Tuesday, May 31, 2016

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA WAFANYAKAZI WA WIZARA YAKE

Katibu wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Cyprian Kuyava, akitoa neno la shukrani mjini Morogoro, baada ya kuchaguliwa kushika nafasi hiyo kwa kipindi kingine cha miaka mitatu ijayo.
Mkurugenzi wa Idara ya Uhakiki Mali za Serikali, Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Ezra Msanya, akijibu maswali ya baadhi ya wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo, mjini Morogoro, mwishoni mwa juma.
Baadhi ya wajumbe wa Baraza la wafanyakazi wa Wizara ya Fedha na Mipango, wakifuatilia kwa makini mada mbalimbali zilizotolewa wakati wa Mkutano Mkuu wa Baraza la wafanyakazi wa wilaya hiyo uliofanyika mjini Morogoro, mwishoni mwa juma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, (wa nne kutoka kushoto) akiungana na wafanyakazi wanaounda Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo kuimba wimbo wa mshikamano daima, wakati wa Mkutano Mkuu wa Baraza hilo uliofanyika Mjini Morogoro Mwishoni mwa juma. kushoto kwake ni Naibu Katibu Mkuu Dorothy Mwanyika na kulia kwake ni Naibu Katibu Mkuu Amina Hamis Shaban.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Fedha na Mipango, wakiimba wimbo wa mshikamano daima, mkutano uliopitia bajeti ya Wizara hiyo na kufanya uchaguzi wa viongozi wapya mjini Morogoro, mwishoni mwa juma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, akihutubia wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo (hawako pichani) mjini Morogoro, ambapo amewataka wafanyakazi wa wizara hiyo kufanyakazi kwa bidii na kuacha mazoea ili kutimiza malengo ya kukusanya mapato na kusimamia matumizi yake kikamilifu.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (aliyeketi katikati), akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Baraza la wafanyakazi wa Wizara hiyo uliofanyika mjini Morogoro, mwishoni mwa juma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (aliyeketi katikati), akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Baraza la wafanyakazi wa Wizara hiyo uliofanyika mjini Morogoro, mwishoni mwa juma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (aliyeketi katikati), akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Baraza la wafanyakazi wa Wizara hiyo uliofanyika mjini Morogoro, mwishoni mwa juma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (aliyeketi katikati), akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Baraza la wafanyakazi wa Wizara hiyo uliofanyika mjini Morogoro, mwishoni mwa juma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (aliyeketi katikati), akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Baraza la wafanyakazi wa Wizara hiyo uliofanyika mjini Morogoro, mwishoni mwa juma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, akiagana na katibu Tawala wa mkoa wa Morogoro, Mhandisi Dkt. John Ndunguru, baada ya kuzinduliwa rasmi kwa Baraza jipya la Wafanyakazi wa Wizara hiyo mjini Morogoro Mwishoni mwa juma.

KATIBU MKUU WIZARA YA AFYA AZINDUA BARAZA LA WAFANYAKAZI MUHIMBILI

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Maendeleo Jinsia, Watoto na Wazee, Dk Mpoki Ulisubisya akizungumza na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) LEO. Kutoka kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Profesa Mohamedi Janabi, Katibu wa baraza hilo, Dk Kissa Mwambene. Kushoto ni Mwenyekiti wa baraza hilo na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Museru na Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa MNH, Makwaia Makani.PICHA NA JOHN STEPHEN, HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI (MNH)
Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) wakipiga makofi wakati Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Maendeleo Jinsia, Watoto na Wazee, Dk Mpoki Ulisubisya wakizungumza na wajumbe wa baraza hilo Leo kwenye hospitali hiyo.Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Museru akizungumza na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi LEO kabla ya kupiga kura za kuwachagua viongozi wapya wa baraza hilo. Kushoto ni Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa MNH, Makwaia Makani wa hospitali hiyo.
Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la MNH wakimsikiliza Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali hiyo, Profesa Lawrence Museru katika kikao hicho.
Wajumbe wakipiga kura LEO za kuwachagua viongozi wapya wa Baraza la Wafanyakazi la Hospitali hiyo.
Dk Kissa Mwambene akiwashukuru wajumbe baada ya kumchagua Leo kuwa Katibu wa baraza hilo.
Wakili Eneza Msuya akiwashukuru LEO wajumbe baada ya kumchagua kuwa Katibu Msaidizi wa baraza hilo.
Kutoka kushoto ni Katibu wa Baraza la Wafanyakazi wa hospitali hiyo, Dk Kissa Mwambene, Mwenyekiti wa baraza hilo, Profesa Lawrence Museru, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Maendeleo, Jinsia, Watoto na Wazee, Dk Mpoki Ulisubisya, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Profesa Mohamedi Janabi, Katibu Msaidizi wa baraza hilo, Wakili Eneza Msuya na Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa MNH, Makwaia Makani.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Mpoki Ulisubisya ameipongeza Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa kuboresha maslahi ya watumishi wake na kuendelea kuweka miundombinu bora ya kiutendaji.Akizindua Baraza la Wafanyakazi la Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Dk. Ulisubisya amesema hatua hiyo ni ya kupongezwa kwani inampa motisha mtumishi kufanya kazi kwa bidii.

“Nimefarijika sana kuoana suala la maslahi ya watumishi linapewa kipaumbele hapa MNH kwa kweli mnastahili pongezi na taasisi nyingine hazina budi kuiga mfano huu, lakini napenda kusisitiza kuwa kila mtumishi ni vema akanufaika na maboresho haya amesema,” Dk Ulisubisya.
 
Akizungumza kabla ya uzinduzi wa baraza hilo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Profesa Lawrence Museru amesema hivi sasa hospitali hiyo imeongeza mapato yake kutoka Shilingi Bilioni 2 hadi kufikia Bilioni 4.
 
Pia amesema katika kuendelea kuboresha huduma za matibabu MNH ina mpango wa kuongeza ICU ya watoto wadogo pamoja na ICU ya kina mama wenye matatizo ya uzazi ili kuokoa maisha ya mama na mtoto .Kwa mujibu wa Profesa Museru Hospitali hiyo ipo katika hatua za mwisho za kupata mkopo kutoka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) mkopo ambao utasaidia kupanua huduma za afya ikiwamo kununua vifaa tiba vya upasuaji.

Katika kikao, wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wamemchagua Dk. Kissa Mwambene kuwa Katibu wa Baraza hilo pamoja na Eneza Msuya kuwa Katibu Msaidizi.

Barclays Bank Tanzania conducts a career fair event at University of Dar es Salaam Business School.

Barclays Bank Tanzania Head of Human Resources, Mrs Eutropia Isaack Vegula, talking to some University of Dar es Salaam students during the banks career fair event at the UDSM Business School hall  in Dar es Salaam at the weekend.
 Barclays Bank Tanzania Ag. Head of Marketing and Corporate Relations, Joe Bendera (left) talking to some University of Dar es Salaam students during the banks career fair event at the UDSM Business School hall in Dar es Salaam at the weekend.
 Barclays Bank Tanzania Legal Counsel, Dotto Khabi (left), giving some tips on legal issues to some University of Dar es Salaam students during the banks career fair event at the UDSM Business School hall in Dar es Salaam.
 Barclays Bank Tanzania Company Secretary, Farija Ghikas  (right) talking to some University of Dar es Salaam students during the career fair.
 A cross section of University of Dar es Salaam students during the Barclays Bank career fair event in Dar es Salaam at the weekend.

 Some University of Dar es Salaam students together with Barclays bank officials posing for a group photograph, during the bank career fair event in Dar es Salaam.

WAZIRI MKUU, MAJALIWA AFUNGUA MKUTANO WA 'AFRICA WORLD HERITAGE' JIJINI ARUSHA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea Vitambu kutoka Rais wa Bermuda Emmissions Control Limited, Bw. Donal Smith katika mkutano wa 'Africa World Heritage' aliounfungua kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) Mei 31, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe wakati alipomkaribisha kufungua Mkutano wa "Afrca World Heritage' kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) Mei 31, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifungua mkutano wa 'Africa World Heritage' kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) Mei 31, 2016. Kulia ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumaane Maghembe.
Baadhi ya Washiriki wa Mkutano wa wa' Africa World Heritage ' wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipofungua mkutano wao kwenye kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) Mei 31, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa Mkutano wa 'Africa World Heritage' baada ya kuufungua kwenye kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) Mei 31, 2016. Kulia kwake ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe na kushoto ni Mkuu wa Arusha, Felix Tibenda.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwapungia wasanii waliojitokeza kumlaki wakati alipowasili kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC) kufungua mkutano wa 'Africa World Heritage' mjini Arusha Mei 31, 2016. Kulia ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka wataalamu wa mambo ya malikale na uhifadhi wa urithi asilia (natural heritage) watafute mbinu zitakazoimarisha utunzaji wa rasilmali hizo bila kuathiri mifumo ya uchumi ya nchi zinazoendelea.

