Thursday, November 3, 2016

SPIKA WA KWANZA WA BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI, KATIBU MKUU WA CCM, ABDULRAHMAN KINANA AKUTANA NA WABUNGE WA BUNGE HILO LEO


Spika wa kwanza wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA), Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, akizungunguza na wabunge wa Bunge hilo, walipomtembelea ofisini kwake jijini Dar es Salaam, ili umsalimia na kupata mawazo kutokana na uzoefu wake hasa alipokuwa Spika wa Bunge hilo la Afrika Mashariki. Wa Kwanza kulia upande wa mstari wa kushoto, ni Mwenyekiti wa Wabunge hao, Makongoro Nyerere, Shayrose Bhaji, Yves Nsabimana, Maryam Ussi, Twaha Tasilima, Wilime Asheri ambaye ni mratibu EALA, na kutoka kulia, mstari wa kulia ni, Katibu wa NEC Oganaizesheni, Mohammed Seif Khatib, na Wabunge wa EALA, Adam Kimbisa, Bernard Murunya, Abdulla Mwinyi,Angela Kizigha na mwisho Msemaji wa CCM, Christopher Sendeka.
Mwenyekiti wa Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Makongoro Nyerere, akiwasili Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, kuongoza msafara wa wabunge hao kumsalimia Spika wa kwanza wa Bunge hilo, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, leo
Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Shy-rose Bhanji, akiwasili Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, wakati msafara wa wabunge yeye na wabunge wenzake wa Bunge hilo, walipofika kumsalimia Spika wa kwanza wa Bunge hilo, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, leo
Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Shy-rose Bhanji, akiwasili Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, wakati msafara wa wabunge yeye na wabunge wenzake wa Bunge hilo, walipofika kumsalimia Spika wa kwanza wa Bunge hilo, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, leo. Kulia ni Mbunge Bunge hilo, Yves Nsabimana.
Mwenyekiti wa Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Makongoro Nyerere, akiteta jambo na Mbunge wa Bunge hilo, wakati wakimsubiri kuingia ukumbini, Spika wa kwanza wa Bunge hilo, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, leo
Katibu wa NEC, Oganaizesheni, Mohammed Seif Khatib akisalimiana na Mbunge wa Bunge la Afika Mashariki Bernard Murunya, alipowasili wakati Wabunge wa Bunge hilo, walipofika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumbai Dar es Salaam, kumsalimia Spika wa kwanza wa Bunge hilo, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, leo. Katikati ni Adam Kimbisa.


Katibu wa NEC, Oganaizesheni, Mohammed Seif Khatib akifurahia jambo na Makongro Nyerere wakati wakisalimiana ukumbini, kabla ya Kinana kuwasili
Katibu wa NEC, Oganaizesheni, Mohammed Seif Khatib akisalimiana na Mbunge wa Bunge la Afika Mashariki Shy-Rose Bhanji, alipowasili wakati Wabunge wa Bunge hilo, walipofika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumbai Dar es Salaam, kumsalimia Spika wa kwanza wa Bunge hilo, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, leo.
Katibu wa NEC, Oganaizesheni, Mohammed Seif Khatib (kulia), akiwa na Wabunge wa Bunge la Afika Mashariki, Adam Kimbisa, Bernard Murunya, na Abdulla Mwinyi, wakati wakimsubiri Kinana kuingia ukumbini
Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki Yves Nsabimana na Maryam Ussi, wakibadilishana mawazo ukumbini
Mbunge wa Afrika Mashariki Angela Kizigha akimsalimia Mbunge mwenzake wa Bunge hilo, Bernard Murunya alipowasili ukumbini

Spika wa kwanza wa Bunge la Afrika Mashariki, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimsalimia Mweneyekiti wa Wabunge wa Bunge hilo, Makongoro Nyerere alipowasili ukumbini
Kinana akimsalimia Shy-Rose Bhanji
Spika wa kwanza wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA), Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, akizungunguza na wabunge wa Bunge hilo, walipomtembelea ofisini kwake jijini Dar es Salaam, ili umsalimia na kupata mawazo kutokana na uzoefu wake hasa alipokuwa Spika wa Bunge hilo la Afrika Mashariki.
Spika wa kwanza wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA), Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, akizungunguza na wabunge wa Bunge hilo, walipomtembelea ofisini kwake jijini Dar es Salaam, ili umsalimia na kupata mawazo kutokana na uzoefu wake hasa alipokuwa Spika wa Bunge hilo la Afrika Mashariki.
ukumbini
Spika wa kwanza wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA), Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, akiwa katika picha ya pamoja baada ya kuzungunguza na wabunge wa Bunge hilo, walipomtembelea ofisini kwake jijini Dar es Salaam, ili umsalimia na kupata mawazo kutokana na uzoefu wake hasa alipokuwa Spika wa Bunge hilo la Afrika Mashariki.
Shy-Rose Bhanji akimshukuru Kinana.
Kisha akapozi naye kwa picha ya kumbukumbu
Halafu akapozi na Msemaji wa CCM, Ole Sendeka
Baadaye tena akajipiga selfie, akiwa na Katibu wa NEC, Uchumi na Fedha Zakia Meghji
Spika wa kwanza wa Bunge la Afrika Mashariki, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiagana na Makongoro Nyerere
Spika wa kwanza wa Bunge la Afrika Mashariki, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiagana na Twaha Tasilima. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO-theNkoromo Blog

CHAKALE DHAHABU TAMASHA LA UTAMADUNI LITAKALO KUTANISHA MAKABILA ZAIDI ZAIDI YA 100 NA MACHIFU

Mtaribu wa tamasha la 'Kale ni Dhahabu' ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Seree, Sabina ​Kaphipa akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana kuhusiana na tamasha la utamaduni litakalowahusisha machifu zaidi ya 100 wa Tanzania. Pamoja nae ni Afisa Masoko, Anael Masasi
Mtaribu wa tamasha la 'Kale ni Dhahabu' ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Seree, Sabina ​Kaphipa akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana kuhusiana na tamasha la utamaduni litakalowahusisha machifu zaidi ya 100 wa Tanzania. Pamoja nae ni Afisa Masoko, Anael Masasi (kushoto) na Msemaji wa Tamasha hilo, Juma Mwajacho (kulia) pamoja na Mke wa Chief.
Mtaribu wa tamasha la Kale ni Dhahabu ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Seree, Sabina Maro akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana kuhusu tamasha la utamaduni litakalowahusisha machifu zaidi ya 100 wa Tanzania.
 Logo ya tamasha
Kampuni inayoandaa tamasha.
 Sabina Kaphipa akicheza ngoma na wasanii wa Kundi la sanaa Makumbusho. BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.

MAJALIWA AMTEMBELEA MALECELA , BUNGE

 Waziri Mkuu,  Kassim Majaliwa akizungumza na wabunge  wa Nkansi Kaskazini, Ally Kessy wa Nkansi  (katikati) na Livingstone Lusinde wa Mtera kwenye viwanja vya bunge mjini Dodoma Bovemba 2, 2016.
 aziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akizungumza na Waziri wa Kilimo , Mifugo na Uvuvi ambaye pia ni Mbunge wa Buchosa, Dkt. Charles Tizeba kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Novemba 2, 2016. 
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu, John Malecela wakati alipomtembelea, nyumbani kwake mjini Dodoma Novemba 2, 2016.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
 Wazirii Mkuu Kassim Majaliwa akijibu Maswali  bungeni mjini Dodoma Novemba 3, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Wazirii Mkuu Kassim Majaliwa akijibu Maswali  bungeni mjini Dodoma Novemba 3, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wapiga kura wake kutoka jimbo la Ruangwa waliomtembelea bungeni mjini Dodoma Novemba 3, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wapiga kura wake kutoka jimbo la Ruangwa waliomtembelea bungeni mjini Dodoma Novemba 3, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na wapiga kura wake kutoka jimbo la Ruangwa  waliotembelea bunge mjini Dodoma Novemba  3, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)  

WANAFUNZI WA NELSON MANDELA WATAKIWA KUWA MSTARI WA MBELE KUSAIDIA KUTATUA MATATIZO YA MAZINGIRA, MAJI

Pichani juu na chini ni Balozi wa Umoja wa nchi za Ulaya EU kwa nchi za Afrika Mashariki Roeland Van De Geer akihutubia wanafunzi wa vyuo mbalimbali katika ukumbi Chuo cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela ambapo alifanya ziara ya kutembelea Chuo jijini Arusha.(Picha na Ferdinand Shayo).

Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela Profesa Karoli Njau akifafanua jambo katika ziara ya Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) kwa nchi za Afrika Mashariki, Roeland Van De Geer alipotembelea chuo hicho.
Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) kwa nchi za Afrika Mashariki Roeland Van De Geer akisalimiana na Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela Profesa Karoli Njau, wakati wa ziara ya balozi huyo chuoni hapo.
Picha ya pamoja ya washiriki wa semina ya malengo ya dunia ya Umoja wa Mataifa katika Chuo cha Nelson Mandela wakiwa na Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) kwa nchi za Afrika Mashariki, Roeland Van De Geer.
Picha ya pamoja ya washiriki wa semina ya malengo ya dunia ya Umoja wa Mataifa katika Chuo cha Nelson Mandela jijini Arusha.
Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela Profesa Karoli Njau (wa pili kulia) katika picha ya pamoja na Wawakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa, Hoyce Temu (wa pili kushoto) na Amon Manyama (kushoto).

SIKU 365 ZA DKT. MAGUFULI, HALMASHAURI ZAPOKEA BILIONI 177 MIRADI YA MAENDELEO

Na Eleuteri Mangi-MAELEZO, Dodoma.

Rais Dkt. John Pombe Magufuli ametimiza siku ya 365 Watanzania wameona, kushuhudia utendaji na mwelekeo wake wa kuiongoza Serikali ya Awamu ya Tano kwa mafanikio.

Kauli hiyo imetolewa na leo Bungeni mjini Dodoma na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa Majaliwa kabla ya kuanza kujibu maswali ya papo kwa papo ambayo huulizwa na Wabunge kwa Waziri Mkuu kwa kumwomba Naibu Spika Dkt. Tulia Akson kuridhia kuwakumbusha Watanzania kuhusu muda wa uongozi tangu Rais Dkt. Magufuli aingie madarakani.

“Jukumu letu, ni kumwombea Mhe. Rais aweze kuendelea vizuri na kazi ya kuiongoza nchi yetu na wananchi wote tuungane pamoja kila moja kwa dhehebu lake kuweza kuiombea Serikali hii ili iweze kupata mafanikio makubwa” amesema Waziri Mkuu.

Akijibu swali lililoulizwa na Munde Tambwe Abdallah (Mb) juu ya mifumo ya Serikali ya kupeleka fedha za maendeleo katika halmashauri kwa kuzingatia mifumo, sheria, taratibu na miongozo ambayo husababisha halmashauri kuchelewa kupelekewa fedha mara baada ya bajeti kukamilika, Waziri Mkuu amesema kuwa baada ya Bunge la Bajeti kukamilisha kazi yake, Serikali inawajibika kutekeleza maamuzi ya Bunge kwa kupeleka fedha zilizopangwa kulingana na bajeti hiyo.

Akifafanua suala hilo, Waziri Mkuu amesema kuwa baada ya Bunge kuridhia na kutoa mamlaka ya matumizi ya fedha, Serikali ya Awamu ta Tano ilianza na majukumu muhimu ya kujiridhisha na uwepo wa mifumo sahihi ya makusanyo ya mapato na matumizi yake, kupeleka watumishi watakaosimamia shughuli za usimamizi wa ukusanyaji wa mapato na matumizi yake kwenye halmashauri zote nchini na kuratibu na kutathmini miradi yote iliyokuwa imeanza halafu kutokuendelezwa pamoja na miradi mipya ili kutambua pamoja na thamani zake.

Baada ya kujiridhisha juu ya mambo hayo, Waziri Mkuu amesema kuwa Serikali imeanza kupeleka kwenye halmashauri zote nchini ambapo kufikia mwezi Oktoba kwa mujibu wa Hazina, jumla ya zaidi ya shilingi Bilioni 177 za miradi ya maendeleo zimepelekwa kwenye halmashauri.

Kwa kudhihirisha masuala hayo, Waziri Mkuu amesema kuwa hivi karibuni vyombo vya habari ikiwemo magazeti kwa wiki tatu yameanza kutoa matangazo ya zabuni kutoka kwenye halmashauri mbalimbali juu ya miradi iliyokuwepo na ile inayoendelea na miradi mipya imeanza kutengewa fedha na ambayo imeanza kutangaza kwa ajili ya kuetekeleza miradi hiyo.

Aidha, Waziri Mkuu amewahakikishia wananchi kuwa Serikali itaendelea kupeleka fedha kwenye halmashauri kwa ajili ya shughuli za maendeleo na kuzisisitiza halmashauri ziendelee kukusanya mapato ya ndani ili kuongezea bajeti fedha za Serikali zinazopelekwa na kuongeza kuwa ukusanyaji wa mapato hayo uwe wa mfumo wa kielekroniki ili kudhibiti mapato yanayopatikana.

Akijibu swali la nyongeza juu halmashauri zote kutumia mashine za kielekroniki, Waziri Mkuu amewaagiza Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na Watendaji wote wa Halmashauri wakiwemo Wakurugenzi kuhakikisha kila eneo la makusanyo vifaa vya kielekriniki vinatumika na matumizi ya vifaa hivyo yaendelee ili kuboresha ukusanyaji wa mapato nchini.

Zaidi ya hayo Waziri Mkuu ameendelea kusisitiza kuwa matumizi sahihi ya fedha ambazo zinapelekwa kwenye halmashauri ni lazima zitumike kulingana na malengo yaliyokusidiwa katika kutekeleza miradi iliyoandaliwa kwenye halmashauri na kuwasihi Wabunge wakiwa wajumbe wa baraza la madiwani katika halmashauri zao waendelee kusimamia na kufuatilia matumizi ya fedha zinazopelekwa ili zitekeleze miradi hiyo kikamilifu.

Kuhusu swali la Mbunge wa Ukonga Mwita Witara juu ya Mfuko wa Jimbo, Waziri Mkuu Majaliwa amemhakikishia Mbunge huyo kuwa Serikali haijafilisika, na kusisitiza kuwa suala la Mfuko wa Jimbo bado unatambulika na fedha zitapelekwa kwenye majimbo na wabunge wote watajulishwa ni kiasi gani cha fedha kimepelekwa kwenye majimbo yao ili sheria ziendelee kutumika na kutekelezwa na Mbunge akiwa mwenyekiti wa Mfuko huo anatakiwa kuendelee kuratibu fedha hizo.

Waziri Mkuu amesema kuwa fedha za Mfuko wa Jimbo ni miongoni mwa fedha inayotengwa kwenye Bajeti na kukumbusha kuwa tangu Bunge la bajeti limalize kazi yake miezi mitatu, bado kuna miezi saba ya kutekeleza bajeti hiyo ambapo fedha hizo zitapelekwa kwenye miradi iliyokusudiwa kwenye majimbo mbalimbali nchini.

Kwa upande wa Wafanyabishara kunyanyaswa na Maafisa wa Kodi nchini swali lililoulizwa na Ritha Kabati Mbunge wa Iringoa, Waziri Mkuu amesema kuwa Serikali inaheshimu na kuwathamini wafanyabiashara wote nchini, wawekezaji, wadau na walipa kodi wote wa ndani ya nchi kwa kuzingatia kuwa maendeleo katika nchi yataletwa na sekta ya wafanyabiashara na wawekezaji wakiwa ndio walipa kodi wakubwa nchini.

Kuhusu suala la nidhamu ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Mpato Tanzania (TRA), Waziri Mkuu amewaonya wafanyakazi hao kuwa watumie lugha nzuri na busara wanapokwenda kutimiza majukumu yao kwa kutumia sheria na kanuni na taratibu za kufanya kazi yao.

Kwa upande wa wafanyabiashara, Wairi Mkuu amewataka wafanyabishara hao kutoa taarifa juu ya jambo linalowakwaza kwenye vyombo vya usalama ikiwemo kitengo cha nidhamu kilichopo TRA ili kutafuta dawa sahihi juu ya wafanyakazi ambao hawaendani na nidhamu ya watumishi wa umma.

Swali lingine lililoelekezwa kwa Waziri Mkuu liliulizwa na mbunge wa jimbo la Liwale Zuberi Kuchauka ambalo lilihusu uwepo wa Sera ya wafanyakazi kutoka nje ya nchi (TX) kupitia makampuni mbalimbali, Waziri Mkuu Majaliwa amesema kuwa Sera hiyo bado ipo na Serikali inaisimamia kwa kuzingatia msingi wa kuwapa muda mfupi wataalamu hao wenye ufundi maalumu katika sekta ya kazi ili kujenga wigo mpana kwa Watanzania kupata ajira na kuweza kusimamia maeneo yanayohitaji utaalamu.

“Tumetoa nafasi kwa watumishi wa nchi za nje kuja nchini Tanzania kufanya kazi ambazo hapa ndani sisi tunakosa utaalamu ndio tunafuata msingi huo, tunawapa miaka miwili ya mwanzo, tukiamini Watanzania waambata watakuwa wamejifunza utaalamu ule kwa miaka miwili hadi mitano ambapo baada ya hapo wataalamu wa nje ya nchi wanaweza kuondoka, tunamini Watanzania watakuwa wamepata taaluma hiyo na kusimamia sekta ya kazi” amesisitiza Waziri Mkuu.

Waziri Mkuu amewahakikishia Watanzania kuwa makakati wa Serikali wa kufugua milango ya ajira katika sekta zote ikiwemo utalamu, utaratibu huo utaendelea kusimamiwa wa kupokea utaalamu kutoka nje ambao Tanzania haupo ili kutoa nafasi kwa Wanzania kujifunza.

Kuhusu swali la ruzuku ya pembejeo kwenye sekta ya kilimo kuwafikia wakulima kwa wakati ambalo liliulizwa na Mbunge wa Mbeya vijijini Oran Njeza, Waziri Mkuu amesema kuwa Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imeweka utaratibu wa kusambaza pembejeo nchini kwa kutumia Kampuni ijulikanayo Tanzania Fertilizer Cooperation ili kupeleka mbolea kwa wakulima wakati taasisi nyingine zimepewa kazi kusambaza pembejeo nyingine.

Ili kuhakikisha wananchi wanapata mbolea na pembejeo nyingine kwa wakati, Waziri Mkuu amesema kuwa Serikali imetoa fedhakwa ajili ya kununua pembejeo kwa kampuni hizo na zitatumia mawakala waliopo hadi ngazi za vijiji na kuhakikisha pembejeo hizo zinzwafikia walengwa zinazohitajika katika musimu wa kilimo unapoanza.

Maswali ya papo kwa papo ya Wabunge ambayo huelekezwa kwa Waziri Mkuu yapo kwenye utaratibu kulingana na ratiba ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kila siku ya Alhamisi ili kutoa majibu ya maswali hayo yanayoelekezwa kwenye sekta mbalimbali nchini kwa musatakabali wa kuboresha maisha ya Watanzania na taifa kwa ujumla ili kuwa na maendeleo endelevu ifikapo mwaka 2025 kulingana na Dira ya Maendeleo ya Taifa. 

Uanzishwaji Mahakama ya Mafisadi Kukomesha Rushwa na Uhujumu Uchumi nchini.

Na Eliphace Marwa - Maelezo

Ni mwaka mmoja tangu Serikali ya Awamu ya Tano iingie madarakani na kutekeleza kwa vitendo moja ya ahadi alizozitoa Mgombea Urais wakati ule, Dkt. John Pombe Magufuli ya kuanzisha Mahakama ya Rushwa na Mafisadi.
 

Mahakama ambayo imeanza miezi michache iliyopita inaleta matumaini kwa watanzania hasa wanaipenda nchi yao wakiwa na uzalendo na fikira za kiutaifa. Katika ahadi za TANU, baadae CCM imetamkwa wazi kuwa Rushwa ni adui wa Haki, Sitapokea wala Kutoa Rushwa.

Rais John Pombe Magufuli anatekeleza kwa vitendo anachokiahidi. Leo naomba nizungumzie utekelezaji wa ahadi yake ya kuanzishwa kwa mahakama maalum ya kushughulikia mafisadi na wahujumu uchumi wa nchi yetu.

Ni dhahiri kuwa Dkt. Magufuli anafuata nyayo za muasisi wa Taifa letu, Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambaye alithubutu kukemea na kuwaadhibu viongozi wote wala rushwa.

Mwalimu Nyerere alichukia sana rushwa na alichukua hatua kali sana kwawala rushwa wote bila kujali nyadhifa zao au uwezo wao wa kifedha kwani nakumbuka kuna waziri wake mmoja alihukumiwa kifungo na viboko baada ya kupatikana na hatia ya kula rushwa .

Watumishi wa umma, waliohusika na ufisadi walichukuliwa hatua kali ikiwa ni pamoja na kufungwa jela na kufilisiwa mali zao na hiyo ilipunguza sana rushwa na ifisadi serikalini. Mwalimu aliamini kwamba mtu hawezi kupanda farasi wawili kwa wakati mmoja na alikuwa sahihi kabisa. Kitendo cha kuruhusu wafanyabiashara kuingia kwenye siasa, na viongozi kuruhusiwa kufanya biashara ndio chanzo cha wizi na ufisadi wa mali na fedha za umma.

Katika hotuba ya kufungua Bunge la 11 mjini Dodoma Novemba 20,2015, Rais  Magufuli jambo moja alilolisitiza na kulisemea kwa nguvu ni juu ya ahadi yake wakati wa kampeni ya mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi.

“Sikufanya hivyo kwa sababu nilitaka tu kuwarubuni wananchi ili wanipe kura zao na kunifanya kuwa Rais wao. Nililiongea jambo hili kwa dhati kabisa, na nilichokisema na kuwaahidi wananchi ndicho hasa nilichokikusudia”, alisema Dkt. Magufuli.

Ni kweli kuwa wananchi wanachukia sana rushwa na ufisadi, na wamechoshwa na vitendo hivyo na hata yeye pia anachukia rushwa na ufisadi na wala hafurahishwi kabisa na vitendo vya rushwa na ufisadi vinavyoendelea hapa nchini kwani vitendo hivyo vinawanyima haki wananchi na kuitia hasara serikali kwa mamilioni ya fedha ambazo zingeweza kutumika kwa ajili ya kujenga miradi ya maendeleo..

Rais Magufuli aliongeza kuwa Chama chake, Chama cha Mapinduzi, kimejengwa katika misingi ya kukataa rushwa na ufisadi na ndiyo maana moja ya Imani kuu za CCM ni ile isemayo, “Rushwa ni adui wa haki, sitatoa wala kupokea rushwa” na hivyo Mtanzania mwaminifu kwa imani yake hatakuwa na kigugumizi katika kuwa mstari wa mbele katika kupambana na rushwa na ufisadi.

Rais Magufuli alimnukuu Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, kuwa aliwahi kuifananisha rushwa na ufisadi ‘Kama Adui Mkubwa wa Watu’.

Akiongea Bungeni Mei 1960, Mwalimu Nyerere alisema yafuatayo kuhusu rushwa, “Rushwa [na ufisadi] havina budi kushughulikiwa bila huruma kwa sababu naamini wakati wa Amani rushwa na ufisadi ni adui mkubwa kwa ustawi wa watu kuliko vita.”

Haya ni maneno makali ya mtu na kiongozi aliyeichukia na kuikemea rushwa katika maisha yake yote ya uongozi. Ni maneno yanayotukumbusha tu nini kinaweza kikatutokea kama taifa endapo tutaendekeza rushwa na ufisadi. Chuki za wananchi dhidi ya rushwa na ufisadi ni dhahiri. Watanzania wamechoka kabisa, wamechoka sana, hawako tayari kuvumilia serikali inayoonea haya rushwa na kulea mafisadi.

“Nimewaahidi wananchi, na nataka niirejee ahadi yangu kwao mbele ya Bunge lako tukufu, kwamba nitapambana na rushwa na ufisadi bila kigugumizi na bila haya yoyote na Dawa ya jipu ni kulitumbua, na mimi nimejipa kazi ya kuwa mtumbua majipu. Najua kutumbua jipu kuna maumivu lakini bahati mbaya halina dawa nyingine, hivyo ninaomba Waheshimiwa Wabunge na Watanzania wote mniombee na mniunge mkono wakati natumbua majipu haya”, aliongeza Rais Magufuli.

Aidha, katika siku ya kilele cha Wiki ya Mwaka Mpya wa Mahakama Jijini Dar es Salaam mapema mwaka huu, Rais Magufuli alimtakia Jaji Mkuu, Othman Chande kutosubiri Bunge kupitisha Sheria ya Uanzishwaji wa Mahakama ya Mafisadi, badala yake mahakama hiyo ianze kufanya kazi haraka iwezekanavyo.

Alisema kuchelewesha kuanza kwa mahakama hiyo kunatoa mwanya kwa mafisadi kuendelea kuangamiza nchi na kuifanya kuwa masikini wakati ina rasilimali za kutosha ambazo zinaweza kuiendesha nchi bila kutegemea fedha za wafadhili.

Rais Magufuli alisisitiza umuhimu wa uanzishwaji wa mahakama hiyo ambayo alitaka ifanye kazi ndani ya mahakama kuu kama zilivyo Mahakama za Ardhi na Biashara.

Akifunga maadhimisho hayo, Rais Magufuli alisema azma yake ni kuona nchi inakuwa na uchumi mzuri ambao utamnufaisha kila mtanzania na rasilimali zilizopo badala ya kumilikiwa na watu wachache.

Tamko la kuanza kazi kwa Mahakama hiyo lilitolewa bungeni na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Ofisi yake.

“Kuhusu ahadi ya kuanzisha Mahakama Maalum ya Ufisadi napenda kuliarifu Bunge lako kwamba, Serikali imeanzisha Divisheni ya Mahakama ya Rushwa na Ufisadi katika Mahakama Kuu itakayoanza kufanya kazi mwezi Julai 2016,” alisema Majaliwa.

Aidha, Waziri Mkuu alisema pia Serikali itaimarisha Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ili kwa pamoja ziweze kuharakisha utoaji wa haki kwa kesi zitakazofikishwa kwenye mahakama hiyo.

Akizungumza Bungeni Majaliwa alisema katika jitihada za kukabiliana na changamoto ya uhaba wa majengo ya mahakama na vitendea kazi katika ngazi zote, Rais Magufuli ametekeleza ahadi yake aliyoitoa Februari 4, mwaka huu ya kutoa fedha za maendeleo ya mahakama Sh. bilioni 12.3.

Alisema hatua hiyo imewezesha mahakama kuendelea na ukarabati na ujenzi wa mahakama katika ngazi mbalimbali pamoja na ununuzi wa vitendea kazi kwani Serikali imedhamiria kupunguza kero ya mlundikano wa mashauri mahakamani ili wananchi wapate haki kwa wakati.

Katika kufanikisha dhamira hiyo, Waziri Mkuu alisema Serikali imeimarisha  utendaji wa mhimili wa mahakama kwa kuongeza rasilimali watu na fedha.

“Serikali pia imeboresha na kuongeza ufanisi katika upelelezi na uendeshaji wa mashauri kwa kutenganisha jukumu la upelelezi na uendeshaji mashuari kwa majaji na mahakimu kujiwekea utaratibu wa kuwa na malengo ya idadi ya mashauri ambayo wanapaswa kuyasikiliza kila mwaka,” alisema Majaliwa.

Aidha Tarehe 24 Juni 2016 Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipitisha kwa kauli moja Sheria ya Marekebisho Mbalimbali, ambayo pamoja na mambo mengine, yamempa Jaji Mkuu mamlaka ya kuanzisha Divisheni ya Rushwa na Uhujumu Uchumi ya Mahakama Kuu.

Kwa mujibu wa muswada huo uliowasilishwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju, adhabu kwa watakaokutwa na hatia zimeongezwa, huku mahakama hiyo ikiwekewa mazingira wezeshi ili iendeshe kesi hizo kwa haraka.

Muswada huo wa sheria ambao kwa sasa utakuwa ukisubiri Rais ausaini ili iwe sheria kamili, umekusudia kuanzisha divisheni hiyo ya mahakama, ambayo itakuwa na majaji wake na watumishi wake wanaojitegemea.

“Divisheni Maalumu ya Mahakama Kuu, itakuwa na majaji pamoja na watumishi wengine, ambao wanahusika moja kwa moja na kesi za rushwa na uhujumu uchumi tu, hatua hii itawezesha kesi za makosa ya rushwa na uhujumu uchumi kusikilizwa kwa urahisi, ufanisi na kwa haraka,” alisema Masaju wakati alipokuwa akisoma muswada huo kabla ya kupitishwa na Bunge.

Hatua hiyo ya kuwa na majaji maalumu na wafanyakazi wake, Masaju alisema imelenga kuondoa udhaifu uliojitokeza wakati wa kushughulikia kesi za rushwa na uhujumu uchumi, kwa kuwa majaji waliokuwa wakisikiliza mashauri hayo, walikuwa hao hao wanaosikiliza mashauri mengine ya jinai, madai, katiba na mengine yanayofunguliwa Mahakama Kuu.

Kwa mujibu wa Masaju, hali hiyo ilisababisha uendeshaji wa kesi za rushwa na uhujumu uchumi, kutokuwa na tofauti na uendeshaji na usikilizwaji wa kesi zingine.

Aidha Masaju aliongeza kuwaMazingira mengine wezeshi yanayotengenezwa na sheria hiyo kwa divisheni hiyo, ni thamani ya fedha inayohusishwa na makosa hayo, kuwa inaanzia Sh bilioni moja.

“Inapendekezwa kuwa pale makosa ya rushwa na uhujumu uchumi yanapohusisha thamani ya fedha, basi makosa yatakayofunguliwa katika Mahakama Kuu, Divisheni ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, yawe ni yale ambayo thamani yake haipungui Sh bilioni moja,” alisema Masaju.

Lengo la kuweka thamani hiyo ya fedha, limeelezwa kuwa ni kuiwezesha divisheni hiyo kujikita kusikiliza makosa makubwa ya rushwa na uhujumu uchumi, ili makosa madogo yasiyofikia thamani hiyo, yasikilizwe na mahakama za wilaya, mahakama za hakimu mkazi na Mahakama Kuu.

Hata hivyo, divisheni hiyo pia kwa mujibu wa sheria hiyo itasikiliza makosa mengine ya rushwa na uhujumu uchumi bila kujali thamani ya fedha, kutokana na namna makosa hayo yalivyotendeka, asili yake na ugumu wa kuyawekea thamani ya fedha.

Pia, Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) amepewa mamlaka ya kutoa hati ambayo itataka mashauri mengine yatakayofunguliwa, yasikilizwe katika divisheni hiyo kwa maslahi ya umma.

Marekebisho mengine yaliyopendekezwa ni pamoja na makosa ya rushwa na uhujumu uchumi chini ya sheria hii iwe ni kifungo cha gerezani, kisichopungua miaka 20 na kisichozidi miaka 30 au vyote kwa pamoja na hatua nyingine za kijinai, ikiwa ni pamoja na kutaifisha mali zilizopatikana kutokana na makosa hayo.

Kifungo hicho kimeongezwa kutoka katika sheria ya sasa ambayo ndiyo inayorekebishwa, ambayo ilitaka kifungo kisizidi miaka 15. Kwa mujibu wa Masaju, maneno hayo “kifungo kisichozidi miaka 15”, yaliipa Mahakama mamlaka ya kutoa adhabu ndogo zaidi, ilimradi tu adhabu hiyo haizidi miaka 15, jambo lililoonekana kuwa baadhi ya adhabu zilikuwa ndogo kuliko uzito wa makosa.

Katika kutaifisha mali za waliokutwa na hatia, sheria hiyo imeweka masharti ya kuzuia kutumika kwa sheria zinazohusu ufilisi au uamuzi wa kufilisi kampuni, kwa mali ambayo inachunguzwa chini ya Sheria ya Makosa ya Uhujumu Uchumi.

“Marekebisho hayo yanalenga kukabili vitendo vya watu au kampuni kujifilisisha wakati uchunguzi unapoanza dhidi yao na pia kuhakikisha kuwa mali zote zinazohusika na kosa linalochunguzwa, au linaloendelea mahakamani, inaendelea kuwepo hadi uchunguzi au kesi husika itakapohitimishwa,” alisema Masaju.

Hatua hiyo imetajwa kuwa na nia ya kuiwezesha serikali kutaifisha mali hiyo, wakati kesi husika itakapokamilika na ikathibitika kuwa ina uhusiano na kosa la rushwa na uhujumu uchumi lililothibitishwa mahakamani.

“Kwa ujumla hatua hii ni njia mojawapo ya kuwafanya watu waogope kutenda makosa ya rushwa na uhujumu uchumi na pia kuhakikisha kuwa mhalifu, hanufaiki na uhalifu alioutenda kwa kutaifisha mali zilizopatikana kwa njia ya rushwa, ufisadi na uhujumu uchumi,” alisema Masaju.

Hata hivyo Masaju aliongeza kuwa Marekebisho mengine yaliyoingia katika sheria hiyo, yanahusu ulinzi wa mashahidi, ambapo Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), kwa kushauriana na Mkurugenzi wa Mashitaka, wanatakiwa kuweka utaratibu wa kuhakikisha usalama wa shahidi pamoja na familia yake ikiwa na lengo ni kusaidia usalama wa mashahidi wa kesi hizo, ili mashahidi wawezeshwe kutoa ushahidi wao bila woga, kwa kuwa kesi hizo zinahusisha watu wenye fedha na makosa yanayofanyika ni ya kupanga.

Awali Rais Magufuli alipoahidi kuanzisha mahakama hiyo, wengi walichukulia kama ni suala lisilowezekana, lakini kasi yake ya kusimamia suala hilo, imewafanya baadhi ya mafisadi waingiwe na kihoro na kuanza kutafuta njia za kujinusuru ikiwemo kutoroka nchini.

Mpaka sasa serikali ya Awamu ya Tano katika kipindi cha mwaka mmoja imefanikiwa kufungua majalada zaidi ya 300 yanayohusiana na kesi mbalimbali za ufisadi ambayo yako mezani kwa Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) ikiwa ni sehemu ya hatua muhimu kabla ya kufikishwa mahakamani.

PSPF YAONGEZA WANACHAMA WAPYA 50,185 KWA KIPINDI CHA MWAKA MMOJA.

Na Tiganya Vincent-MAELEZO- Dar es salaam.

Novemba 5, mwaka huu ni mwaka mmoja tangu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli alioapishwa kuwa kiongozi na Amri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama wa nchi hii.

Katika kipindi cha mwaka mmoja cha utawala wa Rais Magufuli nchini, Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) kwa upande wake umesaidia Watanzania wanaopata huduma za Jamii kupitia PSPF kuongezeka kutoka 394,494 hadi kufikia 444,679 ikiwa ni sehemu ya utekeleza wa agizo lake. 

Hatua hii ya PSPF imelenga kutekeza agizo na kutimiza ahadi ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyokuwa akitoa ya kuhakikisha kuwa Watanzania wengi wanufaika na huduma za Hifadhi za Jamii ikiwemo huduma za Bima za afya wakati wa kampeni na baada ya kuingia madarakani.

Kwa mujibu wa taarifa ya mwaka mmoja kwa upande wa Mfuko wa PSPF iliyotolewa na Costantina Martin kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa PSPF ,idadi hiyo hii inajumuisha Watanzania walio katika sekta rasmi na isiyo rasmi nchini. 

Kundi hili kubwa lilikuwa limesaulika kujumuishwa katika hifadhi ya jamii , lakini baada ya Mhe. Rais Magufuli kulizungumzia katika kampeni zake hivi sasa mwamko wa kujiunga na hifadhi ya jamii umeongezeka na PSPF imeanza kulitekeleza agizo hilo kwa kuwahamasisha wananchi waliopo katika sekta isiyo rasmi na sekta rasmi kuchangia na kujiunga katika Bima ya Afya.
 
Katika kuhakikisha kuwa azma hiyo inatimizwa tayari PSPF imeingia makubaliano na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF) kwa lengo la kufikisha huduma za afya kwa watanzania wengi ambao wapo katika sekta isyo rasmi na hivyo kujenga jamii yenye afya bora inayochangia katika ujenzi wa nchi.

Chini ya makubaliano yanawasaidia wanachama wa PSPF walio katika Mpango wa Uchangiaji wa Hiari kuweza kupata ya tiba kupitia NHIF kwa gharama ya shilingi 76,800/- kwa mwaka katika hospitali mbalimbali ziliingia makubaliano na Mfuko huo wa Bima ya Afya.Mpango huo wa PSPF unaounga mkono juhudi za Rais Magufuli za kutaka kuhakikisha kuwa wananchi wengi wanapata huduma na matibabu nchi nzima kwenye vituo vyote vilivyosajiliwa na NHIF kuanzia Zahanati hadi Hospitali ya Taifa kwa gharama nafuu.

Hivi sasa huduma hiyo ya PSPF kuwadhamini wananchama wake kwa ajili ya kupata matibabu imesaidia watanzania wengi sana kunufaika na huduma hii husasan katika kipindi cha mwaka mmoja wa Rais Magufuli.Akifungua rasmi Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Rais Magufuli alisema kuwa dhamira ya kujenga uchumi wa kisasa na suala la kupambana na umaskini linakwenda sambamba na kuwa na wananchi wenye afya bora.

Aliongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Tano itahakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya kwa kuhamasisha wananchi wengi wanajiunga na Bima ya Afya.Katika kutekeleza hilo PSPF kwa kushirikiana na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF) imeshawafikia Watanzania 2,710 walio katika sekta isiyo rasmi kuanza kunufaika na huduma za Afya kupitia PSPF.Mbali na sekta ya afya , katika kipindi cha mwaka mmoja wa Rais Magufuli PSPF kwa upande wake imesaidia kuhakikisha kuwa Tanznaia inakuwa Nchi ya Viwanda kwa lengo la kutoa ajira kwa Watanzania walio wengi.

Viwanda hivyo ambavyo PSPF imewekeza ni pamoja na 21st Century cha Morogoro, Saruji Tanga.Martin ameongeza kuwa hivi sasa PSPF imejipanga kuwekeza katika Kituo cha Biashara cha Kurasini (Kurasini Logistic Center) kwa lengo la kuchochea uwekezaji wa viwanda na kutoa ajira kwa wananchi.

Viwanda vingine ambavyo PSPF imejipanga kuwekeza ni kile cha Nguo cha Urafiki, Morogoro Canvas Mill na Kiwanda cha Viatu Karanga kilichopo Moshi.Hatua hiyo iliyoanza kutekelezwa na PSPF ni sehemu utekelezaji hotuba ya Mhe. Rais Magufuli wakati anafungua rasmi Bunge 11 mjini Dodoma mwishoni mwa mwaka jana ambapo alisema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano itaweka mkazo katika ujenzi wa viwanda ili mwaka 2020 idadi ya ajira itokanayo na viwanda ifikie asilimia 40 ya ajira zote hapa nchini.

PSPF ilianzishwa kwa sheria ya Mafao ya Hitimisho la Kazi kwa Watumishi wa Umma namba 2 ya mwaka 199 . sura ya 371 na inatoa huduma za Hifadhi ya Jamii katika Mapngo wa lazimana wa hiyari.

DC MTATURU AZINDUA UHABARISHO WA MAFUNZO YA KUIJENGEA UWEZO JAMII KATIKA KUIBUA NA KUPANGA MIRADI YA MAENDELEO


Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu aliyesimama akisisitiza jambo wakati wa uzinduzi wa Mradi wa kuijengea jamii uwezo katika kuibua na kutekeleza mpango shirikishi
Madiwani, na Wakuu wa Idara na Vitengo wakisikiliza kwa makini maelezo kuhusu walengwa wa Mradi wa kuijengea jamii uwezo katika kuibua na kutekeleza mpango shirikishi
Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Ally Juma Mwanga, na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Bi Rustika Turuka
Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akisikiliza kwa makini maelezo kuhusu mradi huo
Madiwani,Wakuu wa Idara na Vitengo wakisikiliza kwa makini maelezo ya Mradi wa kuijengea jamii uwezo katika kuibua na kutekeleza mpango shirikishi

Na Mathias Canal, Singida.

Shirika la Health Actions Promotion Association (HAPA) la Mkoani Singida kwa ushirikiano na Shirika la The Foundation For Civil Society la Jijini Dar es salaam linatarajia kuendesha mradi wa miaka mitatu kwa vijiji vyote vya Wilaya ya Ikungi kwa lengo la kuijengea jamii uwezo na mbinu shirikishi kama fursa na vikwazo katika maendeleo.

Mradi huo utaanza na Vijiji 10 vya majaribio (Pilot Villages) kutoka katika kata nne na kila kata itakuwa na Vijiji ama viwili ama Vitatu ambapo uchaguzi wa Vijiji hivyo vya majaribio umezuingatia utayari wa jamii husika katika shughuli za maendeleo pamoja na gharama za uendeshaji wa mradi ili kupata matokeo chanya kwa uendelezaji wa mradi husika.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu amesema kuwa Uongozi wa Wilaya hiyo unaendelea kushirikisha wadau mbalimbali katika kusaidia kutekeleza shughuli za maendeleo, kwani kwa uhabarisho wa mafunzo ya kujenga uwezo wa jamii na Halmashauri yataendelea katika kuimarisha juhudi za Wilaya zinazoendelea kuchukuliwa katika kutekeleza miradi ya maendeleo pia itakuwa ni fursa kwa jamii kuwa na Uwezo na Nyenzo muhimu katika kutekeleza miradi ya maendeleo kwa ufanisi.

Amesema kuwa Wilaya ya Ikungi inakabiliwa na changamoto mbalimbali za kujiletea maendeleo ambapo endapo zitapatiwa upembuzi yakinifu zitapunguza kadhia zinazowakumba wananchi ambapo amezitaja changamoto hizo ikiwa ni pamoja na Ujenzi wa Vituo vya Afya na Zahanati (Kata na Vijiji) ambapo kwa sasa Wilaya ina vituo 39 tu vya kutolea huduma za Afya ambapo upungufu ni Asilimia 60, Ujenzi na Uboreshaji wa miundombinu ya shule za msingi ambapo kuna nyumba za walimu 387 ambapo upungufu ni nyumba 854, Ujenzi na Uboreshaji wa majosho na mifugo kwani kwa sasa yapo majosho 30 huku kati ya hayo majosho 20 ni mabovu.

Dc Mtaturu alisema kuwa Zipo Asasi mbalimbali ambazo zimesajiliwa kwa lengo la kutoa elimu kwa wananchi lakini zimegeuka na kuwa Asasi zinazofanya kazi za kisiasa tofauti na usajili wao ambapo amesema serikali haitasita kuzichukulia hatua ikiwemo kuzifuta Asasi hizo ili ziache kupotosha wananchi.

Dc Mtaturu alisema kuwa Mradi huo unaotolewa na Shirika la HAPA ni lazima uzingatie matakwa ya kutoa elimu kwa wananchi ili wafahamu kuwa wana nafasi kubwa ya kufanikisha maendeleo yao katika jamii hivyo waache kupotoshwa na baadhi ya wanasiasa kuwa maendeleo yataletwa na serikali pekee.

Msimamizi wa Mradi wa HAPA Noel Makyao amewataja walengwa wa Mradi huo kuwa ni wananchi wote wa kijiji cha Mradi wa majaribio, Wawakilishi 100 kutoka kila kijiji ambao watachaguliwa ili kuendesha zoezi la kutengeneza bajeti ya mpango wa kila mradi ulioibuliwa na jamii kwa siku tatu mfululizo na watu mashuhuri, wakuu wa madhehebu ya dini na makundi mengine wapatao 20.

Alisema kuwa Jumla ya gharama zote za kutekeleza mradi wa mbinu shirikishi ya kujenga uwezo wa jamii katika kuibua, Kupanga, Kutekeleza na kupima matokeo ya Mradi katika vijiji kumi vya majaribio kwa robo mbili zitakuwa shilingi milioni hamsini (50,000,000/=).

Makyao alisema katika awamu hii ya vijiji kumi vya majaribio jumla ya watu wapatao 25,511 watafikiwa kati ya lengo la watu 25,334 zaidi ya watu 177 ya walengwa wa mradi.

MKUU WA MKOA WA ARUSHA AAHIDI KUWAINUA WASANII WA FILAMU


Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo akizungumza na makundi ya vijana wajasiriamali na wasanii wa Filamu jijini Arusha.Amesema fani hiyo ni muhimu katika kuhamasisha maendeleo na kujenga mshikamano.

Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Arusha,Rebeca Mongy akizungumza juu ya mipango waliyonayo kuwawezesha vijana kujikwamua kiuchumi,kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo na kulia Mkuu wa Idara ya maendeleo ya Jamii Jiji la Arusha,Tajiel Mahega.

Mkuu wa Idara ya maendeleo ya jamii Jiji la Arusha,Tajiel Mahega akizungumza katika mkutano huo.

Mwenyekiti wa chama cha Waigizaji na Filamu mkoa wa Arusha(TDFAA)Isack Chalo.
Burudani ikiendelea kutolewa na kikundi cha Sarakasi.
Burudani ikiendelea kutolewa na kikundi cha Sarakasi.

DC MTATURU AZINDUA UHABARISHO WA MAFUNZO YA KUIJENGEA UWEZO JAMII KATIKA KUIBUA NA KUPANGA MIRADI YA MAENDELEO

 Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu aliyesimama akisisitiza jambo wakati wa uzinduzi wa Mradi wa kuijengea jamii uwezo katika kuibua na kutekeleza mpango shirikishi.

Na Mathias Canal, Singida

Shirika la Health Actions Promotion Association (HAPA) la Mkoani Singida kwa ushirikiano na Shirika la The Foundation For Civil Society la Jijini Dar es salaam linatarajia kuendesha mradi wa miaka mitatu kwa vijiji vyote vya Wilaya ya Ikungi kwa lengo la kuijengea jamii uwezo na mbinu shirikishi kama fursa na vikwazo katika maendeleo.

Mradi huo utaanza na Vijiji 10 vya majaribio (Pilot Villages) kutoka katika kata nne na kila kata itakuwa na Vijiji ama viwili ama Vitatu ambapo uchaguzi wa Vijiji hivyo vya majaribio umezuingatia utayari wa jamii husika katika shughuli za maendeleo pamoja na gharama za uendeshaji wa mradi ili kupata matokeo chanya kwa uendelezaji wa mradi husika.
 Madiwani, na Wakuu wa Idara na Vitengo wakisikiliza kwa makini maelezo kuhusu walengwa wa Mradi wa kuijengea jamii uwezo katika kuibua na kutekeleza mpango shirikishi

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu amesema kuwa Uongozi wa Wilaya hiyo unaendelea kushirikisha wadau mbalimbali katika kusaidia kutekeleza shughuli za maendeleo, kwani kwa uhabarisho wa mafunzo ya kujenga uwezo wa jamii na Halmashauri yataendelea katika kuimarisha juhudi za Wilaya zinazoendelea kuchukuliwa katika kutekeleza miradi ya maendeleo pia itakuwa ni fursa kwa jamii kuwa na Uwezo na Nyenzo muhimu katika kutekeleza miradi ya maendeleo kwa ufanisi.

Amesema kuwa Wilaya ya Ikungi inakabiliwa na changamoto mbalimbali za kujiletea maendeleo ambapo endapo zitapatiwa upembuzi yakinifu zitapunguza kadhia zinazowakumba wananchi ambapo amezitaja changamoto hizo ikiwa ni pamoja na Ujenzi wa Vituo vya Afya na Zahanati (Kata na Vijiji) ambapo kwa sasa Wilaya ina vituo 39 tu vya kutolea huduma za Afya ambapo upungufu ni Asilimia 60, Ujenzi na Uboreshaji wa miundombinu ya shule za msingi ambapo kuna nyumba za walimu 387 ambapo upungufu ni nyumba 854, Ujenzi na Uboreshaji wa majosho na mifugo kwani kwa sasa yapo majosho 30 huku kati ya hayo majosho 20 ni mabovu.

Dc Mtaturu alisema kuwa Zipo Asasi mbalimbali ambazo zimesajiliwa kwa lengo la kutoa elimu kwa wananchi lakini zimegeuka na kuwa Asasi zinazofanya kazi za kisiasa tofauti na usajili wao ambapo amesema serikali haitasita kuzichukulia hatua ikiwemo kuzifuta Asasi hizo ili ziache kupotosha wananchi.
 Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Ally Juma Mwanga, na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Bi Rustika Turuka

Dc Mtaturu alisema kuwa Mradi huo unaotolewa na Shirika la HAPA ni lazima uzingatie matakwa ya kutoa elimu kwa wananchi ili wafahamu kuwa wana nafasi kubwa ya kufanikisha maendeleo yao katika jamii hivyo waache kupotoshwa na baadhi ya wanasiasa kuwa maendeleo yataletwa na serikali pekee.

Msimamizi wa Mradi wa HAPA Noel Makyao amewataja walengwa wa Mradi huo kuwa ni wananchi wote wa kijiji cha Mradi wa majaribio, Wawakilishi 100 kutoka kila kijiji ambao watachaguliwa ili kuendesha zoezi la kutengeneza bajeti ya mpango wa kila mradi ulioibuliwa na jamii kwa siku tatu mfululizo na watu mashuhuri, wakuu wa madhehebu ya dini na makundi mengine wapatao 20.

Alisema kuwa Jumla ya gharama zote za kutekeleza mradi wa mbinu shirikishi ya kujenga uwezo wa jamii katika kuibua, Kupanga, Kutekeleza na kupima matokeo ya Mradi katika vijiji kumi vya majaribio kwa robo mbili zitakuwa shilingi milioni hamsini (50,000,000/=).

Makyao alisema katika awamu hii ya vijiji kumi vya majaribio jumla ya watu wapatao 25,511 watafikiwa kati ya lengo la watu 25,334 zaidi ya watu 177 ya walengwa wa mradi.
 Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akisikiliza kwa makini maelezo kuhusu mradi huo
Madiwani,Wakuu wa Idara na Vitengo wakisikiliza kwa makini maelezo ya Mradi wa kuijengea jamii uwezo katika kuibua na kutekeleza mpango shirikishi.

MAFANIKIO YA MWAKA MMOJA WA MAGUFULI KATIKA SEKTA YA USAFIRISHAJI

Benjamin Sawe-MAELEZO

Katika kipindi cha mwaka mmoja wa uongozi wa Serikali ya Awamu ya Tano kumefanyika jitahada kubwa za kuhakikisha inafufua mashirika yalifikia hali mbaya na kushindwa kutoa huduma ili hatimaye yaanze upya kutoa mchango wa ujenzi wa uchumi nchi. Mojawapo wa Mashirika hayo ni pamoja na Kampuni ya Ndege ya Tanzania (ATCL) ambapo kabla ya Rais Magufuli kuingia madarakani lilikuwa na Ndege mmoja tu.

Hatua hiyo ya Rais Magufuli kuamua kununua Ndege mbili aina ya Bombadier Q400 zimesaidia kuimarisha Kampuni hiyo na kurejesha nembo ya Twiga iliyoanza kupotea. Licha ya juhudi hizo na kazi mkubwa aliyoifanya Rais Magufuli ya kutimiza ahadi yake ya kuanza kuijenga upya Kampuni hiyo, wapo baadhi ya wananchi wachache ambavyo wamewakuwa hawana shukurani na kuanza kubeza jitihada hizo.

Ni vema wakumbe ule usemi unaotumiwa na baadhi ya watu kuwa “ Hata mbuyu ulianza kama mchicha” .Kauli hii inadhihirisha kuwa kila jambo uwa na mwanzo wake kwani tokana na dhihaka za baadhi ya watu ambao wamekuwa wakibeza juhudi za Mhe. Rais Magufuli. Ununuzi wa Ndege hizo umesaidia kumeimarisha huduma za usafiri wa anga na kuongeza ushindani katika utoaji wa huduma za anga hapa nchini kati yake na kampuni binafsi za ndege zinazotoa huduma hiyo kwa sasa

Azma hiyo ya Serikali ya kununua ndege mpya imetimiza ahadi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.John Pombe Magufuli wa kulifufua tena Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) na kulipatia mtaji ili lianze upya kutoa huduma hiyo kwa Watanzania. Akizindua ndege hizo Rais Magufuli alisema kuwa ,ndege hizo zina sifa ya matumizi madogo ya mafuta na ni suluhisho la kupanda kwa bei ya usafiri wa anga nchini na pia zitasaidia kukuza sekta ya utalii nchini.

“Ndege hizi zinatumia wastani wa mafuta ya shilingi milioni moja kutoka hapa hadi Songea, wakati ndege za Jet zinatumia mafuta ya shilingi milioni 28.1 kwa safari kama hiyo,” anasema Mheshimiwa Rais. Ukitaka kujenga nchi yenye uchumi wa kisasa huwezi kujenga bila kuwa na ndege na ukitaka watalii lazima uwe na ndege.

“Tunataka watalii wanaokuja nchini kuja moja kwa moja bila kushuka nchi nyingine ili kuongeza mapato yetu na kukuza utalii duniani na kuwa na ndege nyingi zaidi kama nchi nyingine” anasema Rais Magufuli. Mbali na kuleta ndege hizo, yapo mambo mengi makubwa ambayo Rais Magufuli ameanza kuyatekeleza, aliyoahidi wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu mwaka jana, hatua ambayo imewavutia watu wengi ndani na nje ya nchi.

Aidha WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa leo alizindua awamu ya kwanza ya upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Dodoma ili uweze kupokea ndege kubwa za mizigo, abiria na viongozi wa kitaifa na kimataifa. Uzinduzi huo ni miongoni mwa maandalizi ya kutimiza azma ya kuufanya mkoa wa Dodoma kuwa Makao Makuu ya Tanzania. Ujenzi huo umegharimu Sh bilioni 11.5 ambazo ni fedha za ndani na utatoa fursa kwa mashirika ya ndege kuanza huduma Dodoma, ikiwemo ndege ambazo zimenunuliwa na serikali.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Jordan Rugimbana anasema, uzinduzi huo hautaathiri mchakato wa kujenga Uwanja wa Ndege wa Kimataifa eneo la Msalato. “Mchakato wa ujenzi wa uwanja wa ndege Msalato uko pale pale,” anasema Rugimbana na kuongeza kuwa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano imeamua kufanya upanuzi wa uwanja huo ili ndege kubwa zitue mkoani humo.

‘’Wizara ya Ujenzi imeamua kufanya upanuzi wa uwanja wetu wa ndege wa Dodoma ili  ndege kubwa ziweze kutua na sisi tunamshukuru Rais kwa kutupa uwanja huo kwani utazidi kufungua fursa katika mkoa wetu,” anaeleza Rugimbana.