu amesema kuwa umefika wakati wa wananchi wa Wilaya ya Ikungi na taifa kwa ujumla kunufaika na mradi huo utakaoongeza Wigo ya ajira na mzunguko mkubwa wa pesa utakaotokana na wingi wa watu watakaodhuru Mkoani Singida kwa ajili ya shughuli za kazi.
Rweyemamu alisema kuwa Mradi huo utakuwa na mahusiano chanya kwa wananchi kwani pamoja na kuchelewa kuanza kwa uchimbaji lakini imeshiriki ujenzi wa Kituo cha Polisi Mang’onyi ulioanza mwezi May 2013 na kukamilika mwanzoni mwa mwaka 2014 na hatimaye kuzinduliwa na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Parseko V. Kone.
Akielezea ujenzi wa Kituo hicho Rweyemamu alisema kuwa Kituo hicho kimegharimu kiasi cha shilingi milioni mia mbili ishirini na tisa, laki tisa sabini na sita elfu na mia mbili thelathini (229,976,230) huku lengola ujenzi huo likiwa ni kwa ajili ya kusogeza huduma ya usalama karibu na wananchi.
Naye Mwanasheria wa Mradi huo wa uchimbaji Madini ya Dhahabu mkoani Singida David Rwechungura amesema kuwa Hadi sasa Shanta imewekeza takribani dola za Marekani milioni ishirini na tano hapa Singida yaani bilioni hamsini za fedha za Tanzania na bado gharama za kujenga mgodi ambazo hazitapungua dola milioni mia moja.
Alisema Mgodi wa Shanta huko Chunya Mkoani Mbeya unazalisha takribani kilo 2700 za dhahabu kwa mwaka ambapo pia umetoa ajira kwa wafanyakazi 800, licha ya wale ambao wanafaidika kwa kuuza vyakula mgodini na kadhalika.
Pamoja na kushiriki ujenzi wa Kituo cha Polisi Mang’onyi, lakini pia Kampuni ya Shanta imeanzisha Mradi wa maji  kijiji cha Mangonyi (Kisima kimoja kirefu kina meta 60, miundombinu ya kusambaza maji yenye urefu wa kilomita 1.3, injini na pampu ya kusukuma maji kwenda kwenye tenki la kijiji na polisi, imechangia Madawati 100, sawia na Samani (yaani vifaa vya ofisi) ya Kijiji hicho.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu ameipongeza Kampuni ya Shanta kwa kutekeleza ahadi yao kwa wakati kwa kuanza kuwalipa wananchi hao fedha zao za fidia kwa wamiliki wa mashamba zaidi ya 130 ambapo zaidi ya watu 85 ndio watakaonufaika  na kuifanya leseni ya kampuni hiyo itaanza kufanya kazi.
Dc Mtaturu amesisitiza agizo lake alilolitoa la kuitaka Kampuni hiyo kuwalipa fidia wananchi 69 wakati wa kikao cha pamoja kilichohudhuriwa na Wawakilishi wa kampuni ya Shanta Gold Mine Ltd, Wananchi wawakilishi kutoka Kijiji Cha Mlumbi na Uongozi wa kikosi kazi ambacho kilipewa jukumu la kuhakikisha wananchi wote ambao watapitiwa na mradi huo wanalipwa fidia sambamba na kusimamia uhamishaji wa makazi.

No comments: