Saturday, March 1, 2014

YANGA YAITANDIKA AL AHLY BAO 1 - 0 UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR LEO

 Kikosi cha Yanga 
 Kikosi cha Al Ahly
 Mshambuliaji wa timu ya Yanga,Mrisho Ngassa akiondoka na mpira huku Beki wa Timu ya Al Ahly ya Misri akitafuta namna ya kumzuia katika Mchezo wa Mashindano klabu bingwa Barani Afrika,uliomalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam hivi sasa.Yanga imeshinda bao 1 - 0.
 Kiungo mchezeshaji wa Yanga,Haroun Niyonzima akitafuta namna ya kuwatoka mabeki wa Timu ya Al Ahly ya Misri katika Mchezo wa Mashindano klabu bingwa Barani Afrika,uliomalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam hivi sasa.Yanga imeshinda bao 1 - 0.
 Kiungo mchezeshaji wa Yanga,Haroun Niyonzima akizuiwa na Beki wa Timu ya Al Ahly ya Misri,Ramy Abdel Aziz katika Mchezo wa Mashindano klabu bingwa Barani Afrika,uliomalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam hivi sasa.Yanga imeshinda bao 1 - 0.
Kipa wa timu ya Al Ahly ya Misri,Sherif Ekramy Ahmed akida moja ya hatari iliyokuwa ikielekeshwa langoni kwake na Mshambuliaji wa Yanga,Hamis Kiiza.
 Heka heka ya kuwania mpira wa Kichwa.
 Mshambuliaji Machachari wa timu ya Yanga,Emmanuel Okwi akiwachachafya mabeki wa timu ya Al Ahly ya Misri katika mchezo wao uliomalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam wa kuwania tiketi ya kusheza 16 bora ya Klabu Bingwa Barani Afrika.katika mchezo huo,Yanga imeifunga timu ya Al Ahly bao 1 - 0. 
 Emmanuel Okwi wa Yanga akichezewa faulo na mabeki wa timu ya Al Ahly ya Misri.
 Heka heka langoni mwa timu ya Al Ahly.
Mshambuliaji Emmanuel Okwi wa Yanga leo ndio alikuwa mwiba kwa timu ya Al Ahly,maana alikuwa akikabwa na Mabeki wawili wawili........
 Kipa wa timu ya Al Ahly ya Misri,Sherif Ekramy Ahmed akiruka mithili ya nyani wakati akiokoa moja ya hatari zilizokuwa zikielekezwa langoni kwake.
 Okwi anatafuta namna ya kuchia shuti.
 Mshambuliaji wa Yanga,Didier Kavumbagu akiwania mpira na Mabeki wa timu ya Al Ahly ya Misri.
 Ulinzi maridhawa kabisa ulitawala Uwanjani hapa.
 Ilikuwa ni nyomi la hatari.
Wachezajiwa timu ya Yanga wakishangilia ushindi wao sambamba na Mashabiki wao lukuki waliofurika uwanjani hapa.

Mfungaji wa bao pekee la Yanga,Nadir Haroub akirejea uwanjani baada ya kutoka kushangilia pamoja na washabiki wao.
 Benchi la ufundi la Al Ahly ya Misri.
 Benchi la Yanga.
 Mashabiki wa Al Ahly wakishangiliwa mwanzo mwisho,wakisaidiwa na Mashabiki wa timu ya Simba. 
 Okwiiiiiiii.......
Kocha wa Al Ahly akihaha kutoa maelekezo kwa Wachezaji wake. 
 Mabeki wa timu ya Yanga,Nadir Haroub pamoja na Kelvin Yondani wakiwa wamejipanga vyema kuuzuia mpira wa Mshambuliaji wa timu ya Al Ahly,Moussa Yedan.
 "Poa tu mwana,hii ni fea pleii tuuuuu......" 
 Ni shangwe tupu kwa Mashabiki wa timu ya Yanga uwanjani hapa hii leo. 
Mashabiki wa timu ya Al Ahly wakifungasha virago vyao baada ya kulala kwa bao 1 - 0.
 Kocha wa Yanga akisema na wachezaji wake mara baada ya kipenga cha mwisho kulia.
 Kufungwa kubaya jamaniiiiii....
 Mara baada ya Yanga kupata Goli la kwanza na la pekee,Mashabiki wa Simba walianza tena kunyoa viti na kuwarushia mashabiki wa timu ya Yanga waliokuwa wakishangilia ushindi wao huo. 
 Wazee wa feva wakiwatuliza washabiki hapo wa Simba.
Cheki mapengo ya kung'olewa kwa viti uwanjani hapa.Hali hii ni nani anatakiwa kuidhibiti???

ukishangaa ya mussa....

Yes, that is cash piled on the table in the background!
Just a small collection of guns - these people are not really dangerous at all; not.
Yes, that is real gold on these guns!
Gold and Titanium 45 Caliber semi automatic pistols - they found 16 of these!
Go and kill in the name of the Lord my son was etched!  There was a matched pair of these found.
357 Magnum semi automatic with solid gold grips.
This guy had a better gun collection then most legitimate museums do.
Just a quaint little villa in the hills - Drug money bought it all!
Man made cave and hot tub inside the home.
A collection of exotic animals - which were cared for in the grandest fashion by the way.
8 Lions were on the property.
A very rare Tiger!
The back yard pool.
Exotic art collection -  some of which was illegal to own - some stolen.
More guns than you could ever imagine!
This pile of cash before it was counted was estimated to be approximately 18 Billion Dollars!  After it was counted it turned out to be a little more than 22 Billion Dollars!
22 Billion Dollars from another angle.
Guns and more cash hidden all over the house, along with ample ammo, just in case of trouble.
Additional stacks of cash were found in every nook and cranny!
This case is filled with 100 dollar Bills estimated to be and additional 1/2 a million dollars and no doubt headed out to make another drug by perhaps from the Columbians.
Additional 18 plastic bins filled with 100 dollar bills were discovered!
Another cabinet stack tight with cash - all 100 dollar bills.
Even more 100 dollar bills!
Each of these stacks of 100 dollar bills holds $250,000 (a quarter of a million dollars)!  They also had millions in Columbian money and Mexico Pesos although they preferred American dollars for the most part.
Folks, there were even stacks of Chinese Yen found in one closet!
More Gold machine guns and pistols -  more were never fired, just held for collection value.
They just burned it all down!
The money and valuables found in this one house alone, would be enough to pay for health insurance for every man, women and child in the USA for 12 years!
There are believed to be approximately 27 more of these houses in Mexico alone not to mention the ones in other countries who are enriching themselves in the illicit drug trade.  
These people have so much money, they make the great Arab oil sheiks look like welfare recipients.  Their money can buy the best politicians, some cops, the best judges, or whatever they need they just throw down stacks of cash and it is theirs! 
This is why the drug problem is so difficult to fight.

MAMBO 6 YANAYOMFANYA MTU AWE KIONGOZI BORA NA SIO BORA KIONGOZI

Tukiacha mbali picha ambayo mara nyingi au kwa miaka mingi imekuwa ikijengwa  vichwani mwa wengi wanapoona na kudhani kwamba fulani ni kiongozi bora [pengine kwa muonekano tu], au kwa sababu anashuka kutoka kwenye gari kwa mbwembwe, tabasamu baada ya kufunguliwa mlango na mkanda na kisha kupokelewa briefcase yake, yapo mambo kadhaa ambayo yanamfanya mtu awe kiongozi bora na sio bora kiongozi. Na kadri siku zinavyokwenda, taswira ya kiongozi kwa muonekano tu inazidi kupotea. Vitendo,maadili,mafanikio, uvumbuzi na maendeleo vinachukua mstari wa mbele.

Tofauti na miaka ile ambayo picha ya kiongozi bora ilikuwa kama hiyo hapo juu, siku hizi viongozi bora wapo na wanajitokeza katika hali tofauti tofauti kabisa. Anaweza kuwa asiyevaa suti kama Dalai Lama na akawa kiongozi bora. Au asiyevaa suti bali t-shirt na jeans tu kama alivyokuwa Steve Jobs wa Apple au Mark Zuckerberg boss wa Facebook. Mifano ya viongozi hawa ipo mingi.

Kituo cha utafiti na mafunzo ya uongozi cha Dale Carnegie cha jijini New York nchini Marekani kinasema katika utafiti wao wamegundua kwamba kinachomfanya mtu awe kiongozi bora sio suti, briefcase, tabasamu[ hususani lile la uongo] bali uwezo na nia ya dhati katika kuamsha ari, kuwawezesha unaowaongoza, kuwafanya wajiamini na kuwapa motisha watu unaowaongoza.

Pamoja na hayo, na kutokana na ukweli kwamba leo hii tuna kila aina ya viongozi, yapo baadhi ya mambo yanayowatofautisha viongozi bora na bora viongozi. Haya hapa ni baadhi yake;
  • Aweze Kuyakabili Matatizo au Changamoto
Kiongozi bora ni yule ambaye ana ujasiri wa kutosha wa kukabiliana na kila aina ya changamoto au matatizo ambayo yanaweza kujitokeza iwe aliyatarajia au hakuyatarajia.

Dunia ya leo imejaa changamoto za kila aina. Kila kukicha kuna jipya na gumu zaidi. Uchumi umeporomoka, fedha haina thamani tena, kimbunga kikali kimekuja na kuipindua juu chini shule ya kijiji. Kiongozi bora anafanyaje? Anapotelea mjini kwa kisingizio cha kuwa “bize” au anakuwepo bega kwa bega kutatua tatizo?

Jibu lipo wazi. Kiongozi bora atakuwepo na kuwasiliana na kila mtu anayemuongoza iwe ni ofisini au jimboni kuhusu ukweli halisi na ukubwa wa tatizo na jinsi ambavyo yeye kama kiongozi analishughulikia [kwa kushirikiana na kila mtu wakiwemo anaowaongoza] tatizo au changamoto husika.
  • Awe Muaminifu
Kiongozi bora lazima awe muaminifu. Uaminifu unaanzia kwenye kuwa mkweli. Anaposema atafanya hili au lile, alifanye. Asipolifanya, awe muwazi na kuwaeleza wale anaowaongoza ukweli wa sababu zilizofanya asitimize ahadi yake na jitihada anazofanya kutimiza ahadi yake.

Kwa mfano wananchi wanapomchangua “kiongozi” kutokana na sera na ahadi za kutatua tatizo la ukosefu wa maji safi jimboni kwao kisha miaka mitano baadae ahadi hiyo ikawa haijatimia, ni wazi kwamba imani kwa kiongozi huyu itafifia kama sio kupotea kabisa. Mbaya zaidi pale atakapokuja na sababu ambazo hazina mashiko huku kila mtu akiona wazi kwamba ahadi yake ilikuwa ahadi hewa au ya kisiasa.

Onyesha kwamba unawajali na kuwathamini unaowaongoza. Yaelewe matatizo na changamoto za unaowaongoza. Shirikiana nao bega kwa bega kuyatatua. Usiwe kiongozi wa ofisini tu bali nenda kule walipo. Na usiende kwa nia ya kupigwa picha tu. Ili wakuamini ni muhimu wakaona kwamba wewe sio “mwizi” tu wa fursa.
  • Kuwa Halisi [Asiwe Feki]
Mojawapo ya mambo ambayo sio tu yanamfanya mtu awe bora kiongozi bali apoteze kabisa hata nafasi ya kuongoza ni pamoja na kuwa “feki”. Ni rahisi sana kwa mtu/watu kutambua kwamba huyu si yeye. Anajifanya kuwa mtu ambaye siye.

Kwa bahati mbaya hakuna mtu anayependa “feki”. Viongozi wanasiasa huanguka sana kwenye mtego huu. Wengi wanadhani wananchi hupenda kusikia mashairi na ngonjera tamu tamu pekee. La. Labda zamani. Siku hizi ukiwa kitimbakwila utajulikana kirahisi na utakuwa nje ya ulingo. Wenzetu wanasema Walk The Walk and Talk The Talk.

Hata kama wewe ni kiongozi wa ofisi au mfanyabiashara, pindi tu utakapokuwa “feki” wateja wako watajua. Watakukimbia. Watahisi hata vitu unavyouza ni “feki” kwa sababu wewe mwenyewe unaonekana feki au unajibeduisha kuwa sivyo. Kuwa orijino. Unapenda kucheka au kuchekesha? Cheka. Wachekeshe unaowaongoza. Unapenda muziki? Usihofu kuonyesha wazi kwamba unapenda muziki. Tumia vitu unavyovipenda au maarifa unayoyamudu zaidi kutengeneza aina yako ya uongozi.
  • Ajiheshimu
Kiongozi bora lazima ajiheshimu. Na dhana ya kujiheshimu ni pana. Kuna kujiheshimu katika nyumba na mahusiano yako iwe na wanao, mkeo, wazazi wako, ndugu, jamaa na hata marafiki. Kuna kuiheshimu ofisi yako na watu unaowaongoza. Kiongozi ambaye kila siku anakabiliwa na tuhuma za ulaji rushwa, uongo, umalaya ni wazi kwamba hajiheshimu na hivyo ni ngumu kuwafanya watu wengine wamheshimu. Nawajua baadhi ya “bora viongozi” ambao wametumbukia huko kutokana na tabia zao za ufuska ambazo ingawa wanahisi watu hawajui, kwa kiasi kikubwa zimewapotezea heshima ya uongozi na hususani uongozi bora.

Unapojiheshimu, inakuwa rahisi kuongoza wengine. Hakuna mtu anayependa kujishirikisha na mtu asiyejiheshimu. Watu hujisikia faraja kuhusiana au kufanya biashara na watu wanaojiheshimu. Pia hata kama unaongoza ofisi au biashara tu,wateja wenye akili timamu wanataka kutumia hela zao mahali ambapo ofisi au biashara inaheshimu na kutimiza ahadi zao kufuatana na misingi. Ukisema kwamba ninyi ndio duka lenye bei chee zaidi na bidhaa halisi, basi iwe ni kweli. Vinginevyo inaashiria kwamba hamjiheshimu. Ni waongo. Uongo ni sehemu ya kutojiheshimu.
  • Jifunze/ Taka Kujua Zaidi/ Nenda Na Wakati
Kiongozi bora ni yule ambaye anataka kujifunza zaidi na ni mtafiti. Mwisho wa darasa sio mwisho wa kujifunza kwa kiongozi bora. Zitto Kabwe, Mbunge wa Kigoma Kaskazini aliwahi kunieleza katika mahojiano yangu naye jinsi ambavyo alishangaa wakati fulani kusafiri na viongozi fulani kutoka Tanzania mpaka Ujerumani na asione wakisoma hata vipeperushi vinavyokuwa kwenye viti achilia mbali vitabu,magazeti nk.Viongozi bora wanauliza maswali. Wanauliza maswali kwa nia ya kujifunza, kupata maarifa na taarifa. Ni wasikivu na wapo tayari kufundishwa.

Kwa bahati nzuri dunia ya leo ina kila nafasi na uwezekano wa kujifunza. Hizi ni zama za sayansi na tekinolojia. Kiongozi bora atataka kujua…hicho kitu kinachoitwa Twitter ni nini? Kinafanyaje kazi? Atajiunga. Atataka kujua jinsi watu wanavyowasiliana siku hizi. Atataka kujua jinsi nchi za wenzetu wanavyofanikiwa katika masuala mbalimbali. Atajitahidi na kuchunguza mpaka mwisho kuona kama sayansi hiyo au maarifa hayo yanaweza pia kutumika nchini kwake,jimboni kwake, ofisini kwake nk. Kiongozi bora atasoma vitabu,majarida,magazeti, nk kwa nia ya kujifunza zaidi.
  • Kuwa Mtendaji
Yote niliyoyataja hapo juu yanakamilishwa au kuhusishwa moja kwa moja na utendaji. Kiongozi bora haishii kwenye kuongea tu huku akijizungusha kwenye kiti na kuagiza chai. La.Anatenda. Ananyanyuka, kwenda na kutenda kama mfano. Tunapomkumbuka Mwalimu Nyerere kama kiongozi bora aliyewahi kutokea ni kwa sababu alikuwa mtendaji. 

Aliongea,kuelekeza,kuonya lakini mwisho wa siku alikuwa mtendaji.
Nyanyuka na enenda ukaifanye kazi. Onyesho kwa vitendo kwamba wewe ni kiongozi bora na sio bora kiongozi.
Jeff Msangi ni mwandishi, mchunguzi wa masuala mbalimbali na mmiliki wa mtandao wa www.bongocelebrity.com. Unaweza kuwasiliana naye kupitia jeffmsangi at gmail dot com

Friday, February 28, 2014

THE AMERICAN PEOPLE’S COMMITMENT TO COMBATING WILDLIFE TRAFFICKING IN TANZANIA

By Virginia Blaser

I would like to take the opportunity of  this year’s World Wildlife Day to highlight the American people’s commitment to combatting the global scourge of wildlife trafficking and to draw attention to how and where the American and Tanzanian peoples and governments can work together to save the world’s precious wildlife.  

I know that everyday Tanzanians share these goals, and I note that President Mwalimu Julius K. Nyerere once said that "…the survival of our wildlife is a matter of grave concern to all of us in Africa. 

These wild creatures amid the wild places they inhabit are not only important as a source of wonder and inspiration, but are an integral part of our natural resources and our future livelihood and well being."  

During his trip to Tanzania last summer, President Barack Obama underscored the American commitment by signing an Executive Order on combating wildlife trafficking.  This order defined wildlife trafficking as “the poaching of protected species and the illegal trade in wildlife and their derivative parts and products.”  

Just a few weeks ago, President Obama added to our U.S. policy directions by signing the U.S. National Strategy for Combating Wildlife Trafficking.  This Strategy established the guiding principles and policy priorities for U.S. efforts to stem this illicit and highly destructive trade.

Combating wildlife trafficking is a global concern of particular significance to Tanzania.  Wildlife trafficking has become a lucrative trade in Tanzania, taking a serious toll on target species, driving poaching activities, and robbing Tanzania of precious resources, including elephants and rhinoceros. 

 Profits from this illicit trade also fund criminal enterprises and activities that endanger national security.  Furthermore, wildlife trafficking threatens a thriving tourism industry that provides employment to tens of thousands of Tanzanians and generates millions of dollars in revenue every year.  

Particularly frightening is the situation in the Selous Game Reserve, which demonstrates the dire need for action.  The Selous is the largest protected area on the African continent, covering 48,000 square kilometers; indeed it is so special that the Selous Game Reserve is one of only three UNESCO World Heritage Sites in Tanzania.  

Three years ago, Selous boasted 40,000 elephants.  Today you have barely 13,000.  If this trend continues unchecked, this unique and globally-recognized element of Tanzania’s natural heritage will disappear forever.

The Government of Tanzania has taken some significant, positive steps to combat wildlife trafficking and is deeply engaged in a process to ensure wildlife security issues are approached strategically and through an appropriate regulatory framework which also respects human rights.  

We support these ongoing efforts and encourage robust engagement across all ministries, including law enforcement and the judiciary.  The wildlife sector earns significant revenue for Tanzania and we encourage the government to dedicate an increased portion of this revenue to protect wildlife and the important jobs and industry that depend on this resource. 

  The American people are committed to working hand-in-hand with the Tanzanian people to build the capacity of local and national government agencies to address this critical issue and we encourage continued progress on these efforts.  To that end, the U.S. Government has offered technical assistance on both the economic and legislative aspects of the wildlife issue in Tanzania.

Through the United States Agency for International Development (USAID), the United States has contributed over $100 million to conservation in Tanzania since 1990 and we will continue our strong support of the biodiversity sector in Tanzania.  

We intend to continue our support of Wildlife Management Areas, landscape conservation and climate resiliency approaches to help conserve wildlife habitats and foster sustainable tourism for generations.  We are also developing a five-year program to assist the government of Tanzania and communities to improve the management and conservation of Tanzania's biodiversity.

Since 1990, conservation partners in Tanzania have received $4.1 million from the U.S. Government, through our Fish and Wildlife Service, for the conservation of elephants, rhinos, chimpanzees, and marine turtles.  We have also provided funds for Tanzanians to be trained in “wildlife investigations” at the International Law Enforcement Academy in Botswana and we recently funded 25 Tanzanian law enforcement personnel from TANAPA and the Wildlife Division to attend Regional Rural Border Patrol training. 

These courses offer Tanzania the opportunity to work with Uganda and Kenya to improve cross border cooperation to combat wildlife trafficking.  

Tanzania has some of the most important and largest wildlife populations and network of protected areas in the world, and these precious resources and treasured national legacy are under immediate threat due to poaching and the illegal wildlife trade. 

 I urge the Tanzanian people to robustly support anti-poaching initiatives at the local, regional and national level. Together we – members of government, international donor community, civil society, law enforcement, and environmentalists – can effectively put an end to this illicit trade and help protect the future of Tanzania’s natural resources for generations to come.

Wanafunzi wa Tanzania Thailand Waizungumzia sekta ya Madini

Kamishna Msaidizi wa Madini Mhandisi,Hamis Komba (wa pili kushoto) akiwa pamoja na Wanafunzi wa Kitanzania wanaosoma masomo ya Geomolojia katika Chuo cha ‘Asian Institute of Geological Science’ (AIGS) nchini Thailand. Wa kwanza kulia ni Agatha Mwinuka, anayefuata ni Emmanuel Minja na wa kwanza kushoto ni Doricas Moshi.
Wanafunzi wa Kitanzania nchini Thailand, wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wenzao kutoka mataifa mbalimbali , ambao wamelitembelea banda la Tanzania.
Wafanyakazi wa Wizara ya Nishati na Madini katika picha ya pamoja na wanafunzi hao katika banda la Tanzania.

Na Asteria Muhozya, Bangkok

Wanafunzi wa Kitanzania wanaosoma masomo ya Geomolojia katika Chuo cha ‘Asian Institute of Geological Science’ (AIGS) nchini Thailand, wamewataka wadau wa tasnia ya madini ya vito na usonara nchini Tanzania kuichukua sekta hiyo kwa umakini mkubwa kutokana na mchango wake kiuchumi.

Aidha, wameeleza kuwa, nchi ya Thailand imepiga hatua kubwa katika sekta ya madini ukilinganisha na Tanzania lakini bado Tanzania inaweza kufaidika zaidi katika sekta hiyo ikiwa kila mdau atatimiza wajibu wake kikamilifu ili madini ya vito yaongeze mchango katika pato la taifa.

Wameongeza kuwa, Tanzania bado ina nafasi ya kujipanga upya kuhusu kuboresha zaidi sekta hiyo kama ilivyo kwa nchi nyingine endapo mipango mikakati ya maboresho itatekelezwa na kusimamiwa kikamilifu.

Wanafunzi hao wameyasema hayo, wakati walipolitembelea banda la Tanzania katika maonesho ya 53 ya Vito vya Usonara na Madini yanayoendelea katika jiji la Bangkok ambapo nchi zaidi ya 150 zinashiriki maonesho hayo.

“Thailand wamejipanga vizuri katika sekta ya madini. Wafanyabiashara wa madini wana umoja. Wadau wa madini wanatakiwa kuelewa kuwa madini yanawakilisha utajiri wetu tulionao”. Amesema Agatha Mwinuka.

Aidha, wameitaka serikali na wadau wa Tanzania wanaoshiriki maonesho hayo kujifunza kutokana na changamoto wanazozipata kutoka kwa nchi nyingine, jambo ambalo litasaidia kuboresha sekta ya madini na vito, ikiwa ni pamoja na wafanyabiashara kuhakikisha kuwa wanafuata sheria na taratibu zilizopo.

“Tunaiomba serikali iendelee kuendeleza viwanda vya kukata madini. Ni jambo zuri kama shughuli hizi za kukata madini zitafanyika ndani ya nchi badala ya nje. Jambo hili linasaidia sana kuongeza thamani ya madini. Ameongeza, Emmanuel Minja.

Akiongelea kuhusu umuhimu wa kuendeleza na kuboresha kituo cha Tanzania Geomological Center, Doricas Moshi, ameeleza kuwa, kituo hicho kinaweza kutoa mchango mkubwa katika tasnia hii hasa katika nyanja ya ukataji madini na uthamini wa madini hivyo, ameitaka Serikali kukiongezea nguvu kituo hicho kutokana na umuhimu wake kwa maendeleo ya Tanzania.

“Chuotunachosoma hapa kinatumia sana mifano ya madini ya Tanzania katika kufundisha. Mengi yametoka nyumbani, hii ni ishara nzuri. Serikali iliangalie hili. Ameongeza Doricas.

Aidha, wameeleza kuwa, soko la kimataifa kwa madini ya Tanzania lipo, hivyo, wamewataka wadau wote kuhakikisha wanashirikiana vizuri na serikali kuendeleza sekta hiyo kutokana na umuhimu na mchango wake kwa taifa.

Akizungumzia mipango iliyopo ya kuboresha sekta hiyo, Kamishna Msaidizi wa Madini, Mhandisi Hamis Komba, amesema kuwa, Serikali kupitia Shirika la Madini Tanzania (STAMICO), inatekeleza mikakati ya kuwasaidia wachimbaji wadogo na wa kati ili waweze kuendana na mahitaji ya soko la kimataifa kwa kuwapatia mafunzo mbalimbali yakiwemo ya kukata madini, kuyaongezea thamani na kuwapatia mikopo kupitia Benki ya TIB.

“STAMICO imepewa jukumu la kuwaendeleza wachimbaji wadogo katika sekta ya madini hususani katika masuala ya uchimbaji, uongezaji thamani madini na biashara ya madini. Serikali imejipanga vizuri katika hilo”. Ameongeza Kamishana.

Ameongeza kuwa, Serikali inatambua kwamba wachimbaji wengi wapo katika sekta ya madini ya vito na usonara hivyo, jitihada za kuwaendeleza zitasaidia kufikia kiwango bora cha utendaji wao wa kazi.

Vilevile, ameongeza kuwa, kutokana na kuboreshwa kwa Sheria ya madini ya mwaka 2010 ambayo inaiwezesha STAMICO kumiliki asilimia 50 ya hisa katika mgodi wa Tanzanite One, jambo ambalo linaifanya Serikali kuwa mmiliki katika mgodi huo.