Ametoa wito huo leo (Jumanne, Mei 31, 2016), wakati akifungua Mkutano wa Kimataifa wa siku nne unaojadili Uhifadhi wa Urithi wa Dunia wa Afrika kama Nyenzo ya kuleta Maendeleo Endelevu ulioanza leo kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Arusha (AICC) jijini Arusha.

Waziri Mkuu amesema kuna baadhi ya nchi ambazo ni maskini sana lakini zimebarikiwa kuwa na rasilmali kama madini na gesi asilia lakini kwa sababu rasilmali hizo ziko karibu sana na vivutio vya urithi asilia wa dunia, watu wa nchi hizo wanazuiwa kuchuma rasilmali zao ili wasiharibu vivutio hivyo.

“Tunatambua umuhimu wa kutunza rasilmali na vivutio vya urithi asilia. Hivi ni kwa nini zisitafutwe teknolojia zinazofaa ambazo zitaruhusu uvunaji wa gesi asilia na madini bila kuathiri uhifadhi wa vivutio vya urithi asilia wa dunia (world heritage sites)?”, alihoji Waziri Mkuu.

“Serikali za nchi za Kiafrika zinahitaji suluhisho kama hili wakati zikiendelea kutafuta njia sahihi za kuwianisha uhifadhi wa vivutio vya urithi wa dunia na changamoto ya kuondoa umaskini miongoni mwa wananchi wake,” amesema.

“Sisi viongozi ambao wengi wetu ni wanasiasa, hatukatai ushauri wa wataalamu lakini tunawasihi baadhi yenu ambao mnashiriki mkutano huu muhimu, mtafute njia mbadala za kufumbua tatizo hili badala ya kuendelea kutegemea njia za kizamani za kukabiliana na changamoto kama hizi ili sote tuweze kunufaika na rasilmali zilizopo ikiwa ni pamoja na kutunza vivutio vya urithi asilia wa dunia,” aliongeza.

Amesema kama rasilmali hizo zitachambuliwa vizuri na kwa njia sahihi bila kuathiri vivutio vya urithi wa dunia, ni dhahiri kuwa zitaingiza mapato ambayo kiuchumi yatasaidia kuondoa umaskini miongoni mwa wananchi ambao pia watasaidia kwenye uhifadhi wa vivutio hivyo.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufungua mkutano huo, Waziri Mkuu alisema Tanzania imebarikiwa kuwa na rasilmali nyingi zikiwemo za ardhini (madini), misitu, wanyama na maeneo ya kihistoria na kusisitiza kuwa Watanzania wana jukumu la kuzilinda ili zilete tija kwa wananchi wote.

“Tukizitunza rasilmali zetu zitasaidia kupata mapato kutokana na utalii Serikali itapeleka sehemu ya mapato haya katika miradi mbalimbali na hivyo kuchangia kwenye pato la Taifa,” amesema.

Kwa upande wake, Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe amesema Tanzania itaendelea kushirikiana na UNESCO hasa katika masuala yanayohusu uhifadhi wa vivutio vya dunia kutokana na umuhimu wake kwenye maendeleo endelevu.

Alisema wizara yake imelenga kusimamia, kuendeleza na kuimarisha utunzaji wa maliasili na uhifadhi wa vivutio asilia na vya kiutamaduni (natural and cultural heritage) kwa kushirikiana na wadau wengine hapa nchini.

Naye Mkurugenzi wa Uhifadhi Malikale wa UNESCO, Dk. Mechtild Rossler aliwataka washiriki wa mkutano huo kutoka nchi mbalimbali duniani wawe tayari kupitia upya shughuli zinazotekelezwa katika eneo la urithi wa dunia na kuangalia wajibu wa nchi za Kiafrika katika kuandaa mwelekeo wa miaka ijayo.

Alisema katika miaka 40 ya utendaji wa UNESCO, idadi ya vivutio vya urithi wa dunia imeongezeka na kufikia 89 ambapo kati ya hivyo viko baadhi vinakavyobiliwa na changamoto ya kufutika kutokana na athari za kigaidi, matukio ya kivita na kazi za kibinadamu.

“Vivutio 16 kati ya 48 viko katika nchi za Afrika zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara na hivi vinakabiliwa na tishio la kupotea kutokana na vita, harakati za kigaidi na shughuli za kiuchumi za kibinadamu zikiwemo uchimbaji wa madini na gesi asilia,” alisema.

Aliwataka washiriki wa mkutano huo wakumbuke kuwa vivutio vya urithi wa dunia ni vielelezo vya jamii na pia huchangia uchumi kwa kutoa ajira kwenye jamii husika.

Mkutano huo unaohudhuriwa na washiriki zaidi ya 150 kutoka nchi mbalimbali duniani, unajumuisha washiriki kutoka nchi 36 zikiwemo nchi 12 ambazo ni za nje ya bara la Afrika.


Waziri Mkuu amerejea mjini Dodoma mchana huu kuendelea na vikao vya Bunge.

LUHWAVI AKAGUA JENGO LA MIKUTANO LA CCM DODOMA LEO

Kaimu Meneja Miliki wa Jengo la Mikutano la CCM la Dodoma Convetion Centre, Christopher Ngalison akimuonyesha Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi hali ya maua kwenye bustani za jengo hilo, alipokagua leo Mei 31, 2016, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCm, unaotarajiwa kufanyika Juni au Julai Mwaka huu.
Kaimu Meneja Miliki wa Jengo la Mikutano la CCM la Dodoma Convetion Centre, Christopher Ngalison akimuonyesha Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi hali ya maua kwenye bustani za jengo hilo, alipokagua leo Mei 31, 2016, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCm, unaotarajiwa kufanyika Juni au Julai Mwaka huu. 
Luhwavi akielekeza namna ya kuboreshwa bustani zinazozunguka jengo la ukumbi huo 
Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi akizunguka jengo la Mikutano la CCM la Dodoma Convetion Cetre, alipokagua leo Mei 31, 2016, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCm, unaotarajiwa kufanyika Juni au Julai Mwaka huu
Luhwavi akiingia ndai ya ukumbi wa jengo hilo kuona hali halisi 
Kaimu Meneja Miliki wa Jengo la Mikutano la CCM la Dodoma Convetion Centre, Christopher Ngalison (kushoto), akimpa maelezo kuhusu hali ya ndani ya jengo hilo, Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi alipolikagua leo Mei 31, 2016, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCm, unaotarajiwa kufanyika Juni au Julai Mwaka huu. 
Kaimu Meneja Miliki wa Jengo la Mikutano la CCM la Dodoma Convetion Centre, Christopher Ngalison (kushoto), akionyesha baadhi ya viti ambayo hutumiwa na wajumbe, katika ukumbi huo, Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi (hayupo katika picha), alipolikagua leo Mei 31, 2016, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCm, unaotarajiwa kufanyika Juni au Julai Mwaka huu. Mkuu wa Idara ya Usalama na Maadili Makao Makuu ya CCM, Masudi Mbengula 
Bendera ya Taifa na bendera ya CCM zikipepea kwenye jengo hilo la Mikutano la CCM, kama ilivyo kawaida.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Rajab Luhwavi (wapili kushoto) akikagua jengo la Mikutano la CCM, Dodoma Convetion Centre leo ikiwa ni maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCM unaotarajiwa kufanyika Juni au Julai mwaka huu katika ukumbi huo. Kushoto ni Ofisa Miliki wa Jengo hilo Tegemeo Saambili 

Luhwavi akitazama hali ya maua kwenye bustani za jengo la ukumbi huo 
Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara Rajab Luhwavi akipata maelezo kutoka kwa Ofisa Miliki wa Jengo la Mikutano la CCM la Dodoma Convetion Centre, Tegemeo Saambili (kushoto), alipokagua jengo hilo leo Mei 31, 2016, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCm, unaotarajiwa kufanyika Juni au Julai Mwaka huu. 
Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Rajab Luhwavi akihoji kuhusu hali ya bustani zinazozunguka jengo hilo 

Kaimu Meneja Miliki wa Jengo la Mikutano la CCM la Dodoma Convetion Centre, Christopher Ngalison akimuonyesha Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi hali ya maua kwenye bustani za jengo hilo, alipokagua leo Mei 31, 2016, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCm, unaotarajiwa kufanyika Juni au Julai Mwaka huu. 
 PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO http://michuzi-matukio.blogspot.com/