Tuesday, July 22, 2014

AZANIA BANK LTD TAWI LA MOSHI YAFUTURISHA WATEJA WAKE KATIKA VIWANJA VYA GOFU, MOSHI

Baaadhi ya waumini wa dini ya kiislamu na wasio waislamu wakipata futari iliyoandaliwa na Benki ya Azania tawi la Moshi.
Mkuu wa wilaya ya Moshi ,Ibrahim Msengi (katikati)akiwa na sheakh mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ,Alhaj Shaban Rashid(kulia)
Waalikwa wakiendelea kupata futari.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira mjini Moshi ,Mhandisi Cyprian Luhemeja (wa nne toka kulia)pia alikuwa mmoja wa waalikwa katika hafla hiyo .
Mjumbe wa Bunge la Katiba na mkurugenzi wa shirika la KWIECO ,Elizabeth Minde (katikati)pia alikuwa miongoni mwa waalikwa katika hafla hiyo.
Baadhi ya waalikwa wakipata futari iliyoandaliwa na benki ya Azania Tawi la Moshi.
Meneja wa Azania Bank tawi la Moshi Bi. Hajira Mmambe(shoto)akiteta jambo na mfanyabiasha ,Ibrahimu Shayo maarufu kama Ibra line(mwenye kanzu) ,katikati ni mfanyakazi wa taasisi moja ya fedha mjini Moshi.
Afisa Biashara Mwandamizi wa Azania Bank makao makuu ,Othman Jibrea akizungumza mbele ya wageni waalikwa mbalimbali waliofika kupata futari ya pamoja iliyoandaliwa na Azania Bank tawi la Moshi.
Shekhe Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Alhaj Shaban Rashid akizungumza wakati wa futari ya pamoja iliyoandaliwa na Benki ya Azania,tawi la Moshi katika viwanja vya Gofu vya Moshi Club.
Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

No comments: