Saturday, December 13, 2014

WENYEVITI WA TAIFA WA VYAMA VYA NCCR -MAGEUZI ,JAMES MBATIA NA TLP,AGUSTINE MREMA WAWANADI WAGOMBEA WAO JIMBONI VUNJO.

Mwenyekiti wa chama cha NCCR-Mageuzi akiendelea na mikutano ya kampeni katika kijiji cha Kisangesangeni kata ya Kahe akiwanadi wagombea wa nafasi za Uenyekiti.
Msafara wa Pikipiki ukiongoza kuelekea kijiji cha Ngaseni kwa ajili ya mikutano ya kampeni ya chama cha NCCR-Mageuzi.
Mgombea wa nafasi ya uenyekiti katika kijiji cha Ngaseni B,Amfrosia Komba akizungumza wakati akiomba kura kwa wananchi wa kijiji hicho.
Mwenyekiti wa chama cha NCCR-Mageuzi taifa ,James Mbatia akimnadi mgombea uenyekiti wa kijiji cha Ngaseni B,Amfrosia Komba ambaye alijitambulisha kuwa binti wa mbunge wa jimbo la Mbinga Magharibi ,Kepteni John Komba.
Wanakijiji wa Ngaseni B,wakifuatilia mkutano.
Wagombea wa nafasi ya Ujumbe wa Halmashauri ya kijiji cha Ngaseni wakitoa salamu za chama cha NCCR-Mageuzi katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika kijiji hicho.
Wanakijiji wa kijiji cha Ngaseni B,wakiitikia salamu ya chama cha NCCR-Mageuzi.
Mwenyekiti wa chama cha NCCR-Mageuzi ,James Mbatia akigawa vitabu kwa wakazi wa kijiji cha Ngaseni.
Mwenyekiti wa chama cha NCCR-Mageuzi ,James Mbatia akiwasili katika kijiji cha Kahe ,jimbo  la Vunjo kwa ajili ya mkutano wa kampeni wa kuwanadi wagombea wa nafasi za uenyekiti.
Mwenyekiti wa chama cha NCCR-Mageuzi ,James Mbatia akiwatuza vijana waliojitokeza kutoa burudani katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika kijiji cha Kahe.
Wananchi katika kijiji cha Kahe wakifuatilia mkutano wa kampeni wa kuwanadi wagombea wa nafasi za uenyekiti katika kijiji cha Kahe. 
Mwenyekiti Mbatia akiwahutubia wanakijiji wa Kijiji cha Kahe katika mkutano wa kampeni wa kuwanadi wagombea katika vijiji mbalimbali katika jimbo la Vunjo.
Mwenyekiti Mbatia akiwahutubia wanachi katika kijiji cha Orio jimboni Vunjo..
Mwenyekiti Mbatia akiwahutubia wananchi katika kijiji cha Uchira jimboni Vunjo.
Wakati Mbatia akiendelea na mikutano katika mikutano yake ,Mwenyekiti wa chama cha Tanzania Labour Party (TLP) Agustine Mrema naye amefanya mikutano yake katika vijiji mbalimbali ikiwemo kijiji cha Mamba Kotela kama anavyoonekana katika picha.
Na Dixon Busagaga wa Globu 
ya Jamii kanda ya kaskazini.

No comments: