Friday, May 24, 2013

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA
TANZANIA, MHESHIMIWA DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE, AKIFUNGUA WARSHA YA WAZI (OPEN DAY) KUHUSU MFUMO MPYA WA UFUATILIAJI NA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA KITAIFA YA KIPAUMBELE, VIWANJA VYA MAKUMBUSHO YA TAIFA, DAR ES SALAAM, MEI 24, 2013

Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mhe. Dkt. Ali Mohammed Shein, Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar;
Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda (Mb), Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mhe. Seif Shariff Hamad, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar;
Waheshimiwa Mawaziri na Manaibu Waziri;
Balozi Ombeni Sefue, Katibu Mkuu Kiongozi;
Makatibu Wakuu;
Dkt. Philip Mpango, Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango;
Washirika na Wadau wa Maendeleo;
Viongozi wa Taasisi za Serikali na Mashirika ya Umma;
Viongozi wa Kidini na Sekta Binafsi;
Wataalamu Elekezi kutoka PEMANDU na Mckinsey;
Washiriki wa Maabara;
Ndugu Wananchi;
Mabibi na Mabwana:
Napenda kuchukua fursa hii kuwakaribisha wote katika Warsha ya Wazi kuhusu mfumo mpya unaoanzishwa na Serikali wa ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa miradi ya kitaifa ya kipaumbele.  Warsha hii inatoa nafasi ya pekee kwa wananchi kushiriki na kutoa mawazo yao jinsi ya kuboresha mfumo huo unaopendekezwa.  Ni Warsha ya kuelimishana, kubadilishana mawazo na kufahamishana mipango na mambo ambayo Serikali inatarajia kuyafanya katika siku za karibuni. 
Namshukuru Balozi Ombeni Sefue, Katibu Mkuu Kiongozi, Dkt. Philip Mpango, Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, viongozi na watumishi wote wa Tume ya Mipango kwa kuandaa Warsha hii mahsusi.  Kwa namna ya pekee nawashukuru pia wataalamu wa PEMANDU na McKinsey kwa kushirikiana vizuri na wataalam wetu katika kila hatua ya safari hii ambayo Serikali yetu imeianza.
Ndugu Wananchi;
Kupanga na kutekeleza mipango ya maendeleo sio jambo geni hapa nchini.  Ni jambo ambalo tumelifanya tangu tupate Uhuru na tunaendelea nalo.  Serikali ya Awamu ya Kwanza chini ya Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Nyerere, ilianza na Mpango wa Kwanza wa Maendeleo mwaka 1961 – 1964.  Mpango huo uliainisha maadui watatu wa maendeleo ambao ni umaskini, ujinga na maradhi.  Mikakati mbalimbali na mipango madhubuti ya maendeleo ilibuniwa ili kupambana na maadui hao.  Baada ya hapo ukaja Mpango wa Maendeleo wa Miaka 15 wa mwaka 1964 – 1980, uliokuwa umegawanywa katika vipindi vitatu vya utekelezaji vya miaka mitano mitano.
Baadhi yenu mtakumbuka kuwa utekelezaji wa vipindi viwili vya mwanzo ulikuwa wa kuridhisha.  Hata hivyo, utekelezaji wa kipindi cha mwisho cha Mpango ule, yaani kati ya mwaka 1975 – 1980, ulikuwa duni mno.  Utekelezaji wake ulivurugwa sana na changamoto za wakati ule kama vile kupanda sana bei ya mafuta, kuvunjika kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki (1977) na Vita ya Kagera.  Mambo haya yalisababisha fedha zetu nyingi kutumika kuagiza mafuta, kujenga taasisi zetu wenyewe na kutetea mipaka ya nchi yetu.  Rasilimali kidogo tuliyonayo ikaenda huko badala ya kugharamia miradi ya maendeleo.   
Ndugu Wananchi;
Pamoja na changamoto zilizojitokeza, Serikali iliamua kuanzisha mpango mwingine wa maendeleo wa muda mrefu wa mwaka 1981 – 2000.  Kwa bahati mbaya mpango huo nao haukutekelezwa kufuatia kuendelea kudorora kwa uchumi.  Kati ya mwaka 1981 na miaka ya 90 mwanzoni, Serikali ilianza kufanya mabadiliko makubwa ya kiuchumi.  Tukawa na National Economic Survival Programme (NESP) mwaka 1981 – 82 na Structural Adjustment Programme (SAP) mwaka 1982 – 1985.  Mipango hiyo haikutekelezwa vizuri kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ya ukosefu wa rasilimali za kutosha.  Kati ya mwaka 1986 – 89, Serikali kwa kushirikiana na Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) ikaanza kutekeleza programu ya kwanza ya kufufua uchumi (ERP – I).  Ya pili ikafuatia kati ya mwaka 1989 – 1992.
Mwaka 1994 Serikali ikaanza kuandaa mpango wa maendeleo wa muda mrefu utaowezesha kuzikabili changamoto mpya kufuatia mageuzi ya kiuchumi na kijamii yaliyokuwa yanaendelea nchini na duniani kwa ujumla.  Kazi hiyo ilikamilika mwaka 1999 na kuzinduliwa kwa Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2025.  Malengo ya Dira hiyo ni kuleta maendeleo ya haraka nchini na kuifanya Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.  Maana yake ni kwamba wananchi wawe na chakula cha kutosha, huduma ya elimu na afya iliyo bora iwafikie watu wengi zaidi, vifo vya watoto na akina mama vipungue, wastani wa kuishi uongezeke, maji safi na salama yapatikane kwa wote, uhalifu upungue na umaskini uliokithiri usiwepo kabisa na pato la wastani la Watanzania liwe zaidi ya dola za Kimarekani 3,000.  Vile vile pawe na maendeleo ya viwanda, matumizi ya teknolojia na sayansi yaongezeke, miundombinu ipanuke na uchumi ukue kwa asilimia 8 au zaidi. 


Ndugu Wananchi;
Juhudi kubwa zilizofanywa na Serikali za awamu zote ikiwemo na hii ninayoiongoza mimi zimeleta mafanikio ya kutia moyo.  Kwa mfano, uchumi wa nchi umekua kwa wastani wa asilimia 7 kwa miaka kumi iliyopita, mfumuko wa bei upo chini ya asilimia 10, mapato ya ndani yameongezeka, mauzo ya nje yameongezeka na hifadhi ya fedha za kigeni imeongezeka pia.  Hata hivyo, idadi ya Watanzania walio maskini bado ni kubwa hususan umaskini wa kipato.  Vile vile bado hatujafanikiwa kufikia malengo katika maeneo mengi tuliyojiwekea.  Hata tathmini ya utekelezaji wa Dira ya Maendeleo 2025 tuliyofanya mwaka 2000 imethibitisha hivyo.  Hatuendi kwa kasi inayotakiwa na utekelezaji wake siyo wa kuridhisha.  Matokeo yake tupo nyuma ya hatua tuliyotakiwa kuwa.  Kwa mfano, kwa upande wa safari ya kuelekea pato la wastani la watu kuwa dola 3,000 mwaka 2025, tulitakuwa tuwe tumefikia dola 995 mwaka 2010.   Lakini ilikuwa tumefikia dola 545 tu.  Kwa ukuaji wa uchumi, tulitakiwa tuwe asilimia 8, lakini tulikuwaasilimia 7
Zipo changamoto nyingi za ndani na nje, zilizofanya tusifikie malengo hayo:  Kubwa ni misukosuko ya uchumi wa dunia, uhaba wa rasilimali fedha na ufuatiliaji mdogo katika utekelezaji wa miradi iliyoainishwa kuleta maendeleo. Aidha, mipango na mikakati ya maendeleo ilikuwa na vipaumbele vingi kwa wakati mmoja wakati rasilimali za utekelezaji wake ni kidogo.  Hali hii haikutuwezesha kujielekeza ipasavyo kwenye maeneo yenye kuleta matokeo makubwa na kwa haraka.
Ndugu Wananchi;
Baada ya kutafakari yote haya, tukafikiria namna ya kuweza kufikia malengo yetu ya Dira ndani ya muda uliobakia. Hivyo, tukaamua kuja na Mpango ya Maendeleo wa Muda Mrefu wa Miaka 15 ambao utatekelezwa katika awamu tatu za miaka mitano mitano. Katika Mpango wa Kwanza Maendeleo wa Miaka Mitano (2011/12-2015/16), maeneo yaliyopewa kipaumbele ni Miundombinu, Kilimo, Viwanda, Huduma za jamii na Uendelezaji Rasilimali Watu na Utalii, Biashara na Huduma za Fedha.  Changamoto kubwa ikabaki kuimarisha mfumo wetu wa kusimamia utekelezaji wa mipango ya maendeleo ili kuleta matokeo ya haraka.  Kuendelea kufanya vilevile tulivyokuwa tukifanya kusingeweza kuleta mabadiliko tuliyokuwa tunayataka katika utekelezaji wa mipango yetu.  Ilibidi tubadilike, ikiwezekana tukimbie pale ambapo wengine wanatembea. 
Ndugu Wananchi;
Tukiwa katika hali hiyo ya kutafakari cha kufanya, mwezi Mei, 2011 ikawa bahati mimi kuhudhuria Mkutano wa Kimataifa wa “Langkawi  International Dialogue” uliofanyika mjini Kuala Lumpur, Malaysia.  Katika mkutano huo, Serikali ya Malaysia iliwasilisha mada jinsi inavyoendesha na kusimamia utendaji wake ikiwemo utekelezaji wa miradi ya maendeleo na huduma kwa jamii.  Mimi na viongozi wenzangu tuliohudhuria mkutano huo tulivutiwa sana na mfumo wa utendaji wa Malaysia na tukadhamiria kujifunza zaidi kutoka kwao.  Tukaomba watusaidie.  Bahati nzuri Serikali ya Malaysia ikakubali ombi letu na kuandaa warsha maalum mwezi Novemba, 2011.  Ujumbe wa Tanzania kwenye warsha hiyo ya aina yake uliongozwa na Dkt. Philip Mpango.  Waliporudi, tukaamua kuwa na sisi tuanze kutumia utaratibu wa Malaysia wa “Matokeo Makubwa Sasa” ama kwa Kiingereza “Big Results Now”.
Ndugu Wananchi;
Utekelezaji wa mfumo wa “Big Results Now” hapa nchini ulianza kwa kuainisha maeneo sita yenye uwezo wa kutupatia matokeo makubwa kwa haraka. Maeneo hayo ni nishati, elimu, maji, miundombinu, kilimo na utafutaji fedha.  Kazi ya kuchagua maeneo sita ya kwanza nayo haikuwa rahisi.  Tulibishana sana katika kuchagua vipaumbele vichache lakini vyenye kuleta matokeo makubwa.  Hatimaye tukafanikiwa.  Vipaumbele hivi vinabeba msingi wa kufungulia fursa za ukuaji uchumi wa Tanzania kwa ujumla na kuchochea ustawi wa maisha bora kwa wananchi. 
Hatua ya pili ikawa ni kufanya uchambuzi wa kina kupitia awamu ya kwanza ya maabara (lab) kama alivyoeleza Katibu Mkuu Kiongozi. Kazi hiyo ilitekelezwa kwa wiki sita mfululizo na wataalam wetu zaidi ya 300 kutoka nyanja na sekta mbalimbali na kukamilika tarehe 05 Aprili, 2013. Nawapongeza sana kwa kazi hiyo kubwa na moyo wao wa kujitolea. Tumeandaa ratiba ya utekelezaji kwa kila mradi na programu ikionyesha kazi zilizopangwa kufanywa, mtekelezaji-husika na muda na kukamilisha kazi.  
Katika mfumo huu, Mawaziri na Watendaji katika Wizara na Idara watapimwa kwa vigezo vilivyo wazi na ninyi wananchi mtapata fursa ya kuvijua vigezo hivi pamoja na matokeo ya upimaji.  Hapatakuwa na siri. Hii itarahisisha usimamizi wa utendaji kwa maana Waziri au Katibu Mkuu atajifunga yeye mwenyewe kimaandishi na ataweka saini yake kwenye vigezo ambavyo atapimwa navyo na wananchi mtashuhudia matokeo ya upimaji huo.
Ndugu Wananchi;
Ili kuweza kuratibu vyema shughuli za ufuatiliaji wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika mfumo huu mpya, nimeunda chombo maalum kitakachokuwa chini ya Ofisi yangu ambacho kitajulikana kama President’s Delivery Bureau (PDB). Kazi zake za msingi zitakuwa ni pamoja na: kupanga na kuendesha shughuli za uchambuzi wa kina wa kimaabara (labs); kuandaa mikataba ya kupima utendaji kazi wa Mawaziri kwenye miradi na programu za maendeleo katika wizara zao; kwa kushirikiana na Tume ya Mipango kuishauri Serikali kuhusu maeneo machache ya kipaumbele yenye kuleta matokeo ya haraka (National Key Results Areas); kusaidia sekta binafsi kuwekeza kwenye maeneo hayo; na kufanya tathmini huru ya utendaji kwa viongozi wote hususan Mawaziri katika utekelezaji wa maeneo muhimu ya kitaifa.
Ndugu Wananchi;
Tumefanya kazi kubwa sana ya kuandaa na kuainisha maeneo ya kimkakati na kuyaandalia programu za kina kwa ajili ya utekelezaji. Lakini tumeona ni vyema kuwashirikisha wadau na wananchi katika jambo hili kubwa.  Ndio maana tupo hapa kuhakikisha kuwa wananchi kwa ujumla wenu mnapata fursa ya kuchangia katika miradi na programu hizo kwa maendeleo ya taifa letu na watu wake.
Ndugu Zangu;
Sitapenda kuongea sana hivyo basi nataka niwape nafasi wananchi na wadau wengine mliofika hapa kupita katika eneo la kila maabara na kupata maelezo ya kina kutoka kwa wataalam.  Muwe huru kuuliza maswali, kujenga hoja, kutoa maoni na kukosoa na kuboresha katika kila maabara. Baada ya kupata maoni yenu ndipo tutaboresha na kwenda kuyafanyia kazi maoni na ushauri wenu.  
Ndugu Wananchi;
Baada ya kusema hayo, napenda kutamka kuwa Warsha ya Wazi imefunguliwa rasmi.  Ninawatakia majadiliano mazuri na uchangiaji mzuri.
Asanteni kwa kunisikiliza

TUME YA KUREKEBISHA SHERIA YAMPONGEZA JAJI ALOYSIUS MUJULIZI BAADA YA KUAPISHWA NA RAIS JAKAYA KIKWETE KUWA MWENYEKITI WA TUME

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimuapisha Mh. Jaji Aloysius Mujulizi kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania.
Waziri wa mambo ya Nje Benard Membe (wa kwanza kulia) akiwa na Mabalozi wateule pamoja na Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Mh. Jaji Aloysius Mujulizi (wa pili kulia) wakati wakisubiri kuapishwa Ikulu jijini Dar es salaam.
Rais Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Makamu wa Rais Dkt. Mohamed Gharib Bilali pamoja na Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Jaji Mujulizi mara baada ya kuapishwa.
Rais Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Makamu wa Rais Dkt. Mohamed Gharib Bilali, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali George Masaju, Makamishna na watumishi wa Tume.
Watumishi wa Tume wakifurahi wakati wa kumpongeza Mwenyekiti wao Mh. Jaji Aloysius Mujulizi.
Bi. Halima Chawa akimzawadia shada la maua kwa niaba ya watumishi wa Tume Mwenyekiti wa Tume Mh. Jaji Aloysius Mujulizi alipowasili ofisi za Tume mara baada ya kuapishwa.
Kamishna wa Tume Ester Manyesha akizungumza wakati wa kumpongeza Mh. Jaji Mujulizi.
Jaji Mujulizi akiongea na watumishi wa Tume.

Jaji Mujulizi akipongezwa pamoja na familia yake na watumishi wa Tume
Mwenyekiti wa Tume Jaji Mujulizi akiwa katika picha ya pamoja na Makamishna na watumishi wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania.  (Picha zote na Munir Shemweta LRCT).

HAKUNA JAMII ITAKAYOACHWA NYUMA KIMAENDELEO-TANZANIA


Balozi Ramadhan Mwinyi Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, akizungumza wakati wa Mkutano wa Kudumu wa 12 wa Masuala ya Wazawa, katika mchango wake kuhusu mada ya utafiti uliofanywa kuhusu Ujasiri, Maarifa ya Jadi na Kujenga uwezo Jamii ya Wafugaji katika Afrika, Mwakilishi huyo ameeleza kwamba Jamhuri ya Muungano inajukumu la kuwaletea maendeleo wananchi wake wote na kwamba katika hakuna jamii itakayoachwa nyuma. Akasisitiza haja na umuhimu wa Jumuiya ya Kimataifa na wadau wengine kushirikiana na Serikali kufanikisha azma hiyo lakini pia kuunga mkono hatua na maamuzi inayoyachukua kwa manufaa ya wananchi wake na taifa kwa ujumla. Nyuma ya Balozi ni Bi. Ellen Maduhu Afisa wa Ubalozi .

Na Mwandishi Maalum

 Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesisitiza kwamba inajukumu kubwa  la kuhakikisha kuwa mipango yake ya maendeleo endelevu inamfikia kila mwananchi na kwamba hakuna jamii itakayo achwa nyuma.
Na kwa sababu hiyo, Tanzania imeitaka  Jumuiya ya Kimataifa na wadau wengine kushirikiana na Serikali katika kufanikisha azma  yake hiyo, lakini pia kutambua  kuwa maamuzi mbalimbali inayoyachukua  yanafanyika kwa nia njema.

Hayo yameelezwa na   Balozi  Ramadhan Mwinyi, Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa   Tanzania katika Umoja wa Mataifa,  alipokuwa akichangia  majadiliano ya mada   ya utafiti kuhusu Ujasiri, Maarifa ya Jadi na Kujenga Uwezo wa Jamii ya  Wafugaji katika Afrika.

Mada  hiyo ni sehemu ya mada kadhaa zikiwa zao afya, elimu, haki za binadamu, ujasiliamali, vijana mila na tamadu ambazo zimekuwa zikijadiliwa kwa nyakati tofauti katika Mkutano wa Kudumu wa 12  Kuhusu Masuala ya Wazawa. ( Forum on Indigenous Issues) Mkutano huu ambao ulianza mapema wiki hii unafanyika chini ya  usimamizi wa  Baraza la Uchumi na Maendeleo ya Jamii la Umoja wa Mataifa ( ECOSOC).

Washiriki wa  mkutano  huu wapatao 2000 wanatoka katika Asasi zisizo za kiserikali  wakiwamo wawakilishi kutoka   baadhi ya  taasisi za kifedha kama  Banki ya Dunia,  Banki ya Maendeleo ya Afrika  na  Banki  ya Maendeleo ya Asia.

“Tunaendelea na  jitihada za kuwaletea maendeleo wananchi wetu ili kuhakikisha kwamba hakuna jamii inayoachwa nyuma kama ambavyo imeainishwa katika Malengo ya Maendeleo ya Millenia ( MDGs) na  kutafsriwa katika Mpango wa Maendeleo ya Taifa na  mipango migineyo” akasisitiza Balozi Mwinyi.

Hata hivyo akasema licha ya jitihada hizo za serikali , bado kuna baadhi ya jamii chache ambazo zenyewe zimeamua    kudumisha  mila, tamaduni na   maisha yao ya jadi .

Akasema  jamii hizo ni zile ambazo hazifahamiki sana katika Jumuiya ya Kimataifa kama ilivyo kwa jamii ya  wamasaai.

Akizungumzia  masuala ya upatikanaji na ugawaji wa ardhi kwa wananchi  zikiwamo  jamii ambazo mfumo wa maisha yao unategemea zaidi ardhi na mali asili nyingine. Balozi   Mwinyi amewaeleza washiriki  wa  mkutano huo wakiwamo washiriki kutoka Tanzania, kwamba serikali imejiwekea sheria na taratibu zinazosimamia ugawaji wa ardhi.

Akafafanua  kwa kueleza kwamba kwa sheria na taratibu za Tanzania,   Hati ya umiliki wa Ardhi katika  ngazi ya kijiji hutolewa  kwa wanajamii ambao wanaishi au wamekusanyika katika  muundo wa kijiji ambao unatambuliwa rasmi.

“ Kwa mujibu wa sheria zetu, ni kijiji ndicho kinatambuliwa kisheria  kama chombo huru kinachosimamia masuala ya ardhi ambapo cheti  cha ardhi hutolewa kwaajili ya matumizi ya jamii nzima”. Akasema
Na kuongea “ Hata hivyo    kuna  baadhi ya maeneo  hasa yale ya wawindaji ambapo kama idadi ya  jamii ile haikukidhi  matakwa ya kisheria ya kuwa na hadhi ya kijiji kutokana na uchache wao, bado kwa mfano,  mwaka 2011, serikali ilitoa  hati ya  kumiliki ardhi kwa ya Wahdzabe ingawa walikosa sifa  zinazotakiwa kisheria.

Akizungumza kuhusu  Loliondo ambako  Serikali imetangaza kutenga eneo la kiasi cha kilomita za mraba 2,500  za ardhi kwaajili ya  makazi ya jamii ya wamasaai  na ambao wengi wao hawakuwa na ardhi na hivyo kuwa katika mazingira magumu. Balozi amesisitiza kwamba uamuzi huo ulikuwa ni wa manufaa kwa jamii hiyo na taifa kwa ujumla.

Akasema kuwa  eneo  lililotengwa   ni kubwa  kuliko nchi ya Luxeburg au  mara nne ya eneo la nchi ya Singapore ambayo ina kilomita za mraba 624.

Akasema eneo  lililobaki la kilomita za mraba 1,500 Serikali imelitenga kwaajili ya hifadhi ya wanyama pori na mazalia yake ikiwa ni  pamoja na uhifadhi wa uoto wa asili, utunzaji wa vyanzo vya maji  kwa maendeleo endelevu ya  uwepo wa wanyama na kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Naibu Mwakilishi wa Kudumu akafafanua Zaidi kwa kueleza kwamba, uamuzi huu wa Serikali wa kutenga ardhi kwaajili ya matumizi ya binadamu na mengine  kwa hifadhi ya  maliasili ni uamuzi halali na wala haukuanza sasa  bali umekuwa  ukitekelezwa katika  maeneo mengi ya nchi tangu uhuru.

Thursday, May 23, 2013

African Union 50th Anniversary

 On behalf of the Smart Partnership Movement, we would like to extend our best wishes to the African Union on this special day, which marks the fiftieth anniversary of its establishment. From its opening conference in Addis Ababa in 1963, the Organisation of African Unity sought to deepen co-operation and understanding amongst its members in order to improve the lives of Af­ricans across the continent. The African Union has carried on these aims, seeking to promote “an integrated, prosperous and peaceful Africa, driven by its own citizens and representing a dynamic force in the global arena”.

The longevity and continuing influence of the African Union are achievements that resonate strongly with the Smart Partnership Movement, which has always strived to support the Union, and Africa as a whole, in its aims. Since the “Smart Partnership for the Generation of Wealth in
Southern Africa” Dialogue in Kasane, Botswana in 1997, African nations have played increasingly prominent roles in this truly progressive movement. Namibia, Zimbabwe, Mozambique, Uganda, Swaziland, Lesotho and Zambia have all hosted Dialogues in the intervening years.

These Dialogues are unique opportunities for Smart Partners to share the benefits of their knowl­edge, experience and skills while leaving behind the constituencies and commitments which can stand in the way of uncluttered, impartial and imaginative thinking. His Excellency Dr Yoweri Ka­guta Museveni, President of the Republic of Uganda and current Chair of the Smart Partnership Movement, believes Smart Partnership is the only place he knows where people can think and talk independently.
The problem is we are always rushing all the time… CPTM is a caucus for informal think-tanking for new ideas.”

One such new idea is the African Peace Hub, developed at the Global Dialogue in Munyonyo, Uganda in 2009. The African Peace Hub is designed to be the fulcrum of a virtuous wheel of peaceful and sustainable development across the continent, supported by the body of experience developed and held within the centre. The African Peace Hub was officially inaugurated at the opening of the African Union Summit in Munyonyo in 2010.

In 2013, the “Year of Pan-Africanism and the African Renaissance”, we are delighted that Tanzania will join the list of Smart Partnership Dialogue host nations. In selecting the theme for the Dia­logue, “Leveraging Technology for African Socio-Economic Transformation”, His Excellency Ja­kaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania and CPTM Fellow, has chosen a topic at the very heart of the Smart Partnership Movement. Smart Partnership is about creating limitless opportunities and wealth that is shared, sustainable and resilient and that allows the par­ticipants to function in the global economy. Its successful functioning depends on a mutually bene­ficial and ‘prosper thy neighbour’ relationship among ‘Partners’, who believe that the application of technology can support sustainable development and greatly improve socio-economic conditions across the world.
As well as being the collection of devices, components and engineering practices in a given con­text, technology is also a means to fulfill a human purpose. Technology Inclusiveness refers to policy frameworks and approaches for using Innovation to foster ‘inclusive growth’, not only strong growth, but ‘resilient and smart growth’. This approach requires synchronisation, joined up think­ing and action with measures to support new entrants with riskier projects in advanced materials, nanotechnology, information and communication technologies, super computers, biotechnology and advanced manufacturing. Tapping into the vast array of technologies now available enables countries to develop new activities or modernize existing ones, and to increase the competitive­ness of agriculture, industry and services. Education and communication are vital if these new elements are to be accepted and practiced by citizens, leading to positive economic and societal developments. Technology also facilitates the production and deployment of renewable energies and “green” technologies, supporting energy and water efficiency or enabling more efficient health services.
The Smart Partnership Movement prides itself on facilitating the exchange of experience, bench­marking and dialogue, which is particularly relevant to the theme of its Global 2013 Dialogue. The engagement and interactions between members of the public, private and civil spheres within the Movement over the past three years have produced three specific inclusion initiatives that con­tribute to socio-economic transformation and will be key features of the Dialogue in June. Innova­tion is not only about the transfer and deployment of new technologies. Technology management should be integrated into the National Vision and objectives of the people it is designed to serve and a mixture of traditional and modern means is often the most fitting way of turning these visions
into reality. Such innovation plays a key role in Smart Partnership’s continuing support of National Visions in Botswana, Cameroon, Lesotho, Mauritius, Mozambique, Namibia, Seychelles, Swa­ziland and Uganda, among others. These innovative solutions must also abide by international standards, with customer care and awareness as well as quality management integral to sustained success. Adherence to such standards also enables a greater market access and consequently contributes to economic development. Financial inclusion is also vital, covering both the financing of SMEs and encouraging entrepreneurship as well as the optimal use of growing financial re­sources derived from natural resources and raw materials to develop infrastructure, support edu­cation, improve social welfare and invest in local projects.
The Smart Partnership Movement looks forward to supporting the African Union’s valuable work achieving its vision of a prosperous Africa over the next fifty years and beyond.
May 2013
CPTM Smart Partners’ Hub, London

SMART PARTNERSHIP MOVEMENT
Council of Patrons & Advisers
Chair of the Smart Partnership Movement and Host Patron & Adviser of Uganda (Global ‘09) to­gether with Heads of State/Government from Malaysia, Angola, Botswana, Democratic Republic of Congo, Lesotho, Malawi, Mauritius, Mozambique, Namibia, Seychelles, South Africa, Swaziland, Zambia, Zimbabwe, Burundi, Kenya, Rwanda, as well as Ghana & Barbados

HOST PATRON & ADVISER
GLOBAL 2013
H.E.  Jakaya Mrisho Kikwete
President of United Republic of Tanzania; CPTM Fellow

TASWIRA TOKA BUNGENI DODOMA LEO

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Dkt.  Emmanuel  Nchimbi  akitoa kauli ya Serikali Bungeni kuhusu vurugu zilizotokea Mkoani Mtwara. 2 
Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anne Makinda  akiahirisha Bunge kutokana na vurugu zilizotokea Mkoani Mtwara 3 
Waziri wa Nchi  ofis ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji)  Merry Nagu akiomba kutengua kanuni  ya Bunge  Na. 38 ili kuruhusu suala la vurugu za Mtwara kujadiliwa Bungeni.
Waziri Mkuu Mhe.  Mizengo Pinda akizungumza na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Jaji Frederick Werema  pamoja na baadhi ya Mawaziri   ndani ya ukumbi wa Bunge mara baada ya kuahirishwa kwa kikao cha Bunge . 5 
Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Prof. Sospeter Muhongo  akizungumza na baadhi ya Mawaziri na Wabunge ndani ya ukumbi wa Bunge mara baada ya Spika wa Bunge kuahirisha bunge   6 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Emmanuel Nchimbi (Kushoto) akizungumza na mbunge wa Kinondoni Mhe. Iddi Azzan nje ya ukumbi wa Bunge mara baada ya bunge kuahirishwa. 7 
Wabunge wa Viti Maalumu wakiwa nje ya ukumbi wa Bunge baada ya Spika kuahirisha Bunge. Kutoka kushoto ni Mhe. Lucy Owenya(CHADEMA), Katikati  Mhe. Mkiwa Kimwanga(CUF) na kulia ni Mhe. Dkt. Merry Mwanjelwa(CCM).
Naibu Waziri wa mambo ya Ndani ya Nchi Pereira Ame Silima (Katikati), Naibu wa Viwanda na Biashara Mhe. Greygory Teu (kushoto) na mbunge wa Kilosa Mhe. Mustafa Mkullo wakizungumza nje ya ukumbi wa  Bunge.
9 
Kundi la Waandishi wa Habari wanaoripoti  habari za Bunge wakitoka ndani ya ukumbi huo mara baada ya Spika wa Bunge kuahirisha kikao cha Bunge.
PICHA NA ZAWADI MSALLA-MAELEZO DODOMA

Uwazi na Uwajibikaji katika Usimamizi na Matumizi ya Maliasili za Nchi Hukuza Maendeleo


Mojawapo kati ya vipaumbele muhimu vya Marekani nchini Tanzania ni kukuza maendeleo ya kiuchumi na kujenga uwezo (empowerment) wa raia wote kwa ubia na Watanzania kutoka sekta zote. Nchi hii imejaaliwa neema ya kuwa na maliasili nyingi na utajiri mkubwa, mbali na kuwa na vivutio vingi vya dunia kama vile Mlima Kilimanjaro, mbuga za wanyama za Taifa na maeneo ya urithi wa Dunia yanayotambuliwa na UNESCO kuanzia Kilwa Kisiwani hadi Zanzibar. Wakati dunia ikitambua hazina hizi kuwa na thamani kwa dunia nzima, bado ukweli ni kuwa, kwa njia ya kipekee kabisa hazina hizi ni za Kitanzania. Pamoja na hali hii, baadhi ya raia wanajiuliza ni kwa namna gani uchumi wa Tanzania utabadilika na kuwa ule wenye kuleta ustawi. 

Mustakabali wa maendeleo ya Tanzania utategemea mawazo na maono ya uongozi wa Watanzania wenyewe. Nimevutiwa sana na jitihada za Watanzania kutoka serikalini na taasisi huru za kiraia kutafuta njia mpya zenye uwazi, uwajibikaji na uadilifu zaidi katika kusimamia na kutumia utajiri mkubwa wa asili ambao nchi hii imejaliwa kwa manufaa ya wote. Mpango wa Kimataifa wa Uhamasishaji Uwazi na Uwajibikaji katika Tasnia zinazohusika na Uvunaji Maliasili (Extractive Industry Transparency Initiative - EITI)  ni nyenzo inayoweza kusaidia katika kufikia azma hii adhimu na inayostahili kufikiwa kwa haraka .

Yatupasa tutambue kuwa zaidi ya watu bilioni 3.5, takriban nusu ya watu wote duniani, wanaishi katika nchi zilizo na utajiri wa asili kwa mfano mafuta, gesi na madini. Hata hivyo, katika maeneo mengi, utajiri huu hautumiki katika kusaidia mipango ya maendeleo ya mataifa yao au kusaidia kuwakwamua raia kutoka katika lindi la umasikini.  Mojawapo kati ya sababu kuu ya hali hii ni kuwa uvunaji wa rasilimali hizi hutoa changamoto nyingi kwa serikali. Changamoto hizo ni pamoja na ile ya kuhakikisha kuwa uvunaji huo unasimamiwa kamilifu, kwa uwazi na kwa njia inayowahusisha kikamilifu wadau wote. Kutokana na hali hii huu ni wakati mwafaka wa kufikia makubaliano mapana kuhusu viwango vya juu tunavyopaswa kuvifikia katika usimamizi wa rasilimali hizi.

Tarehe 23 na 24 Mei mwaka huu, wawakilishi wa serikali, sekta binafsi na jumuiya huru za kiraia kutoka duniani kote walikutana huko Sydney, Australia kwa ajili ya Mkutano wa Sita wa Kimataifa wa EITI.  EITI ni mfumo kimataifa ambao serikali kwa hiari yao zenyewe, huahidi kusimamia kwa uwazi na uwajibikaji shughuli za utafutaji, uchimbaji na biashara ya mafuta, gesi na madini katika nchi zao.  Ni kwa sababu hiyo, Marekani inaelekea kuungana na Tanzania na jumuiya ya mataifa mengine zaidi ya 35 kutoka Afrika, Asia, Marekani ya Kusini na Ulaya ambayo yameonyesha dhamira ya kuwajibika kwa dhati na kwa uwazi kwa watu wao kwa kuwa wanachama kamili wa EITI. 

Kwa kupitia EITI, nchi wanachama hushirikiana na sekta binafsi na asasi za kiraia kuchapisha taarifa ya mwaka ambayo, pamoja na mambo mengine, huonyesha taarifa za mapato ambayo serikali imeyapata pamoja na taarifa za mapato ya makampuni yanayojihusisha na shughuli za uchimbaji na biashara ya mafuta, gesi na madini. Mfumo huu huongeza uwazi, huimarisha uaminifu na kutoa takwimu muhimu zinazohitajika katika kuhakikisha na kufuatilia uwajibikaji.

Marekani imekuwa ikiisaidia EITI toka kuanzishwa kwake zaidi ya miaka kumi iliyopita. Mwezi Desemba 2012,   tulifurahishwa na tangazo kwamba Tanzania imekuwa nchi ya kumi barani Afrika kukidhi viwango vya EITI. Tunapongeza hatua hii kubwa iliyopigwa na Tanzania katika kukuza uwazi na uwajibikaji. Jitihada za Tanzania kujiunga na EITI zilianza mwaka 2009 na kufanikiwa kwake kufanya hivyo katika kipindi cha miaka mitatu tu  kunaonyesha jinsi misingi EITI kuhusu  uwazi katika mapato ilivyo na manufaa kwa nchi zote katika kanda zote na viwango vyote vya maendeleo.

Bunge la Marekani huzitaka baadhi ya kampuni za Kimarekani zinazojihusisha na shughuli za mafuta, gesi na madini kuwasilisha taarifa zao za kila mwaka kwa Tume ya Masoko ya Hisa (U.S. Securities and Exchange Commission) kubainisha malipo mahsusi wanayoyatoa kwa serikali mbalimbali duniani kwa ajili ya shughuli za mafuta, gesi na madini. Taarifa hizi zitajumuishwa na zile za EITI kuonyesha malipo yanayopokelewa na serikali mbalimbali kutokana na maliasili zake, hata kama nchi hizo si wanachama wa EITI. 

Hata hivyo, uwazi katika mapato pekee hautoshi kuwasaidia raia kuona picha ya jumla ya jinsi ambavyo serikali zao zinasimamia rasilimali  yao ya mafuta, gesi na madini. Ni lazima twende mbali zaidi.  Hivyo wiki hii mjini Sydney, wanachama watakubaliana kuhusu mabadiliko kadhaa ya kimkakati katika mpango wa EITI.

Lengo ni kufanya taarifa za EITI kuwa za kina na zenye kuaminika zaidi  na zilizo rahisi kufanyiwa uchambuzi. Aidha, mabadiliko hayo yatazitaka serikali kutoa taarifa muhimu kwa raia wake kuhusu sekta za mafuta, gesi na madini katika nchi zao, ikiwa ni  pamoja na taarifa kuhusu leseni zilizotolewa, makampuni au watu waliopewa leseni hizo, kiasi gani kinazalishwa na nafasi ya makampuni ya mafuta/madini yanayomilikiwa na serikali katika sekta husika. Aidha, EITI itazihimiza serikali kwenda mbali zaidi na kuchapisha kwa hiari yao wenyewe mikataba halisi iliyoingia na makampuni husika.  Utaratibu huu wa uwazi, utakuwa na manufaa kwa Makampuni ya Kimarekani kwa kuyawezesha kuyaelewa vizuri mazingira ya kiutendaji na kibiashara ya nchi husika yanapofikiria kufanya maamuzi kuhusu uwekezaji.

Marekani inaunga mkono mabadiliko haya yatakayowezesha EITI kuwa chombo che ufanisi zaidi katika kuwasaidia raia katika nchi zenye utajiri mkubwa wa maliasili kufaidika kutokana maliasili hizo. Wakiwa na taarifa, wananchi wataweza kuziwajibisha serikali zao hivyo jamii yote kwa ujumla kunufaika kutokana na mapato yatokanayo na rasilimali zake. Kwa kuwa na uwazi na matumizi yenye ufanisi ya maliasili, raia ambao hapo awali walikuwa katika lindi la ufukara nao pia wataweza kuwa na tumaini la kuwa na mstakabali mwema wenye ustawi ambapo wataweza kupata huduma bora za afya, elimu bora na kuweza kutumia uwezo wao kwa kadri ya upeo wao kuchangia katika maendeleo ya Tanzania.

Alfonso E. Lenhardt 
Balozi wa Marekani katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

CRDB YATOA VIFAA VYA MICHEZO KWA JWTZ KUPITIA AKAUNTI YAKE YA TANZANITE

Brigedia Jenerali wa JWTZ, Paul Peter Massao akimkaribisha Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei Makao Makuu ya Jeshi hilo.
Mazungumzo
Luteni Jenerali, Paul Mella akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa vya michezo vilivyotolewa na benki ya CRDB kupitia akaunti yake ya Tanzanite kwa ajili ya wapiganaji wanaokwenda kulinda amani nchini Kongo.
Luteni Jenerali, Paul Mella akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa vya michezo kwa wapiganaji wanaokwenda kulinda amani nchini Kongo.
Wapiganaji walioshiriki zoezi la kulinda amani nchini Darfur
Wapiganaji walioshiriki zoezi la kulinda amani nchini Dafur
Mkurugenzi Mkuu wa CRDB, Dk Charles Kimei akizungumza katika hafla hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa CRDB, Dk Charles Kimei akizungumza katika hafla hiyo.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akimkabidhi sehemu ya vifaa vya michezo vilivyotolewa na benki hiyo kupitia akaunti yake ya Tanzanite, Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Luteni Jenerali Samwel Ndomba kwa ajili ya wanajeshi wanaokwenda kulinda amani nchini Kongo. Hafla hiyo ilifanyika Makao Makuu ya Jeshi Upanga jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akimkabidhi sehemu ya vifaa vya michezo, Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Luteni Jenerali Samwel Ndomba kwa ajili ya wanajeshi wanaokwenda kulinda amani nchini Kongo. Hafla hiyo ilifanyika Makao Makuu ya Jeshi Upanga jijini Dar es Salaam
Mnadhimu Mkuu wa JWTZ, Luteni Jenerali, Samweli Ndomba akifafanua jambo wakati wa hafla ya kupokea vifaa vya michezo kutoka benki ya CRDB
Mnadhimu Mkuu wa JWTZ, Luteni Jenerali, Samweli Ndomba akifafanua jambo wakati wa hafla ya kupokea vifaa vya michezo kutoka benki ya CRDB.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akiagana na Mnadhimu Mkuu wa JWTZ, Luteni Jenerali, Samweli Ndomba. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akiagana na Lutni Jenerali, Paul Mella, huku Mnadhimu Mkuu wa JWTZ, Samweli Ndomba akiagana na Meneja Wateja Binafsi, Farida Mbwana Hamza. 
 Meneja wa Wateja Binafsi wa Benki ya CRDB, Farida Mbwana Hamza (kulia), Meneja Uhusiano wa Akaunti ya Tanzanite, Lucy Naivasha, na Meneja Mahusiano wa Benki ya CRDB, Godwin Semunyo wakiwa na  Brigedia Jenerali, Paul Peter Massao.
Maofisa wa Benki ya CRDB wakiwa katika picha ya pamoja na wapiganaji wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ)
Meneja Mahusiano wa Benki  ya CRDB, Godwin Semunyu akimpa maelekezo Meja Erick Komba wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa vya michezo kwa ajili ya wanajeshi wanaokwenda kulinda amani nchini Kongo.

DAR ES SALAAM IS READY TO HOST VIBE RUNWAY FRESH NEW FASHION AND MUSIC SHOW DESIGNERS FROM USA, ZAMBIA AND KENYA TO SHOWCASE


 As Fashion Capital city of Tanzania On Saturday 25th of May, 2013 Dar es Salaam will mark its new history in the Fashion Industry by hosting fresh new Fashion show in town VIBE RUNWAY at Ledger Plaza Bahari Beach Hotel, whereby the fashion event will showcase new and established designers both local and International with the latest innovative developments in glamour and style.
VIBE RUNWAY is one of its kind Fashion events that aim to not only combines fashion designers and art, but also brings together live musical entertainers to set the stage up for an unforgettable entertainment experience.
 “This event seeks to further echo fashion as big business and entertainment as well with a host of potential in Tanzania by attracting the city’s talented and successful designers, Infusing unprecedented fashion and music brightest entertainers to provide an extraordinary fashion experience on one runway, as Organizers, everything is ready for our side and we are waiting the excitement from the show”, said Veronica Lugenzi, founder and organizer.
 VIBE RUNWAY is a fashion show and music show, featuring music and designers showcasing top designs, it will pair some of music's hottest acts with a parade of beautiful models and puts them all on the same runway.

The lineup for VIBE RUNAWAY’s most anticipated fashion event has finally been released! As the event day quickly approach, VIBE RUNAWAY is proud to announce 
 the participating designers, Performers, Presenters, and models that will vibrate the city within one night.
 The Iconic designer Asia Idarous Khamsin will make one of the remarkable shows and lead the designer team. As director of Fabak Fashions in Dar es Salaam, she organizes the annual Lady in Red and Kanga Za Kale fashion shows. Khamsin’s interest also lies in aiding and promoting young and aspiring designers in Tanzania by giving them the chance to showcase their designs in the events she organizes.

Self-taught designer Kemi Kalikawe is in the list, founded Naledi Fashion House in 2008 in Dar Es Salaam as an addition to Naledi Interior Design that was founded in 2006 in Nairobi. She always knew she wanted to be a designer from a young age, therefore after a 3 month course in Stage Design and Textile Design at Bagamoyo Art College; she went to Kenya to study Interior Design for 3 years. Other designers are B 
 Designes and VS: VERNIC from Tanzania, Mohamed Bana, Kenya based designer, Estelle Mantel from Zambia and from Washington DC the one and only Ibrahim Pure.
The parade on stage will witness super models from Tanzania, Meena Xirs, Rimaly Said Odemba, Ms. Universe - Winfrida Dominique, Ms. Tanzania Sports Personality -Mary Chizi, Macrida Joseph, Neema Doreen Sylvery, Rachida Ussuale and Lota Mollel.

“As the aim of the show, VIBE RUNWAY features some Music Artists from Tanzania to beautify and vibe the show, 2012 Tanzani Big Brother Representertive Julio Batalia, G1, JC, Melisa John, Makjams and King Kapita, will give the performance on that Saturday night. Host - Kohntar Perry, Presenter from Choice Fm will host the show and our official DJ is DJ 4U” Mentioned Miss Veronica. 
 The VIBE RUNWAY show 2013 is proudly sponsored by Vayle Springs, TeenSpot Magazine,, Gonga Mx Blog, Missie Popular Blog,  and Ledger Plaza Bahari Beach Hotel